Nanaa
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 5,893
- 3,711
Pole sana aisee....
Mie nilikuwa nasaidia sana watu....najitoa kwenye jambo la mtu utadhani ni langu
Kuna kipindi nilupata shida nikawa nahitaji 200,000 tu kuongezea... kila nilomgusa alitoa sababu... nashukuru nilifanyikiwa kusolve ile ishu hata sijui niliisolvije...
Na matokeo menginge mengine nikaja gundua mie nikipata shida hawajitoi ila mie ndo nahangaikaaaaaaaaaaaaaaaa
hiyo ilinifanya nikapinguza hata idadi ya marafiki...
Na kabla sijamsaidia mtu najiuliza mara mbili....je nikipata tatizo hiyo mtu huwa anajitoa kiasi gani kwangu.......
Yaani ilinifanya nijifunze ubandidu.....
Yani nakwambia me nimerithi....Bi mkubwa wangu alikuwa anajitoa sanaaa...yani ile mtu akipata tatizo ye kashafika, home hapakauki wageni, watu wakiwa na kesi huko wanakuja atawahangaikia mpaka yanaisha, akiambiwa tatizo hat saa ngapi atatoka...halafu dizaini kama walikuwa wananusa..akiwa na hela tu, watu hao na matatizo...
Sasa mzee alikuwa bandidu, hapendi zile mishe...basi full kugombana..lakini bi mkubwa hajali...Mzee akawa anamwambia nawajua hawa hawana shukrani...Bi mkubwa wapi...ndo kwanza kageuka shirika la misaada...
Mzee akaja akafariki...Bi mkubwa yupo ndani eda, hana mishe, familia zetu zenyewe hizi za kimasikini...hali tete...tulikumbwa na njaa kama tuma somalia au Sudan....kwani ndo tulimuona mtu?
Wale ndugu walokuwa wanamiminika walikata...hata simu hawapigi...
Kuna mambo mengi yalitokea hapo kati hadi nikatamani kwenda kumfufua yule mzee nimwambie ulisema kweli...
Maisha yakasonga tukasimama tena....Kwani ndo kakoma? Ndo kwanzaaaa analiendeleza....yani hadi muda mwingine namkalisha chini namkumbusha mabaya tulofanyiwa...lakini wapiiii....!
Ndo kwanza najibiwa "Atanilipia Mungu"...