Ndoa inaelekea kunishinda

Ndoa inaelekea kunishinda

Wanawake hapo ndo mnapofeli, et unataman umshirikshe mchungaji wenu??? Huna wazaz, ndugu na jamaa?? Kuwa makin na hao wachungaj watakuomba buree!! Nao binadamu
Weee unawajua ndugu wewe si bora hata mchungaji, kuna ndugu niwanaa hajipata kutokea mie mwenyewe siwezi mshirikisha ndugu mambo mengine bora nife nayo
 
Na Mimi nawaza kitu Kama hicho niwe tu bize na maisha yangu na mwanangu aliye tumboni nafikiria kwanzia Leo nisishike simu yake Wala nisimfatilie akiamua kuchepuka achepuke maana nshaona nikijua naumia alafu ameshanikatisha tamaa coz ndokwanza tuna miezi 6 kwenye ndoa alafu namfuma na wanawake 3 Bora hata angekuwa mmoja ningesema labda kwakuwa na mimba ameona anitafutie msaidizi nafikiria hata siku akitaka nishiriki nae niwe tu Mimi natumia nae condom maisha yote kujiepusha na maradhi maana nimewasiliana na wadada wawili kati ya hao wanasema walikuwa hawatumii condom mmoja ndoanasubiri kazi ya upolisi hivyo alimforce wakapime ukimwi kuhofia asijepata maambukizi akakosa kazi, yani hata hajali afya yangu na mtoto wake mpaka Kuna wakati inanijia roho ya kishetani nawaza sijui nimchomee hata ndani jamani naumia Basi tu mpaka naona tena Kama huu ujauzito nlobeba ni mzigo kwangu maana mimba tu nayo inanitesa naumwa badala ya yeye kuwa faraja kwangu ndokawa Moto ananichoma
acha kufikiria mambo ya kumchomoa mtoto, hilo neno lifute haraka maana shetani naye yuko kazini,,kwani mtoto ana shida gani jaman

omba sana usiwaze mawazo negative juu ya kiumbe asie na hatia

Mungu akushindie
 
Usikate tamaa,vumilia tu,Usiondoke pambana na ndoa yako,hao michepuko wanapita tu

Hiyo ndiyo hulka ya mumeo kwahiyo ipotezee usimfuatilie ukimfuatilia utazidi kuumia kila kukicha,kikubwa asikuletee malazi tu.

Hakuna haja ya kushtaki kwa mchungaji

Wanasema ndoa kuvumilia,kwahiyo vumilia.


Wanaume na michepuko kama chura na maji.
Wanaume wote Baba yao mmoja
 
Simu Mimi ndonilimlazimisha ache nilimwambia kwakuwa ushamwambia una mke na umeomba msamaha tuanze upya simu niachie hakuna tena kumiliki simu ya Siri na nilifanya makusudi ili nijue Kama Kuna wengine Ila sahivi najutia nlichofanya coz naumia hata nikisema nishirikishe wazazi na wachungaji napata wakati mgumu maana najua ni watu wa dini hawatokubali tuachane watafanya juu chini aombe msamaha yaishe mwisho wa siku nitakuwa tu nimejitia aibu kwa kuwaelezea upumbavu wa mme wangu
Halafu yeye akisikia kuna mtu kajisevia huko anavyokuja kama mbogo, ndiyo maana wanakufa mapema kwa stess
 
Kama ni movie ndio kwanza ipo kwenye ....
”Starring”....“Executive Producers”...”Title”... usijaribu kuvunja ambacho mungu amekiunganisha mkuu!

Nachokiona wewe umeolewa ila ni mgeni kwenye michezo ya mapenzi. Nikutoe hofu tu kuwa wanaume 80% huwa wana cheat ila kwa adabu sana! 20% ndio ambao hawana adabu kwenye cheating wao hawana aibu kuonesha kuwa wana cheat na hawa ndio wabaya sana.

Ukivunja ndoa sababu mume ameku cheat jua uendako pia utachitiwa tu na utakuwa dissapoonted mara mbili! Jifunze kuishi na hio hali kuwa mumeo sio muaminifu na maumivu yakizidi na wewe tafta mtu akugongege kwa siri ili akufariji. Hio ndio namna ya kupunguza machungu ila usiache kumuheshimu mumeo hata ukishaanza kuliwa maana ukiteleza hapo tu utapewa talaka kwa aibu na fedhea. Liwa nje ila usianze dharau na kejeli utakamatwa.
Unaona mwenzio mke kajua michepuko 3 ndoa haina hata mwaka , nayeye akipata kamchepuko kamoja atamlilia nani huyo baradhuri!
 
