Hivi ni kwanini unakubali kuvunja ndoa yako?

Makonyeza

Member
Feb 2, 2020
69
252
Cha mno ni nini hasa?

Nini matarajio yako nje ya ndoa yako uliyonayo sasa?

Ninini?, kwamba uliamini kwamba mwenzi wako ni malaika? Au unaamini kwamba ukimwacha huyo then utampata mtakatifu asiyekukosea, asiye saliti wala kukuudhi au uliaminishwa kwamba anayekuoa au umuoae atakuridhisha kwa kila sekta? Bahati mbaya mtu wa aina hiyo bado hajazaliwa na hatozaliwa!

Huyo uliyenaye pamoja na kasoro zake zote ndiye uloandikiwa, jukumu lako ili kutimiza Neno hilo ni kumvumilia tu ili kujisitiri wewe na mwenzio na familia yako kwa ujumla. Kama itathibitika ulikosea kuoa au kuolewa ndugu yangu hiyo ni kashfa, jitahidi kuificha kashfa hiyo. Kuna wanaoamini kwamba ukikutana na aliyeacha au kuachika basi mwangalie kwa macho matatu kwa sababu ni dariri kwamba ni dhaifu wa mahusiano, havumiliki au hajui kuvumilia na kuzikabili changamoto za mahusiano, Kwanini uruhusu jamii ikuangalie hivyo?

Nikikumbushe kidogo, ndoa huwa tamu saaana katika hatua tatu tu, moja ni kabla ya ndoa yenyewe, mwenzio utamuona ni katika watu bora duniani, pili ni wakati wa ndoa yako, ona watu wanavyoacha yao kuhangaika na wewe huku wakijinyima kukuchangieni, unajiona kama malkia au mfalme pale kila aliyekuja kwenye harusi yako anapopambana japo apate picha ya kumbukumbu nawewe.
Na ya tatu huwa ni fungate kama umebahatika kwenda, walioenda fungate wanaelewa ninachosema.

Zaidi ya hapo ladha tamu ya ndoa huanza kupoa taratiiibu, sasa hapa ndipo inapohitajika mwanaume kuonesha uanaume wako katika ndoa.

Ipo hivi, majukumu yako mwanaume katika ndoa ni ya asili na hayatokoma mpaka unafunga kauli. Hapa nazungumzia majukumu ya kutunza familia yako kwa kadri ya uwezo wako bila kuhoji au kutegemea mchango wa mwanamke kwako, mwanamke yeye kwa nafasi yake tu ameshahukumiwa kwa kuwajibika kwako lakini wewe mume ni sharti uoneshe kwa vitendo ili kujenga na kuboresha upendo hata kwa watoto ambao kiasili humwamini mama kwa sababu ndiye wanakuwa naye muda mrefu zaidi yako.

Ni wajibu wako kumuhudumia mkeo na kumpa pesa ambazo pia usijaribu kuhoji anavyozitumia, hata kama na yeye anakipato binafsi, bado nguo zake na viatu vyake ni jukumu lako.

Majukumu ndio kipimo cha uanamume wako nyumbani na watoto watakutambua na kukuheshimu kama ni mwajibikaji wakiuona mkono wako katika makuzi yao, vinginevyo utamlaumu mke kwamba anawaharibu na kuwafundisha vibaya watoto.

Hakuna ndoa isiyo na misukosuko wala usijidanganye kwa kujifananisha na fulani anavyoishi na mwenzie, yao ya ndani huyajui!!
Muhimu na wewe ficha ya kwako ili nao wawaone mfano kwao!

Kuna siku wazee wetu wakikumbuka misukosuko na mitihani waliyoipitia ndo utaona anawaalika ndugu, jamaa na marafiki kusherehekea Jubilee ya miaka kadhaa ya ndoa yao, yaani wanashangaa kuona wamemudu kufika uzeeni licha ya changamoto walizopitia ambazo yamkini ni hizihizi ambazo Leo wewe unaona zinakushinda katika ndoa yako, simama imara watu wajifunze kwako.

Wewe umebahatika malezi ya wazazi wote, ebu fikiria unavyowapa wakati mgumu watoto kwa malezi ya upande mmoja kwa kiburi chako tu cha eti " watoto wangu nawamudu", huwamudu watoto wako kwa sababu huwezi kuwapa malezi ya pande mbili! Jitahidi vumilia taabu kero za mwenzio kwa faida ya watoto wako, hata kwa kinafiki tu maisha yaendelee.

Ebu jaribu fikiri, ni dhambi kubwa saaaaana na ya ajabu ambayo kwako itakuwa ya kwanza kufanyiwa na unaguarantee hutofanyiwa nje ya mahusiano yako haya ya sasa, jibu ni hakuna.

VUA na achana kabisa na joho na kutaka kuhukumu kila jambo, mengine yameze kama yalivyo, mengine yapuuze kama hujaona au kusikia na kisha umlaani shetani na muombe mungu akupe uwezo wa ziada kuyashinda.

