Nchi isiyojali wanaomaliza masomo kwa alama za juu

Zakaria Lang'o

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
2,593
2,767
Inasikitisha Sana kwamba vijana wetu wanajitahidi kimasomo katika mazingira magumu Sana. Wakati mwingine fedha za mikopo ya kujikimu inachelewa, na hata wengine hawapati kabisa. Licha ya magumu yote hayo, unakuta kijana amejitahidi Hadi kufikia hatua ya juu ya ufaulu.

Wengine katika madaraja yanayofikia hadi GPA 4.2 na zaidi kwenye fani mbali mbali. Cha kushangaza ni kuwa serikali ambayo ndiye mwajiri na mlezi mkuu wa watu wake, Haina utaratibu wowote wa kuhakikisha hawa WALIOFANYA VIZURI wanaendelea na MASOMO ya juu zaidi kwa kuwapatia scholarship, au kuwaingiza katika programu inyowawezesha kujiendeleza zaidi. Hapa nawazungumzia vijana wanaohitimu Stashahada na Shahada ya kwanza.

Nchi yenye uwezo wa kununua midege kwa fedha taslimu, inashindwaje kuwawekea vijana wake utaratibu wa ajira au kuwandeleza kielimu wale WALIOFANYA VIZURI kwa viwango vya juu!? Tunawatelekeza bila kujali kwamba vijana hawa walikuwa wakikesha kuhakikisha wanapata ALAMA za juu wakiamini taifa lao litaziona juhudi zao.

Nimejaribu kuwasiliana na wakufunzi wa vyuo vikuu kadhaa ambao kwa masikitiko wamelalamika kuwa siku hizi wamefungwa mikono kwa kutoruhusiwa kuwachukua baadhi ya vijana wanaofanya vizuri ili wajiendeleze vyuoni kuja kujaza nafasi za kufundisha katika vyuo hivyo. Kwamba serikali haina mpango wa kujenga think tank ya Tanzania ni jambo la kusikitisha sana.

Ni wito wangu kwa wahusika, Mhe. Rais pamoja na wizara ya elimu ya juu, wizara ya utumishi, na tamisemi kukaa chini na kuliangalia jambo hili kwa jicho la pili.

"Mcheza kwao hutuzwa" ni msemo wa kiswahili wenye maana ya kuwazawadia mema wale wanaofanya mambo kwa uzuri. Sisi Tanzania tunajenga jamii ya aina gani ambayo hata yule anayefanya jitihada na kufanikiwa anakuwa hatambuliwi!

Serikali ifikirie kujenga watu zaidi kwa kuwajali hasa wale wanaofanya vizuri kwenye MASOMO. Haiwezekani vilaza na vipanga wote wawe "maji ga nyanza" eti kwa vile serikali inajali ndege na magorofa kuliko watu.

A concerned citizen.
 
Wenzako hawajali GPA, wanajali una deliver nini. GPA ya kukariri itasaidia nini Taifa?
Watajuaje uwezo wao wa ku deliver, iwapo hawapati nafasi. Kwa wale wanaosema GPA ya juu siyo hoja, nawashangaa. Ina maana mfumo wa elimu ya vyuo vikuu umeharibika kiasi cha watu kupata GPA za juu kwa kuhonga!!? Ina maana hata serikali inatambua Hilo ndiyo maana haijihangaishi kujali wahitimu wenye ufaulu wa juu!!!?
Naamini kuna watu mahali wanavuruga mfumo wa elimu na ajira nchi hii, mengine ni vijisababu tu.
 
Watajuaje uwezo wao wa ku deliver, iwapo hawapati nafasi. Kwa wale wanaosema GPA ya juu siyo hoja, nawashangaa. Ina maana mfumo wa elimu ya vyuo vikuu umeharibika kiasi cha watu kupata GPA za juu kwa kuhonga!!? Ina maana hata serikali inatambua Hilo ndiyo maana haijihangaishi kujali wahitimu wenye ufaulu wa juu!!!?
Naamini kuna watu mahali wanavuruga mfumo wa elimu na ajira nchi hii, mengine ni vijisababu tu.
Kaka ndio maana unaenda kwenye interview...
 
Hizo GPA za 4.3,4.4,4.5 na kuendelea zimekuwa zikionekana hazileti tija yoyote katika kutatua shida za watanzania,hakuna uvumbuzi,hakuna ugunduzi,hakuna ubunifu ni sheeeda tupu.
 
