Elections 2010 Natamani sana mtu akanushe mambo haya kiuhalisia

Tuma ujumbe huu kwa watu 50 thanks

 
Last edited by a moderator:
Mkuu, hapa umeniwahi, nimesoma mara mbili nikajiuliza, ni mimi tu naona kama huu ni upupu au?
Kama kawaida...........hawasomi hawa!, hii ameinyofoa kwa document za ba**a wake alizofojiwa na wasaidizi wake kwa ajili ya kampeni.............2+2 = 22,

uu UJUHA ndo tusioutaka..........tandaleone and company = 8 X 8 - 64 = ?? weka jibu mwenyewe!!!

Nakusikitikia sana kwa upofu wa kujitakia ndugu.Ila takwimu zipo wazi na bajo hujajibu swali langu la msingi la post hii.
 
No one knows.Ila niko sawa.Hivi JK miaka mitano hajafanya lolote?Weka unafiki pembeni.Niambie ukweli
Amefanya mambo makubwa sana ktk nchi hii kwa kipindi chake cha miaka mitano kama ifuatavyo:-

  1. Kufumbia macho wizi mkubwa wa fedha za umma.
  2. Matumizi makubwa (yenye hati chafu) nje ya bajeti,
  3. Kuingiza familia yake ktk mfumo wa dola
  4. kuridhia waziri wake kuingia mikataba ya kitaifa hotelini ugenini.
  5. kuwaachia majambazi wa EPA baada ya kurudisha walichoiba walipotishiwa na DOLA
  6. Kutofanya homework yake vyema kuhusu chanzo cha umaskini wa watanzania.
  7. Ikulu yake kutumia pesa nyingi kwa ukarabati usioonekana.
yapo mengi ndugu yangu nafasi haitoshi
 
World Development indocators 2010 ina data za Tanzania ambazo zinakaribiana na hizo lakini inaishia mwaka 2008 hata zile za kwenye Poverty and Development Report 2009 zinaishia 2008, sasa hizi za 2009 na 2010 zimepatikana wapi na lini, je tayari tuna Tanzania HIV/ AIDS and malaria indicator survey ya 2009/ 2010, Tanzania Atlas of HIV/AIDS indicators 2009 - 2010, Poverty and Human Development Report 2010, Annual Health Statistical Abstract 2010? Ni BEST ndio ya 2010 ipo tayari ambayo inasema Pupil Qualified Teacher Ratio ni 1:25 lakini kwenye shule binafsi ni 1:37 lakini kwenye public schools wamebaki kimya ambako hali ni mbaya. Kama ni projections bora tuambiwe. Je, ukiangalia hizo statistics against our population picha hiko vipi? Kama Zahanati zimejengwa nyingi na zina all necessary resources bajaji 400 za nini kwa wamama wajawazito? Kama hizi statistics ni za kweli, je kwa nini Naomi Campbell alilia sana dada wa watu kukuta hali ya wodi ya wazazi pale Amana hospital?

Kwa kifupi data hizi zimechakachuliwa na zile zenye kuonesha uozo hazijatolewa kama ratio ya mwalimu na wanafunzi kwa shule za serikali ukoje wakati standard ni 1:25. Ukusanyaji na utoaji taarifa ni mbovu serikalini na hawataki kukosolewa mambo waliyoficha kwenye vitabu vyao vya takwimu.

Hivi kupungua kwa maambukizi ya ukimwi nako ni juhudi ya serikali au mtu binafsi? Vyandarua sio pesa ya wamarekani kweli au ni ya kwetu? Juzi tu kuna mtafiti pale Muhimbili amegundua vyandarua vyenye dawa vinakaa na dawa hiyo kwa takribani siku tano tu na dawa kuishiwa nguvu wala sio miaka mitano!

Kwenye research kuna data na information. Data ni zile namba au takwimu bila maana na information ni zile takwimu zinazotolewa maelezo kama implications ya hizo data, mfano, data hizo inawiana na pato la taifa, idadi ya watanzania, pesa zinazopotea, matumizi mabaya, vipaumbele, n.k. Kwa serikali yenye umri karibu miaka 50 ni aibu kutoa takwimu za chini sana kama hizo! Na je malengo yamefikiwa kwa asilimia kubwa, maanake sio kutoa tu mitakwimu ambayo hayana malengo, sasa sijui unapimaje mafanikio!

Hivi mtu mwenye akili timamu unategemeaje upinzani uje na takwimu jinsi ilivyohudumia wananchi bila kuwa na serikali? MKUKUTA yenyewe ime-borrow MDGs. Hivi mpaka waje akina Bush ndio tuwe na vyandarua jamani!

Mfano, wauguzi kutoka 18,000 mpaka 23,00 kutoka mwaka 2005 mpaka 2010 kuna ongezeko la wauguzi 5,000 sawa na wauguzi 800/ 1000 kila mwaka (nashindwa hata kugawa sijui kwa miaka 6 au 5 ila nime-round up figures). Je, hayo ndio yalikuwa malengo katika mwaka 2005? Je, ongezeko hilo linaendana na mahitaji ya idadi ya watu kila mwaka? Hivi standard ratio (international one) ni muuguzi mmoja wagonjwa wangapi kwa siku? Sisi ratio yetu iko vipi?

