OLESAIDIMU
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 19,139
- 9,574
Maturity ya chama kwenye kuongoza nchi ndio vinasababisha watu wapokezane ofisi kubwa bila shida . .. . . Tutafika huko ila kuna kazi kubwa sana ya kufanyikahapa inazungumziwa TISS kuegemea chama kimoja, ww unaleta mambo ya CIA kupanga nani aongoze nchi, democratic na republican wanabadilishana uongozi bila matatizo nyie mnakumbatia chama kimoja. maendeleo mtasubir miaka 1000
For now 'kitengo' ndo wenye final say
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka huu John Maguli tayari amekuwa na ziara za kutembelea mikoa mbalimbali kabla na toka ateuliwe na CCM kuwa mgombea urais, kuna mambo kadhaa ambayo nimechunguza na kujiuliza kama kweli CCM ilifanya uamuzi sahihi kumteua Magufuli kuwa mgombea wake waburais.
Kwa mfano
1/Wakati wa uchukuaji fomu za kuomba kuteuliwa kugombea urais ndani ya CCM, Magufuli hakuonekana sana kama ni miongoni mwa watu wanaofaa kupeperusha bendera ya CCM, hakukuwa na mshtuko wala hamasa yoyote kutoka kwa wanaCCCM au wasio wanaCCM kuhusu ugombea wa Magufuli. Tofauti kabisa na wagombea wenzake kadhaa. Hakuna mwanasiasa asiyetaka kushangiliwa au kushabikiwa, na hatuamini kabisa kuwa Magufuli hakutaka kushangiliwa au kushabikiwa bali huenda ni mvuto duni wa kisiasa ndani ya CCM au vinginevyo.
2/Hata baada ya Magufuli kuteuliwa rasmi kuwa mgombea urais wa CCM na kufanya mikutano ya Hadhara mjini Dodoma, Dar, Zanzibar na Mwanza bado hatukuona mwangwi mzito wa mwitikio wa watu.
Kwa ujumla mikutano yote hiyo ilijaa makada wa CCM wakiwa na sare zao za kijani(wengi wao walikuwepo kwenye harakati za kumshabikia Lowassa wakati wakusaka wadhamini) wakiwa na sura zenye mashaka makubwa na tabasamu za kutengeneza. Wengi wetu tulitegemea makundi makubwa sana ya watu mbalimbali hususani wasiokuwa wanaCCM.
3/Mpaka sasa hatujaona kishindo cha mtikisiko wa kisiasa kwa upande wa upinzani katika kuhofia ujio wa Magufuli katika mbio za urais mwaka huu. Japokuwa UKAWA hawajatangaza rasmi mgombea wao lakini hatuoni Presha yoyote katika kuhofia nguvu za Magufuli kisiasa.
4/Mwitikio wa Makundi makubwa ya kijamii bado uko chini sana baada ya Magufuli kuteuliwa. Mpaka sasa wingu la kisiasa limegubikwa na kukatwa kwa jina la Lowassa tu, badala ya uteuzi wa Magufuli.
Kila mtu alishuhudia namna Lowassa alivyokuwa akitikisa kila mahali alipopita wakati tu, amechukua fomu kugombea urais.
Tukio la Lowassa kutangaza nia jijini Arusha lilikuwa ni tukio kubwa sana kiasi cha kusimamisha kabisa shughuli za watu katika Miji ya Arusha, Moshi na Manyara. Lakini huwezi amini Tukio la Magufuli kuteuliwa kugombea irais na CCM na kuja Dar na Mwanza halikushtua kitu chochote katika shughuli za watu za kila siku.
Ni wakati gani Vetting inafanyika? Ni muhimu kiasi gani? Ni kwa maslahi gani na ya nini?
Wapiga kura kwa uwingi wao tunaongelea quantity, kitengo kwa uchache wao ni "Quality" based, now chagua mwenyewe unataka kiongozi wako apatikane vipi, kwa quality au quantity. Kwa kilichotokea katika kipindi cha miaka kumi iliyopita nadhani kitengo kimejifunza kazi yake na kutorudia kosa ambalo wananchi walikuwa just about kufanya! Am glad kitengo is getting back to basics!
Na hakuna anaetaka kujadili hili
huu ni mwiko mkubwa demokrasia
​Nawe upo KITENGO eenh?Hakuna demokrasia kwa vi nchi kama hivi, wananchi hawako informed kina lowasa wanawanunua kwa sh elfu kumikumi unategemea waachiwe wafanye maamuzi magumu. Waacheni usalama wafanye kazi zao, hatuwezi kuyaachia nchi magenge ya kifamilia!
Nasikitika kusikia usalama wa taifa 'kitengo' mlihusika kukatwa majina ya wagombea urais ccm.Tiini matakwa ya umma.
SOMA UZI WA The Boss https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/888264-nchi-inaendeshwa-na-kitengo.htmlNasikitika kusikia usalama wa taifa 'kitengo' mlihusika kukatwa majina ya wagombea urais ccm.Tiini matakwa ya umma.
We unafikiri edo ni mjinga kama wewe? Wewe unafikiri apson ambae ni mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa mstaafu alikuwa ana kazi gani? Watu wapo extra smart..Km kuna pahala TISS walicheza kwa ufanisi na busara ni pale walipohakikisha jina la Lowasa linakatwa.Ingekuwa enzi zile,Edo angelikwisha pata ajali siku nyngi.Hyo iko pote duniani hata Us.Hata opp. Kunyimwa ushndı ni kazi ya TISS, to be fair hauwezi kukabidhi nchi kwa watu km Mbowe.TISS ndo inasaidia kuwajengea uwezo opp na baada ya muda nadhani watawapa nafasi wakishnda.Wanaimprove kila siku na watu wenye akili wanawajoin, tutafika.
Mkuu, kuna watu wajinga sana humu
Je Kitengo kipo kikatiba?Kama jibu ni hapana mbona kina nguvu sana hadi Mzee Kingunge anakihofia?Labda Kitengo ni baadhi ya vyombo vya usalama wa Taifa ambavyo vipo very invisible but very powerful and untouchable.Mh Lowassa amekuwa Waziri Mkuu,na amekuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Bungeni,hivi hakujua nguvu ya kitengo kabla ya kutangaza nia?
Uchaguzi Mkuu ujao Ngazi ya raisi na wabunge hauna maana kwa wananchi ni kupoteza pesa za walipa kodi kwani kitengo kimeisha maliza kazi yake.
Yameanza leo??!!
Waliokuwa viongozi mbona hakuna aliyewahi kuhoji uteuzi wake??!!!
Ndio maana mi naamini hii nchi haitapiga hatua kidemokrasia wala kiuchumi hadi nafasi za kiutendaji zitakapoachwa kuongozwa kisiasa...
Usalama wa taifa, polisi, jeshi, TAKUKURU, mahakama, watendaji wa bunge, wakuu wa mashirika na taasisi za umma nk ... wote wapo affiliated kwa chama kimoja cha siasa...
Ili hali hii iweze kuondoka ni lazima wananchi wawezeshwe kukidhoofisha chama hiki kwa kukipunguzia sauti kwenye vyombo vya maamuzi kuanzia chini kabisa kwenye ngazi za halmashauri za vijiji, za wilaya na bunge...