Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Status
Not open for further replies.
unakumbuka yale maisha ......kule ilikuwa full mkimbizano.hakuna kuremba wala nini..mi nilisomaga na wadada

fulani wakawa wanajifanya High class mashauzi mengi baada ya muda mbona waliisoma namba..

na wakawa wachapakazi kuliko hata sie wengine

hizo boarding ni za siku hizi bana,,sie wa enzi zile tunaelewa

Ahahah!hata mimi kuna ambao walileta mashauzi masista waliwanyoosha within a year.
Nakumbuka siku ambazo mkitoka na zile fuso inakua more of an outing,aki i miss those days.
 
kama hajui kupika na kazi nyingine
unamfundisha kwani kuna ubaya jamani?
unaweza ukasoma day na bado usijue kufanya chochote
ni kujituma kwa mtu maana hata hao wa boarding hua wanaenda likizo!!
so kama mwanamke anapenda kujua kazi za nyumbani atajua tu!!
 
Sasa my dear ndio maana nikasema hii research haieleweki kabisaaa..mi pia nimegraduate post 2005
alitakiwa basi afanye hata sampling(time,aina ya shule,etc) maana ipo too general.
na pia waseme kuwa hao watoto huwa hawarudi kwao likizo
 
Huyo wako bro uliingia chaka! mbona hao ndio wana full maujanja? mtoto anajua kubembeleza, kila kitu kwake ni kisafi sasa huyo wako vipi tena? au anaumwa? ehm mpeleke hospital hayuko sawa bro!
 
na pia waseme kuwa hao watoto huwa hawarudi kwao likizo

ni wazazi wachache sana ambao watoto wakirudi likizo huwa na muda wa kuwafunza house works. wengi wa wazazi hasa wa kileo huwa bize na kazi na hivi ukizingatia maisha yako kimjini zaidi, kwasababu mtu hata bustani huna, uwanja wa kufagia hakuna, nyumba ya kudeki ndo hvy kuna house girl wewe unategema huyu mtoto kazi atajifunzia wapi??

kama umeweza of which najua uliweza ni kwasababu ulidevote sana na hukuona uvivu kwenye kumfunza kazi.
 
hujakosea mkuu mimi wangu nahisi nitamtoa depo la JKT
 
binti yangu kasoma boarding kuanzia darasa la 5 mpaka sasa yupo form 2.
anaporudi home likizo, ndo anatupangia tule nini likizo yoote..... yeye ndo anajua lunch tutakula hiki na dinner tutakula hiki. siyo kupanga tu, na kupika pia. anapika siyo mchezo. Hii inatokana na mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana kuwa naye jikoni na kumfundisha kupika.
Usafi room kwake anafanya mwenyewe, hayo ya 6x6 siwezi kumsemea, lol!
sasa hizo shule za boarding ambazo wanasoma hao ambao yeye kamuoa sijui ni za wapi?
labda asingizie wazazi wa huyo binti aliyemuoa, siyo boarding school


na malezi pia yanachangia.......we si unaona binti ako alivyo active lakin kama
angekuwa anarudi home na wewe u care less about her ukiwa na housegel ye
ndo afanye kila kitu matokeo yake ni nini.....

My dada kumbe you have a big girl..Congrats,,Ur such a SUPER WOMAN
 
Jamani hii aibu nyingine wazazi tunajitakia. Mimi wakati nalelewa tulianza kufundishwa shughuliza zote za nyumbani tukiwa wadogo sana tena hatukubaguliwa kwamba hawa ni watoto wa kiume au wakike.
 
pia maisha ya kazi mtu hujifunza toka kwao hata kama anasoma boarding akirudi likizo full kazi sasa kama mtu hajazoea kufanya hawezi kujifunza kwa bf au mume na kparty ya siku moja haimbadili kitu
 
Ahahah!hata mimi kuna ambao walileta mashauzi masista waliwanyoosha within a year.
Nakumbuka siku ambazo mkitoka na zile fuso inakua more of an outing,aki i miss those days.

hahaaa na wewe unakumbuka.....mie mwenyewe I miss those days for sure.....
 