Maendeleo uwekewa malengo halafu mafanikio yake upimwa kutokana na malengo yaliyoweka hiyo ndio serikali ya Chadema chini ya Rais Dr. Slaa na sio ya CCM chini ya Rais JK na watakaofuata!!!!!!!
 
Utoaji wa huduma za Afya uliendelea kuboreshwa kwa kiasi kikubwa na kuleta
mafanikio yafuatayo:-
(a) Kutoka mwaka 2005 hadi 2009, jumla ya zahanati 464, vituo vya afya 98
na nyumba za waganga 394 zilijengwa.
(b) Zahanati 1,037, vituo vya afya 285 na hospitali 112 zimekarabatiwa.
(c) Zahanati zimeongezeka kutoka 4,679 mwaka 2006 hadi 5,422 mwaka
2009.
(d) Vituo vya afya vimeongezeka kutoka 526 hadi kufikia 663 mwaka 2009.
(e) Idadi ya Madaktari imeongezeka kutoka 3,528 mwaka 2005 hadi 4,502
mwaka 2010. Vile vile idadi ya Madaktari Wasaidizi imeongezeka kutoka
9,028 hadi 14,017 katika kipindi hicho hicho.
(f) Idadi ya Wauguzi na Wakunga imeongezeka kutoka 18,123 mwaka 2005
hadi 23,886 mwaka 2010.
(g) Chanjo ya watoto dhidi ya kifua kikuu, polio, kifaduro, pepopunda, donda
koo na homa ya ini iliongezeka kutoka watoto 1,243,388 mwaka 2005
hadi 1,356,421 mwaka 2009. Aidha, watoto waliopatiwa chanjo ya surua
imeongezeka kutoka 1,267,716 hadi 1,455,100 katika kipindi hicho hicho.
(h) Katika kuzuia na kudhibiti malaria Tanzania Bara vyandarua 9,000,000
vyenye viuatilifu vimegawiwa kwa watoto wenye umri wa miaka 5 mwaka
2009/2010 bila malipo. Aidha, vyandarua 4,200,000 vya hati punguzo
viliuzwa kwa mama wajawazito.
(i) Vifo vya watoto chini ya miaka 5 vimepungua kutoka 158 kwa kila 1000
mwaka 2005 hadi 75 kwa kila 1000 mwaka 2010.
(j) Aidha, katika kuleta ufanisi wa huduma za afya, mashine za kuchunguza
damu, uwezo wa figo na ini pamoja na mashine za X-Ray zimewekwa
katika kila hospitali ya wilaya na huduma za maabara zimeimarishwa.
(k) Kitengo cha magonjwa ya moyo kimeanzishwa na upasuaji unafanyika
nchini. Aidha, mashine 7 za kusafisha figo zimefungwa na hivyo
kuwezesha usafishaji wa figo kufanyika hapa nchini.
(l) Maambukizi ya UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 7 na kufikia asilimia​


Kaka hapa hakuna wa kukuunga mkono hata kwa moja. Zaidi utaambiwa ni kampeni za kikwete hizo ila sijaona zikiitwa kampeni za lipuimba au slaa. Tuombe mungu atufikishe fainali hapo kwenye uchaguzi. Nchi ya Tanzania ni ya watanzania. Na watanzania ndo watakaoamua ni nani anafaa kuwaongoza na si vinginevyo bila ya kujali vitisho na migandamizo kutoka pande zozote zile. Hakuna mtanzania atakayedanganyika katika kupiga kura, bali ni utashi wake ndo utamfanya amchague anayeona anafaa.
 
mtu wa pwani- waandishi wetu wengi wa sasa wanatokana na jamii yenye elimu duni kutokana na serikali ya ccm hivyo uchambuzi wao pia una walakini na pia wana uwezo mdogo sana wa kupambanua mambo. Wengi wanafaa sana kwa magazeti ya udaku tu!!
 
Kaka hapa hakuna wa kukuunga mkono hata kwa moja. Zaidi utaambiwa ni kampeni za kikwete hizo ila sijaona zikiitwa kampeni za lipuimba au slaa. Tuombe mungu atufikishe fainali hapo kwenye uchaguzi. Nchi ya Tanzania ni ya watanzania. Na watanzania ndo watakaoamua ni nani anafaa kuwaongoza na si vinginevyo bila ya kujali vitisho na migandamizo kutoka pande zozote zile. Hakuna mtanzania atakayedanganyika katika kupiga kura, bali ni utashi wake ndo utamfanya amchague anayeona anafaa.

Wenye macho wanaona kaka.Na comments zao zinawahukumu.Huwezi kuwa na serikali madarakani miaka mitano isifanye chochote kabisa na watu wakaendelea na kazi zao kama kawaida.Tumezidi unafiki!!!Mtaji nadhani.
 
