Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Kwanza tujiulize, mawaziri wa wizara zisizo za muungano huwa wanawakilisha
serikali ya nchi gani?

Katiba ya Tanganyika iliyounda muungano imeendelea kulindwa na Serikali yake bado ipo,
pamoja na viongozi wake kuwepo na kusimamia mambo yasiyo ya Muungano.
Katiba na sheria za Tanganyika ndizo zinazotumika katika eneo la Tanganyika kwa yale mambo
yasiyo ya Muungano kama ambavyo Katiba na sheria za Zanzibar zinavyotumika katika eneo
la Zanzibar kwa yale mambo ambayo si ya Muungano.


Kimtazamo, malalamiko ya wanancchi kudai uwepo wa serikali ya Tanganyika yana mantiki
kwa kuwa pamoja na hatua ya kuifuta Katiba ya Tanganyika, lakini kule kuendelea kutambua
kuwepo kwa sheria zisizo za muungano ni kutambua kuwepo kwa mamlaka ya Tanganyika
ambako sheria hizo kwa mambo yote yasiyo ya Muungano zinaendelea kutumika hadi leo.

Kwa maana hiyo sioni sababu ya watawala wa nchi hii kukataa serikali tatu...
 
Huyo Sitta ni mnafiki hakuna deni munalo tudai,zanzbar hatuna viwanda lakini deni munaloleta sio la uhakika hilo deni mulotoa tunaweza kulipia mikoa miine ya tanganyika umeme bure,lzanzbar tuna population 1.2 milion umeme wa kiasi gani tunao tumia ?

Hilo deni ni nothing tu kwetu kwa sababu kuna fedha nyinga ambzo tunazikosa sisi wazanzbari kwa kupitia bank kuu ya tanzania,wakati zanzbari imetoa zaidi ya asilimia 10 katika kujenga bank hio,kuna fedha za mikopo,fedha kutoka UN kusaidia nchi masikini zinapokewa kwa jina la tanzania lakini matumizi hufanyika tanganyia na sisi kuangukia patupu.

Ukiona mtumzima analia ujue kuna jambo,na ndio maana wazanzibari wamechoshwa na muungano mkubwa kumla mdogo,na haiwezi kani.

Kama ndoa imekushinda chukua talaka yako uende. Ya nini kulialia huku ukijiegemeza kwa bwana. Wazanzibari mnaiweza sana sitaki-nataka!
 
Na sisi tunaitaka Tanganyika yetu ili isimamie mambo ambayo si ya muungano ili yale ya muungano yashughulikiwe na serikali ya muungano.
Kaka dai kwa kutumia activities,kuna majukwa sasa hivi kama bunge,na makongamano ya katiba,sasa huo ni wakati wako kuingia katika hilo,na hamasisha wenzio katika kudai hilo na unajua faida ya kuwa na taifa lako,kwaa maana hiyo waelimishe wenzio.

Ikiwezekana mfuate hata mbunge wako mueleze afikishe ujumbe bungeni,kama sisi wanzanzibari tunavyodai nchi yetu soveregn state of zanzibar.
 
kwa upande wangu mi naona ilibidi iitwe Tanzibar, hv ilikuaje mpaka ikatokea tanzania? Maana kule mwishoni hupati ule muunganiko wa haya maneno mawili.
 
Nampongeza miss judi. Mchango wake umeenda shule. Lakini pia kuna umuhimu wa tanganyika kuwa na chombo kinachosimamia masuala ya tanganyika kama ilivyo kwa zanzibar. Na pia tanganyika isipoteze utaifa wake, japo ni ndani ya nchi moja
 
Ukweli ni kwamba; Rais wa Tanganyika/Tanzania Mwl. J.K.N na Marais wa Tanzania pekee naongelea hao jamaa watatu ni sawa na maji na mafuta. Hii inanituma niseme kuwa miaka 50 ya UHURU imegawanyika hivi: -
  1. Miaka 21 ya UHURU (wakati wa Nyerere)
  2. Miaka 13 ya IBA LAKINI USISHIKWE (wakati wa mzee wa Ruksa)
  3. Miaka 10 ya UBINAFSI (wakati wa mzee wa Ubinafsishaji)
  4. Miaka 6 ya UFISADI (wakati wa Baba Riz a.k.a HB bingwa wa wake za watu)
Yakumbukwe maneno ya Baba wa Wataifa Mheshimiwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere a.k.a Mzee wa Kuota

Ni hayo tu!!!!!!!!!!!!!
 
Ukweli ni kwamba; Rais wa Tanganyika/Tanzania Mwl. J.K.N na Marais wa Tanzania pekee naongelea hao jamaa watatu ni sawa na maji na mafuta. Hii inanituma niseme kuwa miaka 50 ya UHURU imegawanyika hivi: -
  1. Miaka 21 ya UHURU (wakati wa Nyerere)
  2. Miaka 13 ya IBA LAKINI USISHIKWE (wakati wa mzee wa Ruksa)
  3. Miaka 10 ya UBINAFSI (wakati wa mzee wa Ubinafsishaji)
  4. Miaka 6 ya UFISADI (wakati wa Baba Riz a.k.a HB bingwa wa wake za watu)
Yakumbukwe maneno ya Baba wa Wataifa Mheshimiwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere a.k.a Mzee wa Kuota

Ni hayo tu!!!!!!!!!!!!!
then inafwata kizazi ya watoto wa watawala kutawala
 
Ukweli ni kwamba; Rais wa Tanganyika/Tanzania Mwl. J.K.N na Marais wa Tanzania pekee naongelea hao jamaa watatu ni sawa na maji na mafuta. Hii inanituma niseme kuwa miaka 50 ya UHURU imegawanyika hivi: -
  1. Miaka 21 ya UHURU (wakati wa Nyerere)
  2. Miaka 13 ya IBA LAKINI USISHIKWE (wakati wa mzee wa Ruksa)
  3. Miaka 10 ya UBINAFSI (wakati wa mzee wa Ubinafsishaji)
  4. Miaka 6 ya UFISADI (wakati wa Baba Riz a.k.a HB bingwa wa wake za watu)
Yakumbukwe maneno ya Baba wa Wataifa Mheshimiwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere a.k.a Mzee wa Kuota

Ni hayo tu!!!!!!!!!!!!!

Pamoja na sifa nyingi anazostahili huyu Hayati J.K.N. anawajibika kwa kiasi kikubwa na haya matatizo tunayoyakabili sasa kwani huu mfumo tulionao ni yeye aliyeutengeneza. Kiongozi mzuri ni yule anayeandaa mifumo na taasisi imara za utendaji na viongoziwarithi thabiti wenye upeo na uwezo mkubwa wa kiuongozi watakaoendeleza mazuri aliyoyaanzisha na kuyaacha yale mabaya (i.e. succession plan). Kwa bahati mbaya huyu mzee alihakikisha kuwa amezungukwa na viongozi dhaifu waliokuwa wanajua kazi moja tu - kumsifu na kumtukuza yeye. Hii ilisababisha awe ni yeye peke yake ndiye anayeng'ara siku zote. Kwa bahati nzuri kwake alifanikiwa ila kwa bahati mbaya kwa taifa tunalipa gharama za sifa za J.K.N.
 
Duh sasa kama trend hii itaendelea (ya kutawaliwa na ccm) basi tunakoenda ndiyo kubaya zaidi maana graph inazidi kushuka
 
kuelekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara /Tanganyika..
najua kwa uhakika kwamba Muungano ulioleta Tanzania ulikuwa kati ya Tanganyika na Zanzibar...baada ya Muungano Zanzibar ilendelea kujulikana kama Zanzibar huku upande mwingine Tanganyika ikipotea!!swali langu ni lini Tanganyika ilianza kuitwa Tanzania Bara badala ya Tanganyika.?na kwa nini Zanzibar iendelee kuwa Zanzibar huku Tanganyika ikiwa Tanzania Bara..?
 
Huo ni utashi tu lakini Tanzania ni nchi mpaya iliyozaliwa baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Mara nyingine upande wa bara huitwa Tanzania bara kama ambavyo watu wengine wanavyoiita Zanzibar Tanzania visiwani.
 
naamini hii ni zaidi ya utashi,..!kuna any official documentation inayoitambulisha Tanzania bara kwa jina la Tanganyika kama ilivyo kwa Zanzibar, km hakuna je wewe huoni km suala hili ni zaidi ya utashi.?
 
Very interesting! By the way, is the name "Tanzania Bara (Tanzania Mainland)" referring to/replacing Tanganyika in the Constitution? If yes, it is OK; otherwise, full "magumashi".
 
lini jina Tanzania bara liliingizwa kwenye Katiba kuri place Tanganyika?
 
kwenye katiba hakuna Tanganyika kuna Tanzania Bara toka katiba ilipoundwa 1977.
 
kuna Tanzania Bara na Tanzania visiwani au Tanzania Bara na Zanzibar?
 
kwenye katiba hakuna Tanganyika kuna Tanzania Bara toka katiba ilipoundwa 1977.
basi kama ni hivyo hata zanzibar isiwepo iwepo tanzania visiwani!
NAITAKA TANGANYIKA YANGU NIJIVUNIE KAMA WAZANZIBARI!
 
nataka Tanganyika na Zanzibar....au Tanzania Bara na Tanzania Visiwani...
 
Tanganyika, Tanzania Bara, Zanzibar, Tanzania Visiwani, Unguja na Pemba, Tanzania, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania n.k ...n.k hayo yote ni majina tu hata kama tutaiita nchi Tangawizi, tuimarishe maendeleo ya kiuchumi na kijamii na tuachane na utegemezi wa nchi nyingine. Ninakerwa na tabia ya kuomba omba.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom