Ndege Njiwa amejenga pembeni ya nyumba yangu!

Ndege Njiwa amejenga pembeni ya nyumba yangu!

Naombeni kujua hii ina maana au inaashiria nini.

Ni kwamba wakati najenga kibanda changu nilipomaliza kupaua siku kadhaa baadae nilikuja gundua kuna njiwa wa porini wamejenga kiota ktk mbao za paa kwa ndani.

Baada ya kuziba kwa kuzunguka nje na baadae kuhamia wale njiwa waliondoka, ila nimegundua kuna ndege wengine wamenjenga pembeni ya nyumba, na baadae km miezi mitano mbele wale njiwa wamerud na wamejenga kiota chao pembeni kwa nje karibu na kenopi.

Sijapata tatizo lolote wala usumbufu wowote kwani pia napenda hawa viumbe.

Ninachotaka kujua kama kuna mahusian yoyote na mambo ya kiroho.


Hao njiwa huwa hawatengenezi viota katika nyumba ambazo hazivutii (masikini),
Hicho ni kiashiria kuwa upo vizuri kiuchumi na una nyumba nzuri.
 
Una Bahati sana kuwa na njiwa nyumbani ambaye hukumfuga. Pamoja na kwamba njiwa wanatumika kichawi lakini wa kichawi ni tofauti kabisa. Njiwa kwa asili huwa anaashiria upendo hivyo Mara nyingi anatua Nyumba zenye upendo na Baraka. Kama wewe kwako kumejaa ugomvi njiwa hawezi kutua kula chakula au kuweka kiota. Likewise kwa paka wale ambao siyo wa kichawi akija kwako na Watoto au akizalia jua ameona Amani na upendo Kutoka kwa familia hiyo. Sasa jichunguze hali ya hapo nyumbani ulinganishe na maneno Yangu hapa. Karibu
 
Una Bahati sana kuwa na njiwa nyumbani ambaye hukumfuga. Pamoja na kwamba njiwa wanatumika kichawi lakini wa kichawi ni tofauti kabisa. Njiwa kwa asili huwa anaashiria upendo hivyo Mara nyingi anatua Nyumba zenye upendo na Baraka. Kama wewe kwako kumejaa ugomvi njiwa hawezi kutua kula chakula au kuweka kiota. Likewise kwa paka wale ambao siyo wa kichawi akija kwako na Watoto au akizalia jua ameona Amani na upendo Kutoka kwa familia hiyo. Sasa jichunguze hali ya hapo nyumbani ulinganishe na maneno Yangu hapa. Karibu
Amen, kuna kila sababu ya kuzidisha amani na upendo!
 
Wanyama wanaakili, hao wanajua alipo binadamu kuna lishe ya urahisi
 
Wanaume wa Dar bwana,unauliza ukifanyie nini kitoweo???
 
Ni ishara ya ngekewa hiyo.Utateuliwa kushika wazifa wa juu.
 
Back
Top Bottom