binti yangu kasoma boarding kuanzia darasa la 5 mpaka sasa yupo form 2.
anaporudi home likizo, ndo anatupangia tule nini likizo yoote..... yeye ndo anajua lunch tutakula hiki na dinner tutakula hiki. siyo kupanga tu, na kupika pia. anapika siyo mchezo. Hii inatokana na mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana kuwa naye jikoni na kumfundisha kupika.
Usafi room kwake anafanya mwenyewe, hayo ya 6x6 siwezi kumsemea, lol!
sasa hizo shule za boarding ambazo wanasoma hao ambao yeye kamuoa sijui ni za wapi?
labda asingizie wazazi wa huyo binti aliyemuoa, siyo boarding school

Yani ndio maana nasema i miss those days..
i miss being the one choosing menu iwe vipi lol
And fixed point,honestly hayo ya 6* 6 sio shule imefanya ni mtu binafsi.
And by the way,mi nlianza std 2 only 7years tena mbali kabisa
i love your spirit
 
binti yangu kasoma boarding kuanzia darasa la 5 mpaka sasa yupo form 2.
anaporudi home likizo, ndo anatupangia tule nini likizo yoote..... yeye ndo anajua lunch tutakula hiki na dinner tutakula hiki. siyo kupanga tu, na kupika pia. anapika siyo mchezo. Hii inatokana na mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana kuwa naye jikoni na kumfundisha kupika.
Usafi room kwake anafanya mwenyewe, hayo ya 6x6 siwezi kumsemea, lol!
sasa hizo shule za boarding ambazo wanasoma hao ambao yeye kamuoa sijui ni za wapi?
labda asingizie wazazi wa huyo binti aliyemuoa, siyo boarding school

Mkwe imekuwaje mwanangu akaanza boarding school akiwa la tano. Ulimchoka kivyo?

Naongeza mahari walah
 
Hiv boarding schools siku hizi zinatoa na vyeti vya 6kwa 6?
 
#Majanga


Ukitaka kuona ndoa ya blue haya sasa uoe mwanamke ambaye maisha yake
yote yalikuwa ni kwenye shule za boarding, chekechea boarding, primary
boarding, secondary boarding, a level boarding, chuo kikuu boarding.

Yaani ndani hawajui lolote, wachafu wa mazingira ya ndani, hawajui
kupika vyakula vyote na vya kwenye 6X6 kiujumla hawafai. yaani anaweza
akaacha vyombo vichafu mlangoni mpaka jioni viko palepale tu halafu
wavivu muda mwingi ni kusinzia tu.

hebu na wengine toeni egisipiriensi yenu.

mmh..mi nakataa kabisa hoja yako..inategemea shule gani ya boarding amesoma,au hujui kuna kayumba na international boarding school..mi nimesoma boarding toka darasa la 4 hadi sasa,but i dare say naweza vitu vingi kuliko ata ao day scholars..huwezi kufananisha mtoto alietoka weruweru girls na wa feza girls two different people
 
Hao unaokutana nao ni vimeo wenzio. Huko shule za boarding kuna somo la cookery and home economics, needle work inaanzia primary. Hakuna kisingizio, watu wanaamua kuwa walivyo. Hata kama hukufundwa kwenu ama shule, mbona tunajifunza lace wig kwa kina wema sepetu? Ukitaka kujifunza usafi unakuwa msafi, ukitaka kujifunza kuwa mume, baba, kaka, mama, ama sada bora hakuna kizuizi. You are what you think, and even the sky aint the limit no more.
 
NAFIKIRI ANAONGELEA HIZI BOARDING ZA FEZA etc ambazo shuleni hata kudeki room wanadekiwa na wakirudi nyumbani wazazi wanawapa madriver full time, wao ni beach, kushinda kwenye chatrooms na kushionda mlimani city, wazazi wakidhani ndo kutunza watoto vizuri..lakini boarding zile tuzosoma sie enzi za mwalimu hadi somo la mapishi, kushona, yapo. kufanya usafi nje na ndani ya dom ni kawaida hadi jiko la shule so angalieni type za wanawake mnaooa sio kulalama tu.
 
halafu on the other side..there is more to life than just to know how to cook n wash n take care of you men...yopu never know what passion a person have
 
lakini ni ukweli kwamba waliosoma boarding schools toka wako wwadogo primary school huwa hawajui house works kabisa. mambo ya kufagia sijui kuosha vyomb sijui kufua kwao yamewapitia kushoto na si wa kike tu hata wa kiume.

sasa atauaje ilihali shulen wanafuliwa kwa mashine, msosi wanapikiwa usafi wanafanyiwa, akifunga shule akija hme kuna madada 3 wa kazi, yy kazi yake ni kuangaia muvi, kuskiliza mziki, kuchat kwenye sosho media na kulala unategemea nini??

