Nimepitia kumbu kumbu zangu za vyama vya upinzani nchini na kujikumbusha kuwa NCCR mageuzi walikuwa na nguvu sana miaka ya tisini wakati mheshimiwa Mrema alipohama CCM.
Tukumbuke kipindi kile mfumo wa vyama vingi ndio ulikuwa unaanza nchini lakini Mrema aliweza kujizolea umati mkubwa wa wafuasi na mimi nikiwa mmoja wao. Lakini pamoja na wafuasi wote aliokuwa nao Mheshimiwa Mrema sikuwahi kusikia mtu akilalamika kung'olewa kucha bila ganzi au kusikia vijana wakitembea na sumu mfukoni.
Lakini leo Jamaa zangu wa Chadema ambao ndio chama kikuu cha upinzani kila kukicha ni lazima usikie sarakasi za mauza uza tu.
Mara utasikia kuna kijana anatembea na sumu mfukoni katumwa na nani sijui
Mara utasikia kuna video imenaswa mkurugenzi wa Chadema anapanga mauaji na ung'oaji wa kucha
Mara utasikia wanatangaza kuwa watasimamisha nchi nzima kwa maandamano bila kibali
Na mengine meengi ambayo sasa naona hata wanachama wao wenyewe wameisha anza kuwachoka.
Hiki Chama kimekosa mwelekeo kwani wao njia pekee ya kupata attention ya wananchi ni kuitisha maandamano, kufanya vurugu na sasa kwa sababu wameona wanachi wamechoka na maandamano wameanza kunyofoa watu kucha kama tulivyoona kwenye ile video ya Lwakatare.
Nakaa najiuliza,
Hivi chadema wameshindwa kuwaambia wananchi watawafanyia nini ili wachaguliwe?
Hakuna njia nyingine za busara na amani za kujipatia umaarufu zaidi ya kusababisha uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya watu?
Chadema jaribuni kujifunza kutoka NCCR mageuzi ambao pamoja na migogoro yote waliyokuwa nayo na umaarufu walioupata hatujawahi kusikia wana vijana wanaotembea na sumu mifukoni.
Vijana inabidi mkatae kutumiwa kama misukule, kumbuka ukikamatwa na sumu mfukoni watakukana kama LUDO
Chadema ni kama time bomb, siku likiripuka wengi mtajutia muda wenu mliopoteza kucheza karata tatu
AMKENI