Kwenye ndoa kuna chokochoko, kuna maudhi, kuna husda, vijicho, wivu, kuna nongwa, kuna fitna, chuki, kero na yafafayo mengi tu, na bahati nzuri unao uwezo wa kuyashinda yote haya, na ukiona haya yote hayatokei kwenye ndoa yako nakuhakikishia hiyo ni NDOTO sio NDOA halisi, amka haraka usije ukakojoa kitandani mtu mzima!

Silaha zako ni tatu tu, VUMILIA, SAMEHE na SAHAU.
 
Cha mno ninini hasa??

Nini matarajio yako nje ya ndoa yako uliyonayo sasa?

Ninini?, kwamba uliamini kwamba mwenzi wako ni malaika? Au unaamini kwamba ukimwacha huyo then utampata mtakatifu asiyekukosea, asiye saliti wala kukuudhi au uliaminishwa kwamba anayekuoa au umuoae atakuridhisha kwa kila sekta?? Bahati mbaya mtu wa aina hiyo bado hajazaliwa na hatozaliwa!

Huyo uliyenaye pamoja na kasoro zake zote ndiye uloandikiwa, jukumu lako ili kutimiza Neno hilo ni kumvumilia tu ili kujisitiri wewe na mwenzio na familia yako kwa ujumla. kama itathibitika ulikosea kuoa au kuolewa ndugu yangu hiyo ni kashfa, jitahidi kuificha kashfa hiyo. Kuna wanaoamini kwamba ukikutana na aliyeacha au kuachika basi mwangalie kwa macho matatu kwa sababu ni dariri kwamba ni dhaifu wa mahusiano, havumiliki au hajui kuvumilia na kuzikabili changamoto za mahusiano, Kwanini uruhusu jamii ikuangalie hivyo?

Nikikumbushe kidogo, ndoa huwa tamu saaana katika hatua tatu tu, moja ni kabla ya ndoa yenyewe, mwenzio utamuona ni katika watu bora duniani, pili ni wakati wa ndoa yako, ona watu wanavyoacha yao kuhangaika na wewe huku wakijinyima kukuchangieni, unajiona kama malkia au mfalme pale kila aliyekuja kwenye harusi yako anapopambana japo apate picha ya kumbukumbu nawewe.
Na ya tatu huwa ni fungate kama umebahatika kwenda, walioenda fungate wanaelewa ninachosema.

Zaidi ya hapo ladha tamu ya ndoa huanza kupoa taratiiibu, sasa hapa ndipo inapohitajika mwanaume kuonesha uanaume wako katika ndoa.

Ipo hivi, majukumu yako mwanaume katika ndoa ni ya asili na hayatokoma mpaka unafunga kauli. Hapa nazungumzia majukumu ya kutunza familia yako kwa kadri ya uwezo wako bila kuhoji au kutegemea mchango wa mwanamke kwako, mwanamke yeye kwa nafasi yake tu ameshahukumiwa kwa kuwajibika kwako lakini wewe mume ni sharti uoneshe kwa vitendo ili kujenga na kuboresha upendo hata kwa watoto ambao kiasili humwamini mama kwa sababu ndiye wanakuwa naye muda mrefu zaidi yako.

Ni wajibu wako kumuhudumia mkeo na kumpa pesa ambazo pia usijaribu kuhoji anavyozitumia, hata kama na yeye anakipato binafsi, bado nguo zake na viatu vyake ni jukumu lako.

Majukumu ndio kipimo cha uanamume wako nyumbani na watoto watakutambua na kukuheshimu kama ni mwajibikaji wakiuona mkono wako katika makuzi yao, vinginevyo utamlaumu mke kwamba anawaharibu na kuwafundisha vibaya watoto.

Hakuna ndoa isiyo na misukosuko wala usijidanganye kwa kujifananisha na fulani anavyoishi na mwenzie, yao ya ndani huyajui!!
Muhimu na wewe ficha ya kwako ili nao wawaone mfano kwao!

Kuna siku wazee wetu wakikumbuka misukosuko na mitihani waliyoipitia ndo utaona anawaalika ndugu, jamaa na marafiki kusherehekea Jubilee ya miaka kadhaa ya ndoa yao, yaani wanashangaa kuona wamemudu kufika uzeeni licha ya changamoto walizopitia ambazo yamkini ni hizihizi ambazo Leo wewe unaona zinakushinda katika ndoa yako, simama imara watu wajifunze kwako.

Wewe umebahatika malezi ya wazazi wote, ebu fikiria unavyowapa wakati mgumu watoto kwa malezi ya upande mmoja kwa kiburi chako tu cha eti " watoto wangu nawamudu", huwamudu watoto wako kwa sababu huwezi kuwapa malezi ya pande mbili! Jitahidi vumilia taabu kero za mwenzio kwa faida ya watoto wako, hata kwa kinafiki tu maisha yaendelee.