Hizo GPA za 4.3,4.4,4.5 na kuendelea zimekuwa zikionekana hazileti tija yoyote katika kutatua shida za watanzania,hakuna uvumbuzi,hakuna ugunduzi,hakuna ubunifu ni sheeeda tupu.
Kwa hiyo una maana nchi ipuyange tu kwa kuwa GPA hazina maana tena!!!? Si sahihi. Ukweli ni kuwa wanafunzi wanaofanya juhudi kufanya vizuri Ni muhimu juhudi zao zitambuliwe na kupewa nafasi. Nchi zote zilizopiga hatua zilihakikisha kwamba wale wanafunzi Bora wanaendelezwa ili walete tija. Tukisema GPA za juu hazina maana basi tuna maana kuwa tunashawishi tuwe na taifa la vilaza.
 
Nchi inatakiwa kujengwa kwa mifumo inayoeleweka. Hebu fikiria juu ya kijana aliyefanya jitihada Hadi kupata GPA ya 4.3 ; 4.4 au 4.6 tena kwenye sayansi au Engineering. Unamwacha akajihangaikie ajira sawa na yule wa GPA 2.7, kweli.
We have a real problem with people in the decision making. Something is terribly wrong somewhere.
Halafu watu kama Ndugai wanaojitibu kwa mabilioni ya shilingi wanabwabwaja eti vijana wajiajiri!!!
Huyo wa GPA ya 2.7 anaweza kuwa mzuri ktk kazi kuliko huyo wa GPA ya 4.4.

Elimu ya sasa ya kukariri na kuSolve mitihani iliyopita. GPA za kuGoogle.

Bora sisi tuna GPA ya 2.2
 
Inasikitisha Sana kwamba vijana wetu wanajitahidi kimasomo katika mazingira magumu Sana. Wakati mwingine fedha za mikopo ya kujikimu inachelewa, na hata wengine hawapati kabisa. Licha ya magumu yote hayo, unakuta kijana amejitahidi Hadi kufikia hatua ya juu ya ufaulu.

Wengine katika madaraja yanayofikia hadi GPA 4.2 na zaidi kwenye fani mbali mbali. Cha kushangaza ni kuwa serikali ambayo ndiye mwajiri na mlezi mkuu wa watu wake, Haina utaratibu wowote wa kuhakikisha hawa WALIOFANYA VIZURI wanaendelea na MASOMO ya juu zaidi kwa kuwapatia scholarship, au kuwaingiza katika programu inyowawezesha kujiendeleza zaidi. Hapa nawazungumzia vijana wanaohitimu Stashahada na Shahada ya kwanza.

Nchi yenye uwezo wa kununua midege kwa fedha taslimu, inashindwaje kuwawekea vijana wake utaratibu wa ajira au kuwandeleza kielimu wale WALIOFANYA VIZURI kwa viwango vya juu!? Tunawatelekeza bila kujali kwamba vijana hawa walikuwa wakikesha kuhakikisha wanapata ALAMA za juu wakiamini taifa lao litaziona juhudi zao.

Nimejaribu kuwasiliana na wakufunzi wa vyuo vikuu kadhaa ambao kwa masikitiko wamelalamika kuwa siku hizi wamefungwa mikono kwa kutoruhusiwa kuwachukua baadhi ya vijana wanaofanya vizuri ili wajiendeleze vyuoni kuja kujaza nafasi za kufundisha katika vyuo hivyo. Kwamba serikali haina mpango wa kujenga think tank ya Tanzania ni jambo la kusikitisha sana.

Ni wito wangu kwa wahusika, Mhe. Rais pamoja na wizara ya elimu ya juu, wizara ya utumishi, na tamisemi kukaa chini na kuliangalia jambo hili kwa jicho la pili.

"Mcheza kwao hutuzwa" ni msemo wa kiswahili wenye maana ya kuwazawadia mema wale wanaofanya mambo kwa uzuri. Sisi Tanzania tunajenga jamii ya aina gani ambayo hata yule anayefanya jitihada na kufanikiwa anakuwa hatambuliwi!

Serikali ifikirie kujenga watu zaidi kwa kuwajali hasa wale wanaofanya vizuri kwenye MASOMO. Haiwezekani vilaza na vipanga wote wawe "maji ga nyanza" eti kwa vile serikali inajali ndege na magorofa kuliko watu.

A concerned citizen.

MM SIJAFIKISHA GPA YA NNE + ILA MTOA MADA UTAPINGWA KWEL KWEL WATANZANIA WENGI WANA GPA CHINI YA NNE NA HAWATAKI KUSIKIA KUHUSU FEVA YOYOTE ILE KWA MTU YOYOTE MAALUM SO WANAHITAJ KILA KITU KIMWAGWE CHINI WATU WAGOMBEE

MAONI YANGU NI KWELI WANAOPATA GPA KUBWA WANATAKIWA KUENDELEZWA HATA KAMA KUNA BAADHI WANAZIPATA KIUJANJA UJANJA(KWENYE MSAFARA WA MAMBA NA KENGE WAMO) ILA SIO SABABU YA KUWANYIMA HAKI YAO WALIOFANA VIZURI CHUONI HATA KAMA KWA KUKARIRI(SIDHAN HATA HAO MAGENIUS WAKUBWA DUNIAN WASINGEKUWA WANAKARIRI WANGEWEZA KUWA NA MUENDELEZO WA KUFANYA MAMBO MAKUBWA)

HATA KATIKA MPIRA MFUNGAJI BORA HUTUNUKIWA ZAWAD BILA KUJALI KAZUNGUKWA NA NAN AU MAGOLI KAYAFUNGAJE YAAN GOLI NI GOLI TUU
 
Hizo GPA za 4.3,4.4,4.5 na kuendelea zimekuwa zikionekana hazileti tija yoyote katika kutatua shida za watanzania,hakuna uvumbuzi,hakuna ugunduzi,hakuna ubunifu ni sheeeda tupu.
Watumie utaratibu upi sasa kama huo wa GPA za juu hauleti tija?
 
Siku moja tulikuwa Bungeni. Kamati ya Bunge ilikuwa inapokea maoni ya wadau kuhusu umri wa maprofesa, masinia-lekchara na madaktari bingwa kustaafu. Mmoja miongoni mwa wadau aliponda sana suala la GPA kwenye ajira za walimu wa chuo. Alikuwa amekuja kuwakilisha kundi la elimu ya juu. Wawakilishi wenzake wengine wakampinga vikali, wakisema suala la elimu siyo la masikhara. Huwezi kuletaleta tu watu na viGPA vyao visivyofika 3.8 kwa undergraduate, hata kama ana GPA ya 5.0 Masters chuo cha kimataifa, na PhD. Basi ulikuwa ni mtifuano wa wenyewe kwa wenyewe. Niliweza kuona kwamba Wabunge kwenye ile kamati walikuwa wakifurahia mfarakano ule wa wenyewe kwa wenyewe.

Mwenyekiti wa kikao, aliwauliza wale wa upande wa viwango vya GPA kubwa, waliojitambulisha awali kwamba wanatoka ndaki fulani ya chuo kikuu kimoja almaruuf hapa nchini. Mwaka jana, ni asilimia ngapi ya wahitimu waliopata GPA ya 3.8 au zaidi?

Jibu lilikuwa ni wanafunzi wawili-watatu.

Mwenyekiti wa kamati akawauliza, sasa kama ninyi walimu wenye maGPA ya ukweli mnashindwaje kuandaa wahitimu watakaokuwa na GPA kubwa kama yenu?

Acha tu. Hivi mada hii inazungumzia nini kuhusu GPA?
 
Wengine katika madaraja yanayofikia hadi GPA 4.2 na zaidi kwenye fani mbali mbali. Cha kushangaza ni kuwa serikali ambayo ndiye mwajiri na mlezi mkuu wa watu wake, Haina utaratibu wowote wa kuhakikisha hawa WALIOFANYA VIZURI wanaendelea na MASOMO ya juu zaidi kwa kuwapatia scholarship, au kuwaingiza katika programu inyowawezesha kujiendeleza zaidi. Hapa nawazungumzia vijana wanaohitimu Stashahada na Shahada ya kwanza.
Ukianzia degree ya kwanza unakuwa na shida ya mkopo. Nafikiri wanaopata hawazidi asilimia 60 ya waombaji. Baada ya hapo ukiingia masomo ya juu zaidi, kwa ujumla Tanzania inasomeshewa watu wake na serikali haina mchango wakuridhisha. Chunguza vyuoni utakuta wahadhiri wetu wanategemea scholarship toka nje au hela za project zenye training tena toka nje. Mchango wetu wa moja kwa moja na mdogo sana.
Ni wakati nchi inatakiwa iweke mfuko wa scholarship kwa watanzania na sio kutegemea nchi nyingine. Tungefanya hivyo basi tunge train watu tuwatakao na mahali tutakapo. Wachina walifanya hivyo kwa kiwango cha juu na jamaa waliporudi wakabadilisha nchi.
Watu tunalaumu kuwa watanzania wanamapungufu mengi lakini ni watanzania hao hao wakienda nje wanaonekana ni wachapa kazi wazuri. Tujipange tutumie wasomi wetu ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuwawezesha wasome zaidi.
 
GPA kubwa si inaonesha maarifa makubwa muliyopata huko shuleni?
Na hayo maarifa bila shaka ni kwa ajili ya kutatua changamoto za jamii, tatueni basi ili tuone kweli kua GPA zenu ni kubwa.
Kama tatizo ni hela basi hamna haja ya hayo maGPA yenu maana hata asiyesoma anaweza kua na pesa
 
Mwenyekiti wa kikao, aliwauliza wale wa upande wa viwango vya GPA kubwa, waliojitambulisha awali kwamba wanatoka ndaki fulani ya chuo kikuu kimoja almaruuf hapa nchini. Mwaka jana, ni asilimia ngapi ya wahitimu waliopata GPA ya 3.8 au zaidi?
Kuna kitu mimi nakiita "kuchoma daraja" yaani mtu yeye anavuka daraja halafu akifika upande wa pili anchoma daraja wengine wasivuke. Hali hii iko sana vyuo vikuu kwenye ajira (kupata kazi na kupandishwa cheo). GPA kwa kuwa ndiyo kipimo chetu cha "uelewa na skills" lazima itumike, lakini ni GPA kiaso gani hapo ndio utaona shida inakuja.
Niliwahi kuona tangazo la Kampuni yetu ya mafuta wanatafuta HRO (Human Resource Officer) na wakadai GPA ya 3.5 sasa jiulize hiyo GPA kubwa hivyo ya nini?. Hata vyuo bado sijaelewa GPA ya 3.8 tulipo ajiriwa sisi hayo mambo hayakuwa hivyo lakini wachoma madaraja wametufikisha hapo. Likazuka la GPA ya 4 kwa masters. Hata huko kwa wenzetu hawaendi hivyo.
 
Wewe unashangaa hilo ? Tanzania ajira ikitangazwa hakuna tofauti ya mshahara mwenye Bsc, Msc au PhD, kama ni Serikalini wote mnaanza na kipato sawa, kwa kifupi nchi yetu siyo perfomance orienting society, watu ambao ni mediorcre ndiyo wanaofika juu na ndiyo walioshikilia nafasi muhimu kama Mbunge Msukuma kutwa kucheka na kukejeli wengine, hata humu JF watu wanakejeli hard working students wanaopata alama za juu kabisa, nafikiri ni sababu ya Ujamaa, ...
 
Wewe unashangaa hilo ? Tanzania ajira ikitangazwa hakuna tofauti ya mshahara mwenye Bsc, Msc au PhD, kama ni Serikalini wote mnaanza na kipato sawa, kwa kifupi nchi yetu siyo perfomance orienting society, watu ambao ni mediorcre ndiyo wanaofika juu na ndiyo walioshikilia nafasi muhimu kama Mbunge Msukuma kutwa kucheka na kukejeli wengine, hata humu JF watu wanakejeli hard working students wanaopata alama za juu kabisa, nafikiri ni sababu ya Ujamaa, ...
Nafasi ipo. Kila anayeomba anafikiriwa. Mshahara ni Shilingi Y kwa kazi iliyotangazwa. Kwa hiyo akipata mwenye PhD, mshahara uongezeke tofauti na akipata mwenye BSc?
 
Nafasi ipo. Kila anayeomba anafikiriwa. Mshahara ni Shilingi Y kwa kazi iliyotangazwa. Kwa hiyo akipata mwenye PhD, mshahara uongezeke tofauti na akipata mwenye BSc?

Hakuna tofauti wote mkiomba Mshahara ni sawa, yaani ni Mshahara wa BSc, sasa ukiwa na Msc au Phd hiyo ni shauri yako, ndo maana mimi sipendi communism, ...
 
Back
Top Bottom