Nchi haiwezi kuendelea kwa staili hii

Mamzalendo

JF-Expert Member
Dec 29, 2010
1,670
558
Jamani ndugu zangu kwa nini tunategemea nchi iendelee kwa staili hii, mimi mwaka jana niliomba kufungiwa maji kwenye plot yangu mwezi wa tisa mpaka sasa hamna kitu na nimelipia kila kitu nikifuatilia napigwa tarehe tu, januari wakaniambia chimba mtaro nimechimba mpaka sasa mtaro umeziba hawajaja, hivi niwafanyaje? Naongelea Kilimanjaro ambayo watu tunategemea iwe na maendeleo. Hatuwezi kuendelea kwa sababu toka mwezi wa tisa ningekuwa nimetumia maji na likawa pato kwa taifa kwa ulipaji wa bili zangu, pili ningeweza kufanya biashara zangu na kuiingizia nchi hela lakini hawa watu hawafikiri wanabaki kusema mishahara inachelewa itaendelea kuchelewa kwa sababu ya ujinga na kutotaka kufikiri. Jamani kila mtu kwa nafasi yake atoe huduma kwa wakati. Ningekuwa na uwezo ningeishtaki idara ya maji kwa hasara yote niliyopata kwa kutopata maji. Sasa hivi nimeamua kutofuatilia maana ufuatiliaji wangu hauzai matunda au mnanishauri nifanyaje jamani? Nimechoka kabisa kila siku nasikia watu wanafungiwa lakini mimi nikiuliza vipi tarehe tu! Na rushwa sitatoa hata shilingi kama ndo wanachosubiria.
 
EE bwana hayo pia yamenikuta mimi pia, nilidhani ni mji ninaoishi peke yake, kumbe hata huko, mimi nililipia kila kitu, nikachimba mtaro, sasa kila nikifuatilia ni kupigwa tarehe, kwa kweli hii nchi ni failure kila mahali.
 
Tatizo system nzima toka juu ilishaoza,kuwa tu mpole kuna siku wakipenda watakuja,ila bill huwa haichelewi.
 
Katoe hela kidogo kwa bosi wao utapata maji siku hiyo hiyo...lakini pole sana kwa usumbufu uliopata
 
Mkono mtupu haulambwi,umesahau unaishi Tanzania hakuna kinachowezekana bila kitu kidogo.
 
Katoe hela kidogo kwa bosi wao utapata maji siku hiyo hiyo...lakini pole sana kwa usumbufu uliopata

ahsante nikitoa hela tutakuwa tunawazoesha vibaya na kuwafanya wasifikiri na je wasioweza kutoa?
 
Mkono mtupu haulambwi,umesahau unaishi Tanzania hakuna kinachowezekana bila kitu kidogo.

najua ni tz lakini hapa watalamba tu mkono mtupu, kila sekta imeharibika kwa kupewa kitu kidogo, its time they learn to work without this. na nkiona wajeuri ntawafata lakini wataishia mikononi mwa takukuru.
 
Tatizo system nzima toka juu ilishaoza,kuwa tu mpole kuna siku wakipenda watakuja,ila bill huwa haichelewi.

nakubaliana na wewe yaani hadi walinzi na messengers,mfano yaani utakuta umeenda ofisi fulani ya serikali umepaki gari parking ya hizo ofisi ukitoka mlinzi anakataa kufungua geti eti hadi umpe hela ya kulinda gari yako this is extremely insane hadi umuite bosi wake atukanwe kwanza ndo anakufungulia
 
nakubaliana na wewe yaani hadi walinzi na messengers,mfano yaani utakuta umeenda ofisi fulani ya serikali umepaki gari parking ya hizo ofisi ukitoka mlinzi anakataa kufungua geti eti hadi umpe hela ya kulinda gari yako this is extremely insane hadi umuite bosi wake atukanwe kwanza ndo anakufungulia
Hii nlikua sjaiskia. Kila mtz sasa ame-adapt tabia za mbwa mwitu wene njaa na wasio na utu. Kha!
 
Back
Top Bottom