Navunja ndoa ya mtu!!!!

Navunja ndoa ya mtu!!!!

Mvaa Tai,

Naomba ninukuu maneno yako:

Wadau mwenzenu nipo kwenye wakati mgumu sana psychologicaly, kuna dada anataka kuachika kwasababu yangu ilihali hana kosa lolote....Ishu iko hivi Kuna dada(mke wa mtu) nipo naye karibu sana kikazi..."

Nimeweka msisitizo kwenye hiyo sentensi na hasa neno 'Ukaribu sana'. Turudi kwenye mada halisi, kutokana na maneno yako inaonekana 'huo ukaribu sana' si wa kawaida katika macho ya binadamu. Kumbuka huyo ni mke wa mtu na nyiye mmezungukwa na jamii. Mtu hawezi mnyima mtu mwingine neno. Yaonyesha mume wa huyo dada kisha fikishiwa maneno ya huo ukaribu wenu. Angalia sana bwana mdogo mambo ya kujishebedua na wake za watu utafikiri mko shule ya sekondari yatakutokea puani. Pili, mtu yupo likizo, ukiw unajua maana ya likizo huwezi kurupuka na kumpigia mtu eti 'i am seeking some clarification', je hiyo ofisi yenu haina watu wengine wenyekuweza kutoa ufafanuzi? matendo mzee, matendo yako yanaonyesha mikono yako si misafi pengine bila kujua kwamba wewe si msafi.

Tafakari, chukua hatua!!

Wasalaam,

Shadow.
 
Mkuu napata wasiwasi kama kweli umeoa ama kama kweli hiki kisa kimekukuta??...Kama alivyosema Speedy inaonyesha hujali kilichotokea na unachukulia for granted...Binafsi huwezi nipangia jinsi ya kuishi na mke wangu na jinsi ya kupokea simu zake...nani alikwambia kumuamini mkeo/mumeo ni kutochungulia simu yake??...Nyie kujua kuwa nisimuamini mkewangu inaweza isinikere mradi mie naona ndio njia sahihi ya kumaintain ndoa yangu....kama kweli imekutokea please be eyes, it wanna get hot soon!!!!

Waweza kuwa sahihi, lakini Kwanini upokee simu ya mkeo ilihali yupo jirani huoni kwamba unaichoresha sana ndoa yako kwamba hamuaminiani?
 
Last edited by a moderator:
Mchukue rafiki yako, nenda nae ofisini kwa jamaa, ukiwa mapokezi mwenzio ndo aseme anahitaji kumuona huyo jamaa, mkifanikiwa kumuona muelezee kinagaubaga.

Tafuta rafiki yake wa karibu muelezee akuelewe, kisha nenda nae kwa jamaa ukamuelezee kwa kushirikiana na huyo rafiki yake. Akikataa kabisa kukusikiliza basi huyo jamaa alikuwa anatafuta upenyo wa kumwacha mkewe
 
Waweza kuwa sahihi, lakini Kwanini upokee simu ya mkeo ilihali yupo jirani huoni kwamba unaichoresha sana ndoa yako kwamba hamuaminiani?

hapa kaka nimetofautiana nawewe!kwanini nipokee simu ya mke wangu?kuna kitu nadhani kinaendelea hujataka kutuambia,haiwezekani umlaumu mwanaume mwenzako kwa kupnkea simu ya mke wake!
 
Daah, umenikumbusha mbali kweli.....ila sina hata cha kushauri manake sijui hata liliishaje.

Kwa kifupi, yakitengemaa, kaa mbali na huyo mwali, na wala usimpigie simu asipokuwepo ofisini hata kama ni issue za kikazi. Potelea mbali, acha tu hilo zege lilale utamuuliza unachotaka kuuliza akifika ofisini.
 
Mimi nadhani hutakiwi kukaa kimya, cha msingi waendee au watafute wazazi wa mume na uwaeleze ishu imekaaje na wao wakusaidie kuzumngumza na mtoto wao. Kama si hao anaweza akawa shangazi yake au ndugu yeyote anayemuheshimu. Wakati unayafanya haya hakikisha mke wako anajuwa unachofanya na mwisho wa siku mkutanishwe wewe, mkeo, jamaa na mkewe pamoja na ndugu wa mume alitakayehusika kuanza kuongea na huyo jamaa
umeongea point ya maana sana
 
Alafu mbona muheshimiwa Mvaa Tai unaonekana kujiDefence ww na hyo mke wa mtu?Inaonesha unaijua ndoa yao vizur.Lipo tatizo kbs naliona kwa macho ya nyama.........huyo mume anayo haki yakumtimua hyo.
 
Ishu ni hiyo ya mtoto kupiga simu kwa bahati mbaya.jamaa lazima awaze we ndo ulipiga simu na baada ya yeye kupokea ukakaa kimya.la msingi usijihusishe na ugomvi coz jamaa tayari anawaza unammegea wife so anaona unamuonesha dharau
 
Alafu mbona muheshimiwa Mvaa Tai unaonekana kujiDefence ww na hyo mke wa mtu?Inaonesha unaijua ndoa yao vizur.Lipo tatizo kbs naliona kwa macho ya nyama.........huyo mume anayo haki yakumtimua hyo.

jamaa katafuna hapa anatuzingua.Kwanini anjitetea sana. Hivi watu wanadhan kuachana ni kazi ndogo. Yaan hapo ujue mme moyo ushavurugika toka zaman. Hapa mimi sina cha kushauri kwa sabab jamaa mwenyewe naona anajitetea sana na siku zote mwizi huwa anajitetea Saana
 
na wewe kwa upande mwengine umekosea,kama unajua unaefanya nae kazi yupo katika ndoa,time za kuwasiliana mambo ya kikazi ni time za kazi tu.waume wengine sio waelewa na wako wake wengine sio waelewa pia.kuna dada mmoja alimporomoshea matusi msichana mwengine kwa issue kama hiyo na hawakuwa wapenzi zaidi ya masuala ya kikazi tu.na huyo mke baa huwa wanaenda pamoja na mume wake.kila sehemu wako pamoja ana wivu balaa.usione watu wana smile maofisini utani mwingi,wengine wakiingia majumbani mwao ni moto tu.
 
jamaa katafuna hapa anatuzingua.Kwanini anjitetea sana. Hivi watu wanadhan kuachana ni kazi ndogo. Yaan hapo ujue mme moyo ushavurugika toka zaman. Hapa mimi sina cha kushauri kwa sabab jamaa mwenyewe naona anajitetea sana na siku zote mwizi huwa anajitetea Saana

Teh teh teh kaz kwel kwel.....hyo ni dharau kwel kwa mume wa watu.
 
Ishu ni hiyo ya mtoto kupiga simu kwa bahati mbaya.jamaa lazima awaze we ndo ulipiga simu na baada ya yeye kupokea ukakaa kimya.la msingi usijihusishe na ugomvi coz jamaa tayari anawaza unammegea wife so anaona unamuonesha dharau

yani eti mtoto alipga simu bahati mbaya!inawezekana kweli lakini hivi kweli inaingia akilini?kirahisirahisi tu? Aliposema mtoto alipga simu ndipo nikapata picha there's smth behind going on! Kazi ni muhimu sana kwa yuld dada lakini kuwa 'KARIBU SANA' na mke wa mtu mi siafiki kabisa hilo jambo!mke wa mtu ni sumu, bora kutafta msichana yeyote asiye mke wa mtu ndo uwe 'KARIBU SANA' naye..mi namshauri aache kabisa kuwasiliana na huyu dada pia aripoti police.
 
ni dhahiri kwa vigezo vya jamaa,umevuka mpaka wa mawasiliano na mkewe!fanya kila uwezalo uonane nae na umuombe msamaha kwa hilo na kusababisha yote yaliyotokea.kisha ndio ulete hizo explanations zako baada ya kuomba msamaha!
hata ukitoa taarifa polisi mwenye lake moyoni anaweza fanya;kwani wafanya uhalifu hawajui kuna polisi?lingine,polisi wanachunguzaga nguvu za giza?
kamuombe jamaa msamaha,kwa faida yako binafsi na familia yako,sio kwa kuokoa ndoa ya huyo dada.
 
Ndo maana dada zetu wanakimbilia kutoa matangazo gazetini ya kutafuta wazungu!

Jamaa hana akili. Kama huyo dada huwa amchiti, je siku akianza kumchiti atamlaumu nani?
 
Ndo maana dada zetu wanakimbilia kutoa matangazo gazetini ya kutafuta wazungu!

Jamaa hana akili. Kama huyo dada huwa amchiti, je siku akianza kumchiti atamlaumu nani?

Kwakuwa Wazungu hawana moyo au?
 
Matumizi ya simu za mkononi/phone manners
Una shauriwa kila unavo piga jitambulishe vema/full introduction
Kama ni simu ya kazi eleza vizuri lengo lako kama ni zaidi ya muda wa kazi.
Chunga saana jinsi unavo toa sauti yako hapa usichanganye na ile ya kimahaba.
Muda pia ni muhimu kuangalia kama ni baada ya kazi kwann upige muda huo?na kama jinsia tofauti basi tuma ujumbe unaojieleza ili hata mweza akiona asiwe na wasiwasi na kama ni weekend pia angalia saana
Piga simu mara moja tu!ukipiga mara nyingi itachukuliwa kama unamlazimisha apokee! Maisha ya ndoa ni magumu saana huyo bwana anaweza akawa amefanya utafiti mdogo tu na akaja na majibu hayo pia na kama wewe unafanya kazi kwa karibu na huyo dada ilibiidi pia umfahamu kwa karibu mumewe!hivyo basi kaa nae mbali wata suruhisha na watamalizana wenyewe
 
too much coincidence. .

Kwani lazima uwasialiane naye? Si bora kazi zilale?

Kwa wanawake walioolewa mme ndo ajira ya kwanza.

Na kumbuka 'mke' mtamu
 
Back
Top Bottom