Nchi yetu inaitwa Tanganyika

mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui?

Jamani hebu nisaidieni hapa.....ni mkoloni gani alieipa mipaka yetu jina la Tanganyika?

Na pia najua kabla hawajaja wakoloni mababu wa mababu zetu walikaa kwenye mipaka hii hii,,,hivi kuna mwenye Idea ilikuwa inaitwaje hapo awali? kabla ya kuitwa Tanganyika ......

Ila pamoja na kuitwa na mkoloni bado naweza jivunia nalo maana ni jina lenye maneno ya kiswahili "Tanga" na "Nyika" na lina tafsirika kwa lugha yangu.....

Mimi ni Mtanganyika na kama muanzisha Thread nachukia kuitwa M-bara......na ndugu zetu wa Zanzibar hawawezi kutuita Watanzania, huishia kutuita wabara kama tunavyowaita wazanzibar au wavisiwani.....
 
kama ni usawa kwenye revenue kwa kweli wasahau watapata kwa proportionality tu not otherwise hakuna haja ya kufavourana hapa so what? Usawa wa kisiasa huo wanao tena nadhani unaona wanvyotamba huku tanganyika

hata wamasai ,wanyamwezi, wasukuma na wengineo wanatanua tu zanzibar...usimuonee choyo mtu anadai haki yake just do the same dai haki yako ...taka kuwepo kwa katiba ya tanganyika na rais wa tanganyika na bunge la tanganyika na baadae ndio tuanze mambo ya muungano
 
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa tanganyika,
maana ya neno tanganyika, siijui,
tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui

nilizaliwa tanzania,
nilizaliwa afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu

kwa hiyo;

mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu

maana ya tanzania, najua
maana ya afrika, najua
maana ya dunia, najua
maana ya mwandamu, najua

nawauliza wazanzibari,
nini maana ya zanzibari,
nani aliipa jina zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
Kwa nini wasijivunie utanzania?

look ,miss judith...you can dye your hair and change the color ...you can bleach your skin to whiten it...you can dress up like madonna or lady gaga...but as long as you miss ugali and chips kuku then you are still a tanganyikan...the last time i checked tanzania was not a real name.
 
Kabla ya Aprili 1964 kulikuwa na nchi mbili: Tanganyika na Zanzibar.

Hata kabla ya Muungano wa hizo nchi mbili, kulikuwa na ofisi huko London ikishughulikia mambo ya Wanafunzi waliokuwa wanatoka nchi hizi mbili, na sisi tuliokuwa masomoni huko tulikuwa tunaiita "TANZANREP" tulipokuwa tunapeleka telegram huko. Kwa hiyo:
TAN = TANGANYIKA
ZAN = ZANZIBAR
Kwa hiyo zilipoungana zikajiita "TANZANIA".

Sasa kama kuna mwananchi asiyependa kujiita Mtanganyika kutokana na ukweli kuwa jina "Tanganyika" lilianza baada ya Vita Kuu ya Kwanza, 1919 wakati Waingereza walipokabidhiwa sehemu ya German East Africa, lililokuwa koloni la Wajerumani, basi labda apendekeze jina jingine. Kujiita "Tanzania Bara" au "Tanzania" tu ni kosa kwa vile Zanzibar ikiwa imejitoa, hakutakuwa na "ZAN". Hata sasa kwa kweli tunapojiita Tanzania "bara" si sahihi, kwa vile Mafia Island ni sehemu ya Tanganyika, na si bara ni kisiwa kama Pemba au Unguja.
 
Tanganyika nakupenda sana
Tanganyika naamini utarudi
Tanganyika sehemu yako tukufu ipo na utaikuta muda ukifika
Mwenzako Congo alipotea kama wewe katika mazingira tofauti na yako na pahala pake aliwekwa Zaire sasa alisharudi na anatamalaki, Tanganyika naziona dalili zako kurudi nami nafurahia ujio wako...
Mimi ni mtanganyika halisi Tanzania ni muungano wa mapanya na Mbwa watatoka tu ukifika. Njoo TANGANYIKA nijivune tena kwani mambo mapya yatatawala ndani na nchi.
 
jina ni jina tu, hata kesho likibadilika na kuwa JAMHURI YA SOKWENYIKA kwa mfano, it doesnt make any difference. mimi nilizaliwa Tanzania kwa maana ya the land of Tanzania. any time and under proper condition, the same land can be called any other name,

watu wa dunia ya leo wanatazama mbele sio nyuma.

watu wanajiuliza juu ya uraia wa nchi mbili au zaidi, sisi tunajiuliza uraia wa nusu nchi!

watu wanazungumza namna ya kuvutia uwekezaji wa kimataifa, uondoshwaji wa masharti ya visa, sisi tunazungumzia kichefuchefu cha neno "bara" kwenye utambulisho wetu, tunataka turejee kwenye nchi mbili na kurudisha masharti ya passport na visa

watu wanahangaika na mazungumzo ya ushirikiano/uundwaji wa shirikisho, soko la pamoja, ushirikiano katika masuala ya sayansi na tekinolojia, umoja wa forodha, sarafu moja nk sisi tunazungumza namna ya kuvunja muungano!.

jambo la msingi la kujiuliza ni je, tunapiga hatua kimaendeleo au tunarudi nyuma? tunakwammishwa na jina hili tanzania, au ni kitu gani kinatukwamisha tusiendelee kwa kasi tuliyotazamia? kama hatupati maendeleo tunayohitaji kwa kasi tunayotazamia, je, tatizo ni nini, ni jina la Tanzania?

tusijidanganye wapendwa. watoto na wajukuu zetu watatuthamini zaidi sisi na mchango wetu kama watakuta nyumba nzuri, barabara (na miundombinu mingine) nzuri, katiba nzuri, sheria nzuri, jamii iliyostawi vizuri, amani, maelewano mazuri ya kimataifa, maelewano mazuri ya kijamii nk hata kama tutakuwa bado tunabeba utambulisho wa "Tanzania". kinyume chake, hata tukirudia utambulisho wetu wa "Tanganyika" lakini tukakosa haya mambo niliyoyataja, watoto wetu watajuta kuzaliwa "Tanganyika".

tusipoteze dira ya maendeleo, tukageukia jina kama mwarobaini kwa kisingizio cha "jasiri haachi asili" ama uzalendo nk. tusipoangalia tutapoteza muda mwingi sana kwenye cheap politics za majina tukaacha kando masuala muhimu ya maendeleo na hakika tutachekwa na wenye akili
 
jina ni jina tu, hata kesho likibadilika na kuwa JAMHURI YA SOKWENYIKA kwa mfano, it doesnt make any difference. mimi nilizaliwa Tanzania kwa maana ya the land of Tanzania. any time and under proper condition, the same land can be called any other name,

watu wa dunia ya leo wanatazama mbele sio nyuma.

watu wanajiuliza juu ya uraia wa nchi mbili au zaidi, sisi tunajiuliza uraia wa nusu nchi!

watu wanazungumza namna ya kuvutia uwekezaji wa kimataifa, uondoshwaji wa masharti ya visa, sisi tunazungumzia kichefuchefu cha neno "bara" kwenye utambulisho wetu, tunataka turejee kwenye nchi mbili na kurudisha masharti ya passport na visa

watu wanahangaika na mazungumzo ya ushirikiano/uundwaji wa shirikisho, soko la pamoja, ushirikiano katika masuala ya sayansi na tekinolojia, umoja wa forodha, sarafu moja nk sisi tunazungumza namna ya kuvunja muungano!.

jambo la msingi la kujiuliza ni je, tunapiga hatua kimaendeleo au tunarudi nyuma? tunakwammishwa na jina hili tanzania, au ni kitu gani kinatukwamisha tusiendelee kwa kasi tuliyotazamia? kama hatupati maendeleo tunayohitaji kwa kasi tunayotazamia, je, tatizo ni nini, ni jina la Tanzania?

tusijidanganye wapendwa. watoto na wajukuu zetu watatuthamini zaidi sisi na mchango wetu kama watakuta nyumba nzuri, barabara (na miundombinu mingine) nzuri, katiba nzuri, sheria nzuri, jamii iliyostawi vizuri, amani, maelewano mazuri ya kimataifa, maelewano mazuri ya kijamii nk hata kama tutakuwa bado tunabeba utambulisho wa "Tanzania". kinyume chake, hata tukirudia utambulisho wetu wa "Tanganyika" lakini tukakosa haya mambo niliyoyataja, watoto wetu watajuta kuzaliwa "Tanganyika".

tusipoteze dira ya maendeleo, tukageukia jina kama mwarobaini kwa kisingizio cha "jasiri haachi asili" ama uzalendo nk. tusipoangalia tutapoteza muda mwingi sana kwenye cheap politics za majina tukaacha kando masuala muhimu ya maendeleo na hakika tutachekwa na wenye akili

Hii post yako inaleta maswali mengi na kuhoji uelewa wako juu ya muungano na maendeleo. Kama wewe ni pro-union naomba unijibu swali hili. "Kwa nini nchi mbili ziliungana na kuunda nchi moja yenye serikali mbili?
 
Nasikia mara ohhhh, wabara wanatuonea, wabara wanatudharau. Sisi si wabara, ni watanganyika bana!

Muungwana haachi asili. Nia yangu si kuanzisha thread ya kupinga muungano, bali sipendi kuitwa mbara na ndio maana ninasema sisi sio wabara, ni watanganyika. Ukisema Tanganyika ni jina la kikoloni, basi kataa pia majina ya Tabora, Mwanza, Dar es salaam, Tanga na mengine mengi yanayopatikana katika ramani iliyochorwa na mkoloni.

Hii thread yako inaleta maswali mengi na kuhoji uelewa wako juu ya muungano na maendeleo. Kama wewe sio anti-union naomba unijibu swali hili. "Kwa nini unapinga nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja yenye serikali mbili?
 
Yupo mchangiaji mmoja mara nyingi zikiingia hoja za Kizanzibari hukimbilia kusema ukivunjika muungano wazanzibari watabaguana Wapemba na Waunguja,hii ni kwa sababu wapemba walitishia kujitenga.

Napenda kuwafahamisha kua Tatizo hilo lilikuja baada ya Watu wa Unguja kujikabidhi madaraka yote ya serekali,lakini kwa mara ya kwanza tokea mapinduzi 1964 uchaguzi wa 2010 wazanzibari wamekubaliana kuwa wamoja na kushirikiswa kikamilifu pande zote katika serekali chini ya serikali ya umoja wa kitaifa.hapa Wapemba walikubali kufuta madai yao ya kujitenga.

Tatizo hilo hilo ndio lililopo sasa katika serekali ya Tanzania ndio maana wazanzibari watalalamika hadi wapate haki zao kama nchi iliokubali kuungana au kujitoa katika muungano au kukubaliana upya aina ya muungano.

Nakubali kua Tanganyika itadhulumiwa wakigawana sawa na znz lakini na zanzibar itazulumika zaidi muungano huu ukiendelea.

Sasa wazanzibari na watanganyika tukaeni chini kufikiria n njia nzuri ya muungano itakayo zingatia mazingira ya kigiografia tulionayo.
 
nyeyerere alitabiri hivyo tu ? hata bara alitabiri itakuwa wanyamwezi na wamakua na wachanga na wamasai
Alisema kama wao "Wanzanzibari watawakataa Watanganyika na kujitenga, hawatabaki salama wataendelea kujibagua kiasi cha kuwa na wapemba na wa unguja. Na ikitokea hivyo basi Tanganyika itabaki salama." Ila na sisi Watanganyika tukiwakataa wale na kujitenga pia hatutabaki salama, ndiyo itatokea sasa wao wasukuma na sisi ni wanyamwezi. Na na dalili za awali zimeoneshwa na uvccm,baada ya kumtenga Masauni sasa wanasema Rais si lazima atoke Kaskazini, hii ndiyo dhambi ya kubaguana, Muundo wa muungano ndio unaotubagua mpaka tunapata Mzanzibari na M bara, na mswada hautaki tujadili muungano na unatutisha kuwa tutatupwa jela 2yrs, na sisi wengine tunataka kuwepo Jamhuri ya Tanzania itakayokuwa na serikali moja tu, na tukikubaliana hivyo kelele zote zitakwisha.
 
@miss Judith
NInawasiwasi historia ulioisoma kuhusu Muungano ni hile iliopotolewa kua Tanzania ni chi moja.Haina tofauti na ya wale Wakenya walio someshwa mashuleni kwao kua mlima Kilimanjaro na serengeti ni mbuga zao.

