Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Status
Not open for further replies.
hahahaha, umenichekesha sana sana...............nimemkumbuka baba ghafla.
watoto wa siku hizi sisi wazazi ndio tumeaharibu kwa kujidai tunawapa raha ya maisha kumbe hovyo kabisa.

Jana kuna kijana mmoja alinipigia simu akanishtakia jambo nilicheka sana moyoni mwangu, ni kijana wa 27 na ana gf ambaye anataka kumchumbia sasa kwa muda wote aliokaa na huyo gf wa miezi 6 kila akienda kumtembelea gf wanakula hotelini home hakupikwi, lkn kila mdada anapokuja kumtembelea kidume anakuta kidume kapika msosi fresh na binti anakula na kufurahia menu tamu. sasa mie nikamuuliza kwann binti hapiki?? akadai binti anasema hapendi kupika nikamuulza wewe uliamuaje?? akasema alimlazimisha siku moja ampikie ugali basi binti alichofanya alienda kununua ugalai wa mama ntilie akautia kwenye poti kisha akanunua na mboga. kijana alipofika akatengewa vizuri kwenye sahan sasa akashangaa mbona msosi wenyewe kama vile ugali mbichi manake sasa umejaa maji akamwambia binti huu ugali ni mbichi ngoja tuupike tena uive vzr binti alianza kujiuma uma kumbe hata kusonga ugali hajui................. mkaka wa watu ikabidi aairishe kula akaondoka kwa hasira.

Mama nanihii wa magorofani Shekilango,ambaye binti zake mmoja yuko UD mwaka wa kwanza na mwingine anaua four mwaka huu still wanafuliwa vyupi na dada wa kazi...eti kisa anawapenda! Huwa nawaangaliaaaa hadi natema mate chini...kimbembe ni siku dada aliposafiri kwenda kwao kusalimu,huyu wa UD si ilibidi apike ugali wa mbwa? Unaambiwa asubuhi tumekuta mbwa wamenunaaaa...hawakugusa chakula cha bi dada...kilikuwa kibichi!
 
wa feza anakuaje na wa weruweru anakuaje,explain yourself.

mmmh weruweru utaisoma kama lele mama apo ndo mahali pake kulima,ufugaji mambo kibao lakin watoto wa feza akuna ayo mambo,.......wana weru nisaidien kueleza maana mi sio mzuri wa kujieleza
 
Me naamini tabia na mienendo ya mtu huanzia nyumbani.Nyumbani ndiko mtu ana tengenezwa na kurekebishwa.

Hata kama binti shuleni hajishughulishi lakini kama nyumbani anapewa kazi na kuimizwa usafi lazima abadilike.

Lakini ukweli ni kwamba uvivu wa watu au ugoigoi unachangiwa na malezi.

Mvivu shule hata nyumbani mvivu
Mchafu shuleni hata nyumbani mchafu.

Tabia nyingi za watoto zina mchango mkubwa wa wazazi.
Kuna watoto hawalijui jiko maana kuna mfanya kazi.
Kuna mabinti na watoto wako form 2,lakini bado wana fuliwa nguo alaf mtu ana walahumu wakiwa wachafu au wasipo jua kupika.

Wazazi wengi wanalea watoto kama mayai kabisa na wanaona sawa.

Kwakweli mimi huwa nikisikia fulan ajui kupika au ni mchafu naanza kuwalahumu wazazi maana najua wazazi pekee ndio wana mchango mkubwa kuwa shape watoto wao.

Kwenye hayo ni kuwalahumu wazazi.
 
Hahahab umenikumbusha jamaangu alioa mke. Hakuamin kilichotokea siku yake yakwaza tangu watoke honeymoon. Mke hajui hata kupika chai.. Jaman wenzenu kabla hatujaoa tulikua tunawatorosha wachumba zetu tunakaanao ghoto angalau week ama mwez ndio tunajifunza anakuaje akiwa ndan kama mke. Tatizo lenu leo hii mnamkurupua dada wawatu toka kwa wazazi wake na kufunganae ndoa masikin hujawahi hata siku moja ukashinda nae ama hata kulala nae usiku kucha. Kwa kisingizio et kwao get kali. Polen
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom