Natembea na mume wa mtu

Natembea na mume wa mtu

bibie hamisa jipange wee yako baridi tu huipati joto ng'ooooo hao ndo wanaume ukiwaendekeza miaka yote mpaka unakuwa bibi we umekwa kinyumba na mume wa mtu
hakuna kitu kizuri kama kuitwa mke wa fulan (mrs)
 
Sasa wewe dada yangu unaona kuna future kweli hapo, tayari ni mume wa mtu na tayari ana mtoto wewe umo tu.Angalia usije ukashawishika kwenda kwa mganga kumuua mke wa ndoa wa huyo bwana ama angalia usije ukahatarisha ndoa ya huyo ndugu, mwonee huruma mwanamke mwenzako na mwonee huruma mtoto maana ndoa ikiharibika yeye ndo atakaeumia na kuwa mtoto wa mitaani.
Mwombe Mungu atakupa mwanaume mzuri atakaekufaa maishani na kukusahaulisha yote uliyoyapitia huko nyuma.Nakuambia hapo hakuna future kwa huyo bwana maana anakutumia kama kiburudisho chake tu.Tulizana maana kuwa boyfriend wako wa kwanza ama mwanamume kukutoa virgin sio kusema eti hawezi kusahauliwa.
 
adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie. Vijana tuko wengi mjini na kazi zetu ila hatuonekani, loh!
Mko wapi hamuonekani, mtaani tunawaona akina mzabzab wa gegedaji tu ndo wamejaa, real men are hard to find and trace
 
Last edited by a moderator:
Ungejua uchungu wa mke/mume kamwe ungejua ninachoelezea hapa asikwambie mtu mume/mke wa mtu ni sumu hata mandiko ya dini yanakemea swala hili.
 
bibie hamisa jipange wee yako baridi tu huipati joto ng'ooooo hao ndo wanaume ukiwaendekeza miaka yote mpaka unakuwa bibi we umekwa kinyumba na mume wa mtu
hakuna kitu kizuri kama kuitwa mke wa fulan (mrs)

Kweli wanaume ukiwaendekeza utadoda, yani mwanaume mbele ya K atafanya lolote, hapo ameona K ya bure ataongea yooote. Kama alikupenda kwanini asingefanya juu chini akutafute hadi akupate?kama aliweza kupata taarifa kwamba una mtu how come asipate taarifa kuhusu ulipo? au wakati unamuona anatafuta suti si angevunja uchumba ili akuoe wewe kama kweli alikupenda wewe kuliko huyu mkewe......wanawake tusipoangalia wanaume watatumia mwavuli wa neno love kutugegeda kila siku na kutupotezea muda!! amka tafuta wako
 
Pole sana kwa kuingia kwenye maji ambayo hujayajui kina chake cha baadaye.Mapenzi hayana siri, ipo siku mtajisahau mkewe atajua.natamani huyo mke atoke nje ya ndoa ili awaletee kaugonjwa kasiko na tiba, hapo ndio utajua kama uache au uendelee na kamchezo hako.Huyo jamaa anakuzibia usiolewe, na umri unaenda hivyo, endelea kuponda raha, kufa kwaja.
Nafikiri unabidi ushindane na nafsi yako, na ukipata mpenzi wako mwenyewe utakuwa na amani na utamsahau huyu jamaa.kwanza mapenzi haya huna uhuru, kila wakati unahofu ya kukutwa.kwanini ujitese na wanaume hawajaisha duniani?Bado unamuda wa kuamua kabla mambo hayakuendea vibaya.
 
Mungu anasema, ''Ndoa na iheshimiwe na watu wote"...Pia, alichokiunga yeye Mwanadamu asikitenganishe...kwa ile kauli yake ya kwanza....wewe na huyo mume wa mtu mnavunja amri ya Mungu aliyokataza uzinzi...lakini pia hamuheshimu ndoa aliyoifunga yeye Mungu kupitia watumishi wake hapa duniani....aidha ukiendelea, utapelekea kutenganisha alichokiunga Mungu...huku ameshakataza....unajitafutia matatizo, na kama ulivyosema, Mke wa huyo jamaa ni Innocent..hivyo Mlipizi wake atakuwa Mungu Pekee, na Mungu hulipiza hapa hapa duniani...mana anasema, atapitiliza na kuadhibu hata kizazi cha tatu na cha nne cha waliomkosea...manake dada, unaweza pata pigo wewe, uzao wako, uzao wa wanao...na uzao wa wajukuu zako...kisa hizo raha za muda mchache unazopata sasahivi.....Alafu una umri mdogo sana, mtoto wa mwaka 1986?? mmh, achana naye,tubu na Muombe Mungu akufutie makosa na adhabu aliyoipanga.na akutafutie wa kwako...mana unapoelekea, unaweza jikuta unakosa wa kuwa naye hadi kufa kwako...
 
Pole sana kwa kuingia kwenye maji ambayo hujayajui kina chake cha baadaye.Mapenzi hayana siri, ipo siku mtajisahau mkewe atajua.natamani huyo mke atoke nje ya ndoa ili awaletee kaugonjwa kasiko na tiba, hapo ndio utajua kama uache au uendelee na kamchezo hako.Huyo jamaa anakuzibia usiolewe, na umri unaenda hivyo, endelea kuponda raha, kufa kwaja.
Nafikiri unabidi ushindane na nafsi yako, na ukipata mpenzi wako mwenyewe utakuwa na amani na utamsahau huyu jamaa.kwanza mapenzi haya huna uhuru, kila wakati unahofu ya kukutwa.kwanini ujitese na wanaume hawajaisha duniani?Bado unamuda wa kuamua kabla mambo hayakuendea vibaya.

Mwenzako anakufanya taulo la gesti, anakutumia kila akijiskia kuja gesti, anakuchakaza weee wakati ana taulo lake jipya, safiii sandukuni
 
Siyo lazima awe muislam. Kwani wakristo wangapi wana mke zaidi ya mmoja? Kama vipi nyie halalisheni tu, mkafunge ndoa ya bomani. Sioni ubaya katika hilo. Hii habari ya mke mmoja ni sheria ya kanisa tu, haina madhara yoyote kiimani. Kwa uelewa wangu wa biblia, ni askofu tu ndiyo amezuiwa kuoa mke zaidi ya mmoja.

Na wazee wa kanisa...!
 
Mrembo by Nature na Katungunya nimewapenda bure leo...i can see future!!!

In other news, kuna mdau hapa aliwahi kusema, "Ukichoka kufanya siri fumaniwa"
 
Last edited by a moderator:
Ni kurudia tu maneno yale yale "mume wa mtu ni hatari" ndg yangu. Trust me, u are courting a disaster! Huu si utabiri bali ni fact...Usisubiri kuja kutupa taarifa hapa kuwa yamekukuta makubwa zaidi.
 
we mwache mwenzio kapenda kuwa uhawara kugegedwa mchana tu usiku mpaka mume asingizie safari tena na mwenzie anacheo cha mrs yeye hawara a.k.a kimada, nyumba ndogo, kipozeo na kadhalika na usomi wake wote huo kipindi cha baridi anapopata shida wakati mwenzie kakumbatia hata baridi haijui
njoo kwangu mimi mwenyewe single and searching check avatar mwanamke wa kitz haswa
jamani huyo dada musimlaumu yeye hana kosa kosa liko kwa mume inakuaje leo mwanamme una mke na mtoto uende kutafuta hawara uyo dada ilo jambo lina muuma ila huyo mwaume ni shetani no 1 na kushauri dada uyo jamaa achana nae atakupotezea mda wako bure hata mwisho atakupa mimba utaenda kutua mpaka mwisho utachoka jijali dada angu
mimi mwenyewe kuna mke wa mtu ana nizimia sana lakini toka anionyeshe dalili za kunitega hata salam simpî ilo jambo linauma sana mume wa mtu au mke wa mtu kutembea nae noma na huyo jamaa atalipwa hapa hapa duniani leo yupo kwako hapo usiku huo huo kule kwake vile vile anamegewa.
 
I could totally turn Shaaban Robert on this, with classic Swahili morality.

Or just psychoanalyze this as a subconscious suicidal tendency that ought to be encouraged to perfect evolution.

And feel serene with apathetic equanimity, either way.
 
Back
Top Bottom