Ndomana sijashirikisha mtu yeyote mpaka sahivi nimekuja kuomba ushauri kwenu hata wazazi wenyewe na ndugu napata wakati mgumu kuwambia maana ni aibu jamani miezi 6 ya ndoa michepuko 3 na bado usikute wapo pia nisiowafahamu unajua inakatisha tamaa naona tu Kama nitawaumiza wazazi wangu kwanza baba alivyo mkali na hii mimba najua tu hatokubali nirudi nyumbani na hii mimba, jamani ndoa ni ngumu Mungu wangu
Pole sana, vumilia ujifungue kwanza ukipona ndiyo utajua mbivu na mbichi, inamaana hapo mkiwa uchumba alikuwa anakuzunhusha tu kwenye magori ili usijue chochote, subili ujifungue kama si tabia yake labda atabadilika lakini kama ndiyo zake mmm hapo kisu utakuwa nacho mkononi
 
Bado una hasira za kitoto Sana, mi siwezi kumpigia mchepuko wa mume nikigundua kuna uchepukaji we komaa na mwanaume

Kwa jinsi maisha yalivyo achepuke kwa kunipumbaza nisijue nikihitaji mkuno naupata fresh arrrghhh jinsi uwanja wa mapenzi ulivyo chafuka huko kitaa dah naweza kumfuma na nikamsamehe vizuri tu, Kwanza naona km mumeo anakupenda au nae Bado ana akili za kitoto kukubali kupigia simu mchepuko na kuweka loudspeaker,
 
Simu Mimi ndonilimlazimisha ache nilimwambia kwakuwa ushamwambia una mke na umeomba msamaha tuanze upya simu niachie hakuna tena kumiliki simu ya Siri na nilifanya makusudi ili nijue Kama Kuna wengine Ila sahivi najutia nlichofanya coz naumia hata nikisema nishirikishe wazazi na wachungaji napata wakati mgumu maana najua ni watu wa dini hawatokubali tuachane watafanya juu chini aombe msamaha yaishe mwisho wa siku nitakuwa tu nimejitia aibu kwa kuwaelezea upumbavu wa mme wangu
Kwanza Pole hayo ni mapito katika ndoa yako pia binafsi nisingependa mambo ya ndoa kuyqweka public maqna huwa sioni faida yake direct lqbda ushauri wangu ...umesema ni mume wako hope unajua mapungufu yake sikushauri sana uchunguze simu zake lakini pia jaribu kumfanyia jambo ambalo analipenda sana then mfanyie mara kwa mara lengo ni kumteka kihisia then baada ya mda labda miezi miwili


Naamini hapo atonal umuhimu wako then unanza kumweleza nijinsi gani hupendezwi na tabia yake
Na using penda kuona hiyo tabia inajirudia tena na kama ndo tqbia yake mwambie abadilike jaribu kumweleza athari zake ..... pia mkumbushe hali ya ujauzito uliyo nao ...... kiubinadam lazma atajirudi Pole sana
 
Na Mimi nawaza kitu Kama hicho niwe tu bize na maisha yangu na mwanangu aliye tumboni nafikiria kwanzia Leo nisishike simu yake Wala nisimfatilie akiamua kuchepuka achepuke maana nshaona nikijua naumia alafu ameshanikatisha tamaa coz ndokwanza tuna miezi 6 kwenye ndoa alafu namfuma na wanawake 3 Bora hata angekuwa mmoja ningesema labda kwakuwa na mimba ameona anitafutie msaidizi nafikiria hata siku akitaka nishiriki nae niwe tu Mimi natumia nae condom maisha yote kujiepusha na maradhi maana nimewasiliana na wadada wawili kati ya hao wanasema walikuwa hawatumii condom mmoja ndoanasubiri kazi ya upolisi hivyo alimforce wakapime ukimwi kuhofia asijepata maambukizi akakosa kazi, yani hata hajali afya yangu na mtoto wake mpaka Kuna wakati inanijia roho ya kishetani nawaza sijui nimchomee hata ndani jamani naumia Basi tu mpaka naona tena Kama huu ujauzito nlobeba ni mzigo kwangu maana mimba tu nayo inanitesa naumwa badala ya yeye kuwa faraja kwangu ndokawa Moto ananichoma
Huyo shetani mshinde kabisa, maana shetani mwingine unaye ndani, hana tu akili na inawezekana hakupata malezi mazuri kwa wazazi wake, halafu ndugu wa Mme sio wakuwambia hizo habari wengi wao hawanaga maana kabisa, pambana na mwenyewe ukimtanguliza Mungu basi.
 
Ushauri wenu jamani mimi nimeolewa nipo kwenye ndoa hatujamaliza hata mwaka Ila kinachoniumiza mme Wangu ananisaliti, nimemkuta anamiliki simu ya Siri pamoja na line alikuwa kaficha kabatini baada ya kugombana naye akakubali kuwa ana mchepuko akampigia akaweka loud nikawa nawasikia akamuomba samahani kwa kumchezea akamwambia Mimi nimeoa, nina mke nmeona siyo vizuri kumsaliti mke wangu dada akalalamika we badae akakubali kumblock kidogo nikapata amani.

Baada ya hapo hiyo simu ya Siri akaweka mezani akatoka zake Ila kilichoniumiza zaidi baada ya lisaa zilikuwa zinaingia text kutoka no. tofauti tofauti 2 baada ya kuchart nao kumbe nao ni michepuko yake tena jumla nimemfuma na wanawake 3 kwa wakati mmoja.

Msamaha kaniomba Ila nashindwa kumsamehe, naumia sana Bora ningemkamata hata na mmoja nisingeumia sana Ila wa 3 ukitegemea ndoa haina hata mwaka nawaza sijui kalogwa, natamani nimshirikishe hata mchungaji wetu Ila napata wakati mgumu naona ni vitu vya aibu hata kushirikisha watu wetu wa karibu. Natamani niondoke Ila kinachonipa wakati mgumu tayari Mimi ni mjamzito yaani nawaza ingekuwa siyo hii mimba ningeachana nae ananifanya Hadi nakata tamaa na mimba niliyonayo kitu ambacho ni dhambi, Naombeni mnishauri nifanyaje nahisi kuchanganyikiwa nakosa maamuzi presha imeshuka naona Kama dunia imeniangukia kweli ndoa ni ngumu sana duh! Mungu anitie tu nguvu.
Eeeh usimfatilie unataka kufa uache watoto wako ety .......akimwaga mboga we mwaga ugali...kama uwezi kumwaga ugali jipe likizo hata ya week 2 ukirudi nyumbani maisha yanaendelea

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Jana nimemsema nimemwambia navumilia tu sababu ya hii mimba Ila sitokufatilia maisha yote tutatumia condom na hapa nawaza kujiepusha na maradhi Bora Mimi nitumie nae condom Kama yeye nje anashindwa kutumia tumlee mtoto maisha yaende siku ziende tujifie yeye akipata ukimwi uko au hata akizaa uko nje atajua na maisha yake vinachosha jamani kupigizana kelele na mtu mzima kila siku
Vumilia usikate tamaa hivyo jamani! Mungu akusaidie kulishinda hilo, labda bado mdogo sana yaani upo kwenye uchumba ndoa miezi 6 michepuko 3? Hakuwa siriasi na ndoa huyo, kwanza michakato ya ndoa ikianza michepuko huwa inatoswa ila huyo alikuwa nao , mpe nafasi tena huyo ng'ombe labda atajirudi, kama ni kwa mchungaji angalia maana wote wanaume ujue huwa wanasaidiana hao uchungaji wanaweka kando
 
Ndomana sijashirikisha mtu yeyote mpaka sahivi nimekuja kuomba ushauri kwenu hata wazazi wenyewe na ndugu napata wakati mgumu kuwambia maana ni aibu jamani miezi 6 ya ndoa michepuko 3 na bado usikute wapo pia nisiowafahamu unajua inakatisha tamaa naona tu Kama nitawaumiza wazazi wangu kwanza baba alivyo mkali na hii mimba najua tu hatokubali nirudi nyumbani na hii mimba, jamani ndoa ni ngumu Mungu wangu
ndoa sio ngumu best, unavyoichukulia ndo utapata shida

ndoa ni nzr sana maana mko wawili mnashirikishana maisha na kusaidiana

omba na zungumza na mwenzako mambo yatakaa sawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom