Ndege yatolewa majini Bukoba

Nimesikiliza yule mmama wa CNN alikua anasema hizo ndege marekani zilishazuiwa kutumika as zilianguka zinaanguka sana especially kwenye kutua kama sehemu ina ice au hali ya baridi zaidi
Sasa nimejiuliza mabeberu wao wamezizuia kwao iweje sie ndo tuzitumie?
Hii Afrika Mungu atutetee tu!
Bora tubakie kwenye road trip kwa staili hii,
 
Kumbe impact ilikuwa kubwa ndio maana marubani walifariki.

Hio impact lazima uzimie kwa muda kiasi unakufa maji.
Rubani mzoefu na shupavu anaweza fanya gliding kilomita chache kutegemea na umbali walipo angani. Kama ndege imetokea upande wa Kyaka badala ya Musira kuna shida, ila ingekuwa injini zimefeli zote wakikaribia kutua bado rubani angeweza tembea kidogo na akatua kwenye maji bila impact mbaya hivi. Inategemea na uwezo wa rubani
 
Mi Bado najiuliza,Hawa kenge wenye Kombat walikuwa wapi jana?hapa kwenye msiba kubeba majeneza wamefata posho tu
 

Attachments

  • 20221108_143709.jpg
    106 KB · Views: 9
Bado usafiri wa ndege utabaki kua salama zaidi ukilinganisha na zingine tu mkuu, ajali haiepukiki.... Road trips kwa siku zinachinja wangapi TZ na hata duniani kote? TZ hii ni ajali ya ngapi ya ndege kutokea ndani ya miaka 10 tu na ukilinganisha na za barabarani?
 
Sidhani kama ilikuwa free fall. Rubani angeishusha kama vile anatua uwanjani, alipatia almost 80% ndio maana vifo vilikuwa vichache. Free fall au nose down asingechomoka mtu japo ni majini.
Nose down mbaya kweli asingepona mtu ingesaga watu wote hapo wangekuta ndege yote imesambaa vipande probably hata ingelipuka kabisa..
 
Sasa kama wanaleta ndege ambazo huko nje zimeonekana hazifai hapo kuna usalama kweli?
Sijakataa usafiri wa ndege ni safe ila imagine hiyo ndege ingecrush kwenye runway ikalipuka impact ni kubwa zaidi
 
Economy class kumbe nzuri. Business Class wote wameondoka Kwa muonekno huo.

Wapumzike Kwa Amani.
 
Ndio maana nikawa nashindwa kupata majibu!

Inakuwaje rubani aombe msaada wa kuvunjiwa vioo kanakwamba yeye akikuwa hajiwezi kabisa?

Kumbe alikuwa ameshaumia sababu ya huo mvunjiko wa ndege
 
Nina rafiki yangu Mkenya na nina pilot mkongwe alileta same story siku ya event naweza kukupa ushuhuda?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…