Mwalimu kama unaongelea boarding hizi za fees za milioni kadhaa sawa.

Lakini boarding kawaida ni kinyume chake...

Pia wazazi wanachangia sana sana kufanya watoto wasiweze kujua kazi za nyumbani na mambo mengine yawapasayo kufanya.

Experience ya kweli: Nilichukua watoto wa 2 wa ndugu zangu tofauti wakiume na wakike kukaa nao kwa muda. Yule wa kiume alisoma shule za kawaida na wazazi wake walikuwa strictly, yule a kike ndo walee.

Yule wa kiume alikuwa anaamka ahusbuh na mimi nikishika kazi hii yeye kashika hii, yaani hadi kusonga ugali na kupika mboga alikuwa expert. Yule wa kike saa 2 ndo anaamka....niliamua kumfanyia kazi ya ziada hadi anarudi kwao alikuwa anajua kila kitu ambacho msichana anapaswa kufanya.

Niliongea na mama yake na alikiri kuwa hakuwa na malezi mazuri kwa mwanae, nikamwambia nimemshape so, usijemharibu tena.

Kwa sasa youko boarding na kila likizo nauliza progress zake,she is doing great kwenye home chaos

Wazazi wa kike tuna jukumu kubwa kuhakikisha watoto wetu wanafahamu kazi za ndani km kufua, kuosha vyombo, kupika na kadhalika.
 
ww unaongelea boarding ambazo ulisoma miaka ya <2005 sasa boarding hizi za >2005 ni majanga matupu. na hata wale watt waliosoma primary boarding miaka hiyo nao pia wali lack skills hasa za house works. mie nilisoma boarding toka form 1-6 lkn enzi zile weruweru ilikuwa weruweru kweli manake tulikuwa tunaosha hadi migongo ya ng'ombe. chezeya kilimo wewe...................

Umenikumbusha mbaali, siye tulikuwa wazee wa milimani Lyamungo yaani tukimaliza shamba tunaenda pale Mashine tools au kwenye kile kijisoko uchwara kusafisha macho na vijisamaki na ndizi rost....Don't remembering me ma st...Nakumbuka kulinda usiku na kulima bustani yaani nilishika jembe hadi leo nipo town lakini jembe ninalo...Watoto wetu wa St. Kumezeshwa sijui wataridhi nini.
 
hahahaha, umenichekesha sana sana...............nimemkumbuka baba ghafla.
watoto wa siku hizi sisi wazazi ndio tumeaharibu kwa kujidai tunawapa raha ya maisha kumbe hovyo kabisa.

Jana kuna kijana mmoja alinipigia simu akanishtakia jambo nilicheka sana moyoni mwangu, ni kijana wa 27 na ana gf ambaye anataka kumchumbia sasa kwa muda wote aliokaa na huyo gf wa miezi 6 kila akienda kumtembelea gf wanakula hotelini home hakupikwi, lkn kila mdada anapokuja kumtembelea kidume anakuta kidume kapika msosi fresh na binti anakula na kufurahia menu tamu. sasa mie nikamuuliza kwann binti hapiki?? akadai binti anasema hapendi kupika nikamuulza wewe uliamuaje?? akasema alimlazimisha siku moja ampikie ugali basi binti alichofanya alienda kununua ugalai wa mama ntilie akautia kwenye poti kisha akanunua na mboga. kijana alipofika akatengewa vizuri kwenye sahan sasa akashangaa mbona msosi wenyewe kama vile ugali mbichi manake sasa umejaa maji akamwambia binti huu ugali ni mbichi ngoja tuupike tena uive vzr binti alianza kujiuma uma kumbe hata kusonga ugali hajui................. mkaka wa watu ikabidi aairishe kula akaondoka kwa hasira.
Dah hivyo jamaa alijitahidi kuvumilia kwenda kula hoterini,halafu ukimuona binti anvyong'aa barabarani utamani uende naye,unajua dada yangu wanawake na saiz wanafikiri kuwa na jins ya kike pekee umemaliza sasa kwenye kulea mtoto itakuwaje mtoto ataanza bording school kuanzi baby class mpaka chuo kikuu!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom