Natembea na mume wa mtu

Natembea na mume wa mtu

Nikupe kongole kuwa kwanza umetambua kuwa hicho unachozidi kukifanya ni kosa kubwa na haifai kabisa kutembea na mume wa mtu. Nisikuchoshe, that's is called infatuation. Achana naye, kubali ukweli huyo si wako tena siyo wako tena mama it's over and too late. Sina maneno mazuri zaidi ya hayo. Usidanganyike na maneno eti "ninazidi ku fall zaidi kwake, eti yeye ni mtamu sana. Mandhari sasa umeweka wazi kwa hii thread yako yenye ID fake mkewe kajua na anakutafutia dawa kali ya kukufundisha. Sikutishi japo ukweli unauma. Baadae watu kama nyie mnakujaga kupata shida huko mbeleni mkisahau matatizo yameanzia wapi. Mfano: kutopata mimba, kupata mimba na kutoka, kuzaa na mtoto kufariki; mikosi kwenye familia, maradhi kila kukicha. Haya "asiyesikia la mkuu...."
 
Sisi wanaume mwanamke anayekuzalia mtoto tena wa kwanza huyo ndiye hunasa kwanza ktk akili zetu for the rest of our lives. Wengine tutawakumbuka sababu ya sex nzuri.
Kwa kesi yako, jamaa kwa sasa anakutumia kukidhi haja zake kwa mgongo wa bado anakupenda ila mwisho wa siku ana mke na mtoto. Fungua macho, anakupotezea muda. Itafika mahali option yako pekee itakuwa ni kujilipua kwa mwanaume yoyote ili tu upate mtoto toka kwa mwanaume mwenye mtoto tayari sababu wakati wa kufanya maamuzi magumu ulizembea.
Achana na jamaa na fanya maamuzi sahihi tafuta mme sahihi. Mtangulize Mungu na jiweke ktk mazingira ambayo waume wenye hofu na Mungu wanapatikana.
 
Back
Top Bottom