[QUOTE
Nyani Ngabu;
1. Kutembea nje ya ndoa au niseme usaliti, uwe wa kihisia au kimwili. Hili kwangu halina mjadala kabisa. If I find out you're two-timing on me, we are through. I call it one strike and you're out policy.
2. Physical violence. Ukinitwanga na frying pan kichwani au ukinitandika chupa ya Balimi usoni, kutakuwa hakuna tena ndoa hapo. Kwa sababu nita-swing for the fences, and if I connect, lights out. Lose-lose situation there.
3. Vices nyingine kama ulevi usio wa kupindukia, uvutaji sigara, matumizi mabaya ya pesa, uvivu wa kufanya kazi, kuvaa nguo kama hoochie mama, kutumia lugha chafu chafu, uchafu wa mwili na mazingira, ili mradi tu hazijavuka mipaka na kuwa kero ambazo siwezi kuzivumilia, nadhani ni vitu ambayo mimi na yeye tunaweza kukaa chini, tukavijadili, na kukubaliana namna ya kuvikabili na kuvirekebisha.
Lakini watu tumetofautiana. Wapo ambao hata wachitiwe namna gani bado watang'ang'ana kupigania ndoa zao. Wengine hata wawe wananyanyaswa kiasi gani, iwe kihisia au kwa kupigwa bado tu watang'ang'ana.
Well, siwezi kuwakosoa sana maana huo ni uamuzi wao. Lakini huwa siamini katika upuuzi wa kudhani kuwa kwa vile tu mtu uko kwenye ndoa na kwa vile labda mna watoto basi ndo uendelee kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga.
Kufanya hivyo (kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga) ni kuwa mpuuzi na mjinga. Hata kama kuna watoto, hiyo haina maana ndo ushikwe mateka katika ndoa yenye kila aina ya manyanyaso.
Inafika wakati mtu unaweka mguu wako chini, unachora mstari na kusema 'sasa basi, imetosha'. Unasepa unaenda kuendelea na maisha yako.
Mtoa mada
Realme;
Mimi siafiki kikubwa na ushauri uliotolewa na
Nyani Ngabu kwa vile nadhani uchambuzi wake sio mpana vya kutosha. Hapa nitaeleza kwanini nahisi ushauri huu hautatatua tatizo lako. Tuanze na wanaovunja ndoa zaidi duniani.
1. Nchi kumi zinazoongoza kwa kuvunjika ndoa duniani ni hizi hapa
Countries with Highest Divorce Rates - World Top Ten
Hamna nchi yoyote ya kiafrika. Kabla yeyote hajarukia kuwa Afrika haipo kwa vile ni masikini basi azonagatie kuwa Japan, Ujerumani, China, Marekani hawamo. Katika hizi kumi nyingi ni za ulaya kaskazini na haswa Scandinavia. Hapa la maana ni kwamba kuwa zile nchi zenye kuenzi tamaduni zao, basi hazimo katika kumi bora. Kinachofanana katika nchi hizi ni kule kuaminishwa sana na social media zao kama vile kuolewa ni utumwa. Hawa wanavunjiwa ndoa na social media. Sio culture. Hapa kwetu kudumisha ndoa yako kunaegemea sana umelelewa vipi (zamani ilikuwa kuwekwa ndani 1-2 months, ikazomewa ikapuuzwa, leo inaitwa kitchen party-1 day). Curricular zinafanana ila muda hautoshi (1 day) kwa wanafunzi wa enzi zetu.
2. Hebu tuangalie sababu kubwa zinazovunja ndoa nyingi SIKU HIZI(nachukua mfano toka Afrika Kusini)
Marriage Counselling- combatting SA’s high divorce rate «
Utaona kuwa sumu nambari moja ni
Financial stress and Pressure, ikifuatiwa na SOCIAL MEDIA> Baada ya hapo ndipo unakuta Ku-cheat, Addiction na kama Lack of Communication.
Hapa kwenye Social media lazima uweke aina zote ya mawasiliano. Anzia marafiki, facebooks, emails, simu, JF, na vijiwe vya kijinsia ambavyo ni nadra kupeana ushauri wa kustahimili. Na hapo kwenye Financial stress na Pressure ni papana sana. Ila kila mwanaume mwenye mke na watoto anapajua. Tena kama kachukua hii mikopo (ya kuendeleza kina mama!!!!) halafu imefika siku ya marejesho na hana kitu, hiyo dhahama kwa wewe mume utajuta!!!! Wanachosema hapa ni kuwa pato la familia kuyumba na ushawishi toka nje ndivyo vyanzo vikuu vya matatizo.
Baada ya kuyaona hayo, sasa tuna focus tatizo lako.
- Hapa Tanzania ndoa nyingi zinavunjika mikoa ya pwani ambako watu wake wala siyo VIONGOZI WA KU-CHEAT WALA KUPIGA. Kwa maana hiyo ushauri wa hapa juu kuwa ukipigwa tuu au mume akiiba mdada mwingine wewe unasepa hauelezi ukweli wa matukio yalivyo nchi hii. Potelea mbali, kama wewe ni mwepesi wa kutelekeza ndoa yako sababu umepigwa basi ondoka bila kumwona wala kumuita yule anayeamua kuwa na subira kuwa ni MJINGA. Wewe sepa na WEREVU wako.
- Tutumie mifano hai, Mikoa yenye kuripotiwa vipigo vingi kwa wanandoa imeshamiri kanda ya Kati, kaskazini na Ziwa. Yaani Dodoma, Singida, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, na mikoa ya Ziwa haswa Mara. Lakini jee, utasema ni mikoa hii hii ndiyo yenye ndoa zinazovunjika kwa wingi Tanzania? Mbona ni kama kinyume? Na hapa ndipo utaona UKWELI WA HUU UTAFITI WA SOUTH AFRICA kwamba FINANCIAL STABility ndio inachangia SANA NDOA kuyumba. Huko Ulaya ndoa zinakufa sababu ya Social media kushabikia mno mambo ambayo yanahatarisha maisha ya wanandoa kama ushoga, usagaji na pornography bila kuweka vipindi sawia ili watu waenzi maisha ya kifamilia.
- Ndugu yangu lazima uwe Jasiri KUU-FACE UKWELI; Wanaume kuzaa nje ya ndoa zao hakutaisha na leo na wala hawataacha kwa vile wanasemwa hapa JF. Wakwako sio wa mwisho. Na wala hakuanzisha balaa hili. Rais mmoja wa Ufaransa (yeye alikuwa na watoto wawili kabisa). Orodha wa wazito tena wenye watoto ni ndefu mno. Hujaingia orodha ya watumishi wa Bwana wenye watoto na wake za watu. Tosheka kuwa sio wewe peke yako alikuwa majeruhi wa tatizo hili. Sidhani kusepa ni BIMA AU CHANJO ya tatizo lako. Dawa ni meza ya Mazungumzo na MUMEO. Chumbani.
- Ukweli mwingine unaokufuata ni kuwa WATOTO WAKO wa Kuzaa hawatahuzunika kama wewe. Jiandae, siku moja lazima utawasikia wanacheka wakisema wamempata DOGO. Kama Unaye haswa binti jiandae na kauli kuwa "yule dogo ni baba mtupu" Hii kauli utaambiwa tu na mwanamke mwenzio (binti yako)hata kama utaolewa baada ya kusepa.
MAWAZO YANGU
1. Huna haja ya kusepa. Linda ndoa yako. Kwani umefukuzwa? Upo uwezekano chanzo kilichompelekea huu mwanya labda umechangia. HUWEZI JUA. Wewe tafakuri, fungua mawasiliano na mwenzio, kisha taratiiiiiibu rekebisha BOMA lako.
2. Zidisha mawasiliano rafiki kati yako na mumeo juu ya mtoto huyu hii itasaidia kumwondolea uwezekana wa kulirudia hili pengine.
3. Usifuate KILA ushauri wa SOCIAL networks na media. Pia Huna haja ya kuapa kulipiza kisasi kwa mama mtu. Hakuna haja na wala haina tija.
4. Kila nyumba ina matatizo yake. Haya ya kwako ni matatizo. lakini nakushauri sana tunza ndoa yako. Ilimradi hujamdhulumu huyu bwana kama mkewe kwa hakika lazima Mwenyezi Mungu atakufanyia wepesi. Usikimbie nyumba yako, wanao,na kiapo chako, wende kuwa mdada huna mwenyewe kila mtu anajipanga kukuwahi mwisho na wewe kama mumeo uishie kuzaa watoto wa mababa wengine.
Wengine wataboresha mapungufu yangu