Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Ndio usome somo la siasa ya kwamba Urais unaandaliwa na hivyo vyama vyenu ni vumbi la macho tu kutekeleza agizo la nchi za magharibi lakini hakuna Upinzani pale ni ushindani kaa klabu za mpira..

Ikiwa leo wewe unashangaa KITENGO kumuondoa mtu wakati vyama vinaondoa watu na wengine kupokea watu pasipo kujali historia zao, iweje ufikirie kwamba KITENGO kinaweza kumuondoa mtu asiyekuwa sahihi? sahihi kwa nani? maana usahihi wenyewe lazima utokane na interest za nchi sio za chama.

Na inapotokea mtu kuanzisha Cartel ndani ya Chama huoni kama ndivyo mlivyowadhania kina Kitila na Zitto na mkawafukuza. Huyu kapewa heshima na kaachwa hadi dakika ya mwisho..Kwanza ilitakiwa wagombea wote wa Urais wafanyiwe screen chack na Usalama, kehso wakija kuuza nchi je!

Leo mmekuwa na Ujasiri gani kufanya yale yale mloyakataa kwa kina Zitto kwa tuhuma tu leo ukatae utafiti wa KITENGO juu ya Lowassa!.. halafu maajabu yenyewe wanaopinga ni Chadema ambao wanasema Chama kina KANUNI zake unafikiri nchi haina KANUNI zake? Hao KITENGO unadhani wamejifunza nini kama sio kulinda Katiba na Kanuni za nchi hii... hata huko Marekani CIA lazima wampitishe mgombea Urais, UK lazima M16 wampitishe mgombea Urais sio swala la chama na wananchi pekee.
 
Ndio maana mi naamini hii nchi haitapiga hatua kidemokrasia wala kiuchumi hadi nafasi za kiutendaji zitakapoachwa kuongozwa kisiasa...

Usalama wa taifa, polisi, jeshi, TAKUKURU, mahakama, watendaji wa bunge, wakuu wa mashirika na taasisi za umma nk ... wote wapo affiliated kwa chama kimoja cha siasa...

Ili hali hii iweze kuondoka ni lazima wananchi wawezeshwe kukidhoofisha chama hiki kwa kukipunguzia sauti kwenye vyombo vya maamuzi kuanzia chini kabisa kwenye ngazi za halmashauri za vijiji, za wilaya na bunge...
 
Mkuu hili lingewezekana tu kama nchi yetu ingekuwa haina uadui wa vyama vya siasa. Vyama vingeundwa kuleta denmokrasia nchini wakati Usalama wa taifa wapo kulinda NCHI na katiba iwe msingi na mwongozo wa kiutawala lakini kwa hali iliyopo vyama vya Upinzani havikubaliani na NCHI hii na wamezua uadui usokuwa na maana kabisa.

Hapa inabidi nguvu za ziada zitumike na ndio maana nikasema Katiba inayotakiwa ni ile inayo tuunganisha na sio kututenganisha. Mkumbiuke vyombo hivi vyiote vilinandwa ili kuilinda nchi, sasa ikiwa uadui unaanza katika vyama lazima nguvu ya ziada itumike..

Wewe nambie kwa nini Chadema walifikia mkusema Muunganio wetu ni FEKLI halafu utegemee Usalama wa Taifa utakuwa nanyi? That alone Politivally was wrong! iunaweza mkudai serikali tatu laizni sio kusema Muungano wetu ni Fake hata hadi za Muungano zilikuwa forged.. Ni hatari kabisa..
 

Lengo la KITENGO ni kuweka mgombea dhaifu kutoka CCM na kusababisha mtafaruku ili kusafisha barabara kwa UKAWA kuchukua nchi kiulaini.
 
Uchaguzi ni ule wa Dodoma tu
mengine yoote ni maigizo matupu

Mkuu The Boss historia inatufundisha tofauti. Huwezi kutumia mbinu chafu kushika madaraka wakati wote. Mwisho wa hizo mbinu ni pale umma unapojitambua na kusimamia maslahi yake; na hizo zama zimeshatimia kwa Watanzania. Tanzanians can no longer be carried like a basket of tomatoes to any marketplace.
 

Mkuu kuna maswali mengi sana yanajitokeza ambayo tunatakiwa kujuliza, na kimsingi yanaharatisha usalama wa nchi. Kwanza inaonekana kuwa "KITENGO" kiko juu ya CCM, maana hata uchaguzi kimeingilia na kimevuruga kanuni za chama ni wanachama wachahce tu wanalalamikia hicho.

Lakini vile vile kuna maajabu kuhusu JP Magufuli kupewa ulinzi, hatujui ni kwa minajiri gani amepewa ulinzi na idara za serikali, sijui kama tuna sheria yoyote inayohalalisha hilo na kama kuna fedha zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo (japo hawasemi lakini ni usalama wa taifa wanaotoa ulinzi). Inabidi tujue kama vyama vingine vikichagua wagombea watapewa ulinzi kama JP.

Heavy presence ya usalama wa taifa, polisi na jeshi kwenye mkutano wa CCM ni doa kubwa sana kwenye demokrasia. Inaoanesha by default ni vyombo vya CCM, i wonder kama hayo tutayaona kwenye mikutano ya vyama vya upinzani.
 
Halafu hujiulizi kura za Asha Rose na Amina zilipungua?
kuingia tano bora Asha kura 280 halafu eti baadae akapata kura 50?
huoni hii results ya kutengenezwa ili Magufuli aonekane ana support?
Pengine walijua kura za Magufuli zisingetosha kutokana na hasira za waliokuwa wana muunga mkono Lowasa,na hii ingesababisha kupatikana mgombea dhaifu zaidi miongoni mwa wale kina Mama, huu ni mtazamo wangu kwamba kura zilipigwa na matokeo kutoka kwa staili ile kwa kusudi maalum,
 

Uko sahihi kabisa. Watz tusikubali upuuzi huu. Eti Kitengo!!? Hili ni genge la kimafia lenye lengo la kuendelea kupora rasilimali za hii nchi kwa kushirikiana mabwana zao wa nje ambalo kwa sasa ndilo linalothibiti CCM.
 
Uwezekano wa hili ulosema ni mkubwa sana Kiongozi na hii ina ukweli ndani yake.
 
UKAWA ni kama hawajui wanachofanya nimaigizo tu
KITENGO ndio final say wa maamuzi ya nchi

Labda wanaelewa na ndiyo maana wanasema mwaka huu wamejipanga katika kulinda kura, swala la watazilindaje wanajua wao.
 

Hao uliowataja mieleka yao hukuiona mkuu??!!
 
Nasikitika kusikia usalama wa taifa 'kitengo' mlihusika kukatwa majina ya wagombea urais ccm.Tiini matakwa ya umma.
 
Hans Kitine alikuwa mkuu wa Usalama wa Taifa akaenda chukua fomu za kugombea Urais CCM
na Agustin Mahiga alikuwa deputy wa Usalama wa Taifa
akachukua fomu CCM
What was the motive??!!!
Vipi kama ilikuwa ni colour mixing to get the secondary one. . . . .
 
Kwanini wasubiri hadi uteuzi wa Rais ndo washiriki?
why wasizuie mafisadi wote before?
au kushinikiza wafungwe jela?
Mkuu umeisoma sheria ya 1996 inyoongoza shughuli. . . . ??!!!
Unajua mtu mzima unamshauri mtaa huu sio salama kupita usiku. . . . .Akipita badala ya kuacha vijana wamkabe unaweza andaa mazingira akamwagiwa maji ya ukoko tu kesho hapiti. . . . . .Ila pia anaweza amua pita huku kavaa rain coat kabisa. . . . .
 

Hiko kitengo kipo CCM tu!?
Kitengo hakiwezi kuchagua wapinzani?
Double standards hizi.
 
Bila kitengo kuingilia kati , nchi ingekuwa pabaya kumbukeni hii n nchi ya kiafrika na bado uelewa wa wananchi sio mkubwa hivyo mafisadi kama lowasa , karamagi, kingunge, rostam, Reginald mengi yakiachiwa tuu yajifiche kwenye demokrasia nchi ingekuwa kama Congo DRC

Mnapiga tu kelele kwa kuwa mmo humu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…