1. Kutembea nje ya ndoa au niseme usaliti, uwe wa kihisia au kimwili. Hili kwangu halina mjadala kabisa. If I find out you're two-timing on me, we are through. I call it one strike and you're out policy.
2. Physical violence. Ukinitwanga na frying pan kichwani au ukinitandika chupa ya Balimi usoni, kutakuwa hakuna tena ndoa hapo. Kwa sababu nita-swing for the fences, and if I connect, lights out. Lose-lose situation there.
3. Vices nyingine kama ulevi usio wa kupindukia, uvutaji sigara, matumizi mabaya ya pesa, uvivu wa kufanya kazi, kuvaa nguo kama hoochie mama, kutumia lugha chafu chafu, uchafu wa mwili na mazingira, ili mradi tu hazijavuka mipaka na kuwa kero ambazo siwezi kuzivumilia, nadhani ni vitu ambayo mimi na yeye tunaweza kukaa chini, tukavijadili, na kukubaliana namna ya kuvikabili na kuvirekebisha.
Lakini watu tumetofautiana. Wapo ambao hata wachitiwe namna gani bado watang'ang'ana kupigania ndoa zao. Wengine hata wawe wananyanyaswa kiasi gani, iwe kihisia au kwa kupigwa bado tu watang'ang'ana.
Well, siwezi kuwakosoa sana maana huo ni uamuzi wao. Lakini huwa siamini katika upuuzi wa kudhani kuwa kwa vile tu mtu uko kwenye ndoa na kwa vile labda mna watoto basi ndo uendelee kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga.
Kufanya hivyo (kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga) ni kuwa mpuuzi na mjinga. Hata kama kuna watoto, hiyo haina maana ndo ushikwe mateka katika ndoa yenye kila aina ya manyanyaso.
Inafika wakati mtu unaweka mguu wako chini, unachora mstari na kusema 'sasa basi, imetosha'. Unasepa unaenda kuendelea na maisha yako.