Juzi tu nilikutana na mkenye mwenye umri wa miaka 26 ananiambia kua amesikia kua kilimanjaro walidanganywa mashuleni lakini hadi juzi tunakutana hajui kua serengeti ni mbuga za Tz.
 
hata wamasai ,wanyamwezi, wasukuma na wengineo wanatanua tu zanzibar...usimuonee choyo mtu anadai haki yake just do the same dai haki yako ...taka kuwepo kwa katiba ya tanganyika na rais wa tanganyika na bunge la tanganyika na baadae ndio tuanze mambo ya muungano
nendeni tu ndugu yangu na nchi yenu makijipange upya tutaungana tena mkipata maendeleo mnayo yataka sawa hapo tutaweza kuishi bila manung'uniko
 
Jamani hebu nisaidieni hapa.....ni mkoloni gani alieipa mipaka yetu jina la Tanganyika?

Na pia najua kabla hawajaja wakoloni mababu wa mababu zetu walikaa kwenye mipaka hii hii,,,hivi kuna mwenye Idea ilikuwa inaitwaje hapo awali? kabla ya kuitwa Tanganyika ......

Ila pamoja na kuitwa na mkoloni bado naweza jivunia nalo maana ni jina lenye maneno ya kiswahili "Tanga" na "Nyika" na lina tafsirika kwa lugha yangu.....

Mimi ni Mtanganyika na kama muanzisha Thread nachukia kuitwa M-bara......na ndugu zetu wa Zanzibar hawawezi kutuita Watanzania, huishia kutuita wabara kama tunavyowaita wazanzibar au wavisiwani.....

Jina Tanganyika lilibuniwa na kupewa Tanganyika kati ya mwaka 1919-1920 na mjerumani . Tanganyika lilijumlisha nchi za Rwanda na Burudi. Nafikiri kabla ya hapo kulikuwa hakuna jina maana tulikuwa na vijidola vidogovidogo ambavyo vilikuwa na mipaka yake. Kama dola ya Mirambo na wanajeshi wake walugaluga nk.
 
@ NG'OTIMBEBEDZU

Kama huo ndio muungano mbona wa east afrika hauja ziua zile nchi tano?au huu wa zanzibar na tanganyika ni special?

Nchi za Ulaya pia mbona ziko hai bado? na Muungano upo na hakuna kelele?

hii ni kwa sababu hawakuangalia kua Ujarumani ni kubwa iwe na haki zaidi kuliko Holand wamezingatia usawa kwa maslahi ya nchi zao.
 
Kwa sasa we are busy discuss kuindoa kero namba moja ccm .hili la muungano wenzangu watanganyika na ombi tungepiga kura ya maoni ya kuvunja muungano kwa muda(nashuruku kuna thread imeanzishawa ina sehemu ya kupigia kura naomba wadau tujitahidi kwa nguvu zetu tukapige kura) ili tujifikirie nini cha kufanya kama eac mbona imerudi na taratibu na inaendelea maana isije ikawa agenda wakati suala la msingi kwa sasa ni kuistep down ccm tureform nchi hili ndio kwa sasa muhimu
 
Hii thread yako inaleta maswali mengi na kuhoji uelewa wako juu ya muungano na maendeleo. Kama wewe sio anti-union naomba unijibu swali hili. "Kwa nini unapinga nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja yenye serikali mbili?

Ingawa hujajibu swali langu (post no. 47) nashiwishika kuhoji uelewa wako wa pro-union na anti-union. Nikija na sera ya kutaka nchi yetu iongozwe na serikali za majimbo utaniita anti-union? Watu wanaoshadadia muundo wa mungano wa sasa ni unionist wa aina gani pasipokuwapo na union?

Mimi sio anti-union bali ni unionist wa ukweli mwenye kutaka muungano wa nchi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar; na hata ikiwezekana kuongeza Somalia ni sawa. Kumbuka hata Marekani ni muungano wa nchi 50 ambazo zina-exist, na zina mipango thabiti ya maendeleo. Sasa unapokuwa na muungano wa nchi mbili ambapo moja hai-exist ina maana gani. Huu muungano wenu wa 'Tanzania bara na Zanzibar umetoka wapi?'. Kumbuka hii sio thread ya muungano (maana ipo nyingine). Hapa nilitaka kumkumbusha mzanzibari akitaka kuni-distinguish, asiniite mbara bali mtanganyika. Mbona unapotea kwa kuleta hotuba ndefu ya maendeleo huku ukisahau asili yako? Mimi nina asili, na asli yangu ni Tanganyika.
 
Ingawa hujajibu swali langu (post no. 47) nashiwishika kuhoji uelewa wako wa pro-union na anti-union. Nikija na sera ya kutaka nchi yetu iongozwe na serikali za majimbo utaniita anti-union? Watu wanaoshadadia muundo wa mungano wa sasa ni unionist wa aina gani pasipokuwapo na union?

Mimi sio anti-union bali ni unionist wa ukweli mwenye kutaka muungano wa nchi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar; na hata ikiwezekana kuongeza Somalia ni sawa. Kumbuka hata Marekani ni muungano wa nchi 50 ambazo zina-exist, na zina mipango thabiti ya maendeleo. Sasa unapokuwa na muungano wa nchi mbili ambapo moja hai-exist ina maana gani. Huu muungano wenu wa 'Tanzania bara na Zanzibar umetoka wapi?'. Kumbuka hii sio thread ya muungano (maana ipo nyingine). Hapa nilitaka kumkumbusha mzanzibari akitaka kuni-distinguish, asiniite mbara bali mtanganyika. Mbona unapotea kwa kuleta hotuba ndefu ya maendeleo huku ukisahau asili yako? Mimi nina asili, na asli yangu ni Tanganyika.
mkuu endelea kuwaelishima hawa watu ungwana pasipo haki hakuna .ubarikiwe sana .tuvunje muungano tukajipange upya tutarudi wote tunajua umoja ni nguvu utengano ni udhaifu
 
hapo kweli mnaleta topics ambazo 'zinahatarisha' muungano lakini inaonekana ndiyo dawa, japo ni chungu! Kama kweli Mwalimu aliashindwa kupata jina Tanganyika lilipotoka, alihita to consult others also! Kama ni makosa ya kihiostoria, ni budi kuyarekebisha kabla hayajaturekebisha.
 
Kilicho wazi ni kuwa Zanzibar (hata ikiitwa Tanzania Visiwani) imefanya mabadiliko ya Katiba yake ambayo yamezingatia mahitaji na maslahi yake ki-muungano. Isikubalike kuwa Tanganyika (hata ikiitwa Tanzania Bara) isifanye mabadiliko ya Katiba yasiyozingatia mahitaji na maslahi ya watu wake. Kuwa na uwakilishi wa 50/50 katika kila jambo ni kupuuza milioni 40 ya watu, huku umuihimu ukipewa kwa idadi ya nchi zilizoungana (nusu kwa nusu eti kwa sababu ni nchi 2 zimeungana). Kuchelewa kufanya mabadiliko ya ki-Katiba kusiwe ni udhaifu ambao Zanziba wanataka kuutumia sasa. Wa-Tanzania Bara hawakuhusishwa na mabadiliko ya Katiba Zanzibar. Lilichukuliwa kama ni swala na Ki-siasa zaidi (CCM na CUF).

Hii ndilo kosa ambalo CCM kwa kufahamu au kwa kupuuzia, haikulifanya zaidi. Na CCM isihusike sasa kufanya mabadiliko. Si swala la Rais wa kisiasa, ni swala la wananchi ktk ujumla wao, itikadi zao, imani zao, taaluma zao. It's not a political thing but rather socio-economical !!
Mushirikishwe zanzbar kwani nchi yenu ? Hapa kwani mulipiga kura kumchagua mualishi au rais ? Hii ni nchi kama mchi nyengine,ina maamuzi yake bila ya kumshirikisha mtu yoyote,kwa hiyo basi munachotakiwa nyinyi,murudishe nchi yetu itoeni ndani ya koti la muungano,tungeni katiba yenu,rais wenu,bendera yenu,bunge la sheria lenu,mufanye mutakavyo hatutowaingilia juu yahilo,

kwa hio munahaki ya kuwa na taifa lenu,hilo ni jukumu lenu wananchi sio kikwete wala pinda,ni nyie wenyewe kuleta hoja hapo kwenu,ili taifa lenu lirudi,hapa zanzbar madai yetu ni sisi wenyewe wananchi,hakuna mtu yoyote aneshindikiza masuala haya,tumechoka na muungano ya kitapeli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom