Pole sana haya yanatokea sana katika kazi hasa hizi za kuajiriwa, pole sana. Mumewe anatakiwa kuwa mwelewa ingawa katika mapenzi ni kawaida kuhisi wizi wizi tu na sijui kwa nini mara nyingi wanaume walio wengi hawapendi kuwa na imani na wake zao hasa walioajiriwa...
Ushauri, ongea na huyo mwanamke akuunganishe na rafiki wa karibu sana na jamaa na hata ikibidi wazazi wa mwanaume kama wapo au nduguze, ili uende ukaeleze kilichotokea na ikibidi uende na mkeo itakuongezea uzito na kuaminika katika hili, na with time hasira ya mume itapungua utaweza kukutanishwa naye wewe mkewe na mkeo umweleze kisa kizima, ili kama anayo sababu ya kumwacha mkewe sababu isiwe wewe bali sababu zingine azijuazo yeye mume...
Pole sana maana hata mimi ilishanitokea nikatafuta njia zote hadi nikakutana na mume wa huyo dada tukayamaliza, lakini yangu haikutoka na simu bali mdada fulani aliyekuwa amekaribishwa nyumbani kwa huyu mwingine (wadada wote nilikuwa nafanya nao kazi) ila huyu mmoja alikuwa mgeni mji ule akakaribishwa ili ajipange kupata kwake kumbe nadhani akamtani mume wa mwenzie akawa anatafuta namna ya kupata kwa kupita uwongo wa kumhusisha mkewe na mimi..