Ebu jaribu fikiri, ni dhambi kubwa saaaaana na ya ajabu ambayo kwako itakuwa ya kwanza kufanyiwa na unaguarantee hutofanyiwa nje ya mahusiano yako haya ya sasa, jibu ni hakuna.

VUA na achana kabisa na joho na kutaka kuhukumu kila jambo, mengine yameze kama yalivyo, mengine yapuuze kama hujaona au kusikia na kisha umlaani shetani na muombe mungu akupe uwezo wa ziada kuyashinda.

Kwenye ndoa kuna chokochoko, kuna maudhi, kuna husda, vijicho, wivu, kuna nongwa, kuna fitna, chuki, kero na yafafayo mengi tu, na bahati nzuri unao uwezo wa kuyashinda yote haya, na ukiona haya yote hayatokei kwenye ndoa yako nakuhakikishia hiyo ni NDOTO sio NDOA halisi, amka haraka usije ukakojoa kitandani mtu mzima!

Silaha zako ni tatu tu, VUMILIA, SAMEHE na SAHAU.
 
Hii spirit ndio anayotakiwa awenayo mwanandoa ili ndoa idumu, yaani kutalakiana isiwe ni jambo la kiliendea kirahisi.

Ila tukubali tukatae, kuna hali inafika inakuwa kutengana kwa hao wanandoa ni bora zaidi kuliko kulazimisha kuendelea kuwa pamoja, vinginevyo inakuwa ni maafa.

Kwani hujawahi kusikia watu hadi wanauwana?
 
Ndoa ni tamu katika steji mbili tu!

Hela ikiwepo ya kutosha kukabili majukumu ya familia ipasavyo pamoja na nguvu za kiume za kumchakata mkeo. Hayo mawili yakiwepo ndoa lazma iwe tamu provided mke ulimchagua mwenyewe kwa utashi wako na ukabahatika kumpata mwanamke muelewa na asiye mbinafsi.

Kimoja wapo kikikosekana tu ndoa lazima iwe chungu na kuachana ni swala la muda tu kama time bomb.
 
Cha mno ninini hasa??

Nini matarajio yako nje ya ndoa yako uliyonayo sasa?

Ninini?, kwamba uliamini kwamba mwenzi wako ni malaika? Au unaamini kwamba ukimwacha huyo then utampata mtakatifu asiyekukosea, asiye saliti wala kukuudhi au uliaminishwa kwamba anayekuoa au umuoae atakuridhisha kwa kila sekta?? Bahati mbaya mtu wa aina hiyo bado hajazaliwa na
Ndoa huwa haivunjwi bali inajivunja yenyewe.
 
SI KWELI....
Ndoa ni tamu katika steji mbili tu!

Hela ikiwepo ya kutosha kukabili majukumu ya familia ipasavyo pamoja na nguvu za kiume za kumchakata mkeo. Hayo mawili yakiwepo ndoa lazma iwe tamu provided mke ulimchagua mwenyewe kwa utashi wako na ukabahatika kumpata mwanamke muelewa na asiye mbinafsi.

Kimoja wapo kikikosekana tu ndoa lazima iwe chungu na kuachana ni swala la muda tu kama time bomb.
 
WEWEEEEEEEEE🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄

KATIKA NDOA NA MAHISIANO KUNA WAPENZI AU MWANANDOA AMBAYE ANA TABIA ZISIZOVUMILIKA, TENA ZA KUJIRUDIA,KWENDA ZAKE MTU KAMA HUYO AKAFIE PENGINE.
 
Hakika mm nimependa kipengele cha uvumilivu japo wa kinafiki ili kulinda makuzi na malezi ya watoto wetu,nami nayaishi mpaka sasa ili watoto wapate sitahiki zao.
 
Kumvulia mtu anayefanya makosa ya makusudi ya mara kwa mara hata baada ya kumuonya mara nyingi haikubaliki!

Imagine wengine unakuta mke amejituliza anaimbishwa na wanaume wa nje lakini anawakataa kwa kuona kuwa yeye ni mke wa mtu na inampasa kulinda heshima ya mume wake!

Fikiria mara mke anakuja kujua mume wake amekuwa aki-cheat kwa muda mrefu kiasi cha kuzaa na nje ya ndoa , imagine!


Mke akiamua kumuacha mume wa hivyo itakuwa ni Sawa tu.

Maana akijilazimisha kubaki ataishi kwa sononi na huzuni moyoni !

Ni bora kwenda kuitafuta furaha yake kwingine.
 
Talaka ni nzuri na inaepusha madhara mengi sana pale inapobidi.

Ikibidi ivunjike tu haina haja ya ku-pretend machoni pa watu ili hali moyoni hakuna penzi miongoni mwa wanandoa.
 
Mpaka ndoa inavunjika huwa kunakuwa na facts fulani.

Huwezi kuwa na jibu la aina moja la kuvumilia mtu mwenye kujirudia kufanya makosa ya makusudi.
 
Back
Top Bottom