Ndege ya Urusi imepotea kwenye rada

nadhani upo ndotoni wewe CIA ndo wazee wa fitina za A plus sasa kama unafikiri russia anaweza hii vita subiri uone kila siku ndgu yako anapoteza watu muhimu
 

Well said, na ndege za TU-154 zilikuwa na safety record nzuri ingawa zilihundwa zamani sana.

Nilipo sikia Warusi zaidi ya sabini wamefariki kwa kunywa pombe haramu iliyokuwa unauzwa kwenye supermarket ndio nikashituka na kufikiri isije ikiwa marubani nao walinunua viroba vya a bootleged pombe iliyo changanywa na methanol wakajikuta wanakuwa vipofu ghafla wakati wamefikia phase ya kupaa!!! - Utani.

Ukweli ajali hiyo inasikitisha sana sana.
 
Nakubaliana na wewe.

Walidukua uchaguzi, na kule allepo wakajifanya eti wameshinda. Sasa wazee wa fitina za viwango "A" wameingia mzigoni
Hii vita nilijua tu mrusi anacheza ngoma asiyojua ni ya kabila gani.matokeo yake anacheza vizuri ila hafuati mdundo.

Sijui kama atatumbuiza muda mrefu.
 
Bado inabidi tusubiri habari za kiuchunguzi zaidi.
Maana japo wanasema wameanza kuona mabaki lkn Hali ya hewa ya eneo hilo haisupport ndege kuanguka na ndio maana safari za ndege nyingine hazijazuiwa.

Hii inakuja siku kadhaa baada ya allepo kuangukia mikononi mwa assad. Kama kutakuwa na hujuma basi lengo ni kurefusha vita vya Syria au kuwakatisha tamaa warusi ktk jitahida za Amani Syria.
Ngoja tusubiri maana siku hizi duniani mambo yako kiujanjaujanja sana. What you hear and see is not always the real truth.
 
Aisee naikubali US ila kwa hili kuua watu wasio na hatia inauma sana.
 
Nadhani unajilisha upepo ktk aya ya mwisho ya post yako..
 
Most probable.
 
Ndiyo. Kwa mimi naichukulia kama ajali nyingine, ingawa more than 50% ya ajali zote za ndege duniani zimegunduliwa kuwa ni makosa ya kibinaadamu Zaidi ya kiufundi. Na kwa mujibu wa habari za kuaminika, si mara ya kwanza kwa ndege hizo za kijeshi kufanya safari hizo za Syria kwa kuwa wana kituo chao cha kijeshi na mara zote huwa inasindikizwa na ndege mbili za kivita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…