Natamani sana mtu akanushe mambo haya kiuhalisia
Utoaji wa huduma za Afya uliendelea kuboreshwa kwa kiasi kikubwa na kuleta
mafanikio yafuatayo:-
(a) Kutoka mwaka 2005 hadi 2009, jumla ya zahanati 464, vituo vya afya 98
na nyumba za waganga 394 zilijengwa.
(b) Zahanati 1,037, vituo vya afya 285 na hospitali 112 zimekarabatiwa.
(c) Zahanati zimeongezeka kutoka 4,679 mwaka 2006 hadi 5,422 mwaka
2009.
(d) Vituo vya afya vimeongezeka kutoka 526 hadi kufikia 663 mwaka 2009.
(e) Idadi ya Madaktari imeongezeka kutoka 3,528 mwaka 2005 hadi 4,502
mwaka 2010. Vile vile idadi ya Madaktari Wasaidizi imeongezeka kutoka
9,028 hadi 14,017 katika kipindi hicho hicho.
(f) Idadi ya Wauguzi na Wakunga imeongezeka kutoka 18,123 mwaka 2005
hadi 23,886 mwaka 2010.
(g) Chanjo ya watoto dhidi ya kifua kikuu, polio, kifaduro, pepopunda, donda
koo na homa ya ini iliongezeka kutoka watoto 1,243,388 mwaka 2005
hadi 1,356,421 mwaka 2009. Aidha, watoto waliopatiwa chanjo ya surua
imeongezeka kutoka 1,267,716 hadi 1,455,100 katika kipindi hicho hicho.
(h) Katika kuzuia na kudhibiti malaria Tanzania Bara vyandarua 9,000,000
vyenye viuatilifu vimegawiwa kwa watoto wenye umri wa miaka 5 mwaka
2009/2010 bila malipo. Aidha, vyandarua 4,200,000 vya hati punguzo
viliuzwa kwa mama wajawazito.
(i) Vifo vya watoto chini ya miaka 5 vimepungua kutoka 158 kwa kila 1000
mwaka 2005 hadi 75 kwa kila 1000 mwaka 2010.
(j) Aidha, katika kuleta ufanisi wa huduma za afya, mashine za kuchunguza
damu, uwezo wa figo na ini pamoja na mashine za X-Ray zimewekwa
katika kila hospitali ya wilaya na huduma za maabara zimeimarishwa.
(k) Kitengo cha magonjwa ya moyo kimeanzishwa na upasuaji unafanyika
nchini. Aidha, mashine 7 za kusafisha figo zimefungwa na hivyo
kuwezesha usafishaji wa figo kufanyika hapa nchini.
(l) Maambukizi ya UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 7 na kufikia asilimia


Nafikiri unapotaka kupima utendaji kazi wa mtu ni lazima uangalie ni kiasi gani cha kazi alichopaswa kufanya na kile alichokifanya katika wakati usika.Itakuwa ni ujinga kusema,kwa mfano, tumejenga shule 3000 bila kusema ni shule ngapi ulizopaswa kujenga katika kipindi hicho!unaweza kujenga shule 3000 kati ya shule 30,000 nilizopaswa kujenga.Je hapo naweza kujisifu kuwa nimejenga shule nyingi sana kwa mfano huu?
Acheni kutufanya wajinga,huu ni wakati wa mabadiliko!​

 
mtu wa pwani- waandishi wetu wengi wa sasa wanatokana na jamii yenye elimu duni kutokana na serikali ya ccm hivyo uchambuzi wao pia una walakini na pia wana uwezo mdogo sana wa kupambanua mambo. Wengi wanafaa sana kwa magazeti ya udaku tu!!

Huna substantial argument brother.
 
Mh Tandale Ongezea Temeke/Mwananyamala hospital idadi ya wagonjwa kwa kila kitanda imeongezeka toka mgonjwa mmoja kwenda wawili mpka watatu
 
naomba utapatie data zilizokuwa kwenye ilani ya ccm ili tulinganishe bajeti na uhalisia uliopo,
yaani useme ccm waliahidi kujenga zahanati 20 ila wamejenga 50, pia utupatie na gharama halisi iliyotumika
kujenga zahanati hizo na utueleze ni kiasi gani cha pesa tanzania inapoteza kwa ufisadi, hapo tutatoa
uchambuzi makini.....
 
naomba utapatie data zilizokuwa kwenye ilani ya ccm ili tulinganishe bajeti na uhalisia uliopo,
yaani useme ccm waliahidi kujenga zahanati 20 ila wamejenga 50, pia utupatie na gharama halisi iliyotumika
kujenga zahanati hizo na utueleze ni kiasi gani cha pesa tanzania inapoteza kwa ufisadi, hapo tutatoa
uchambuzi makini.....

Ilani ya CCM unajua pa kuipata hapa online?
 
Amefanya mambo makubwa sana ktk nchi hii kwa kipindi chake cha miaka mitano kama ifuatavyo:-

  1. Kufumbia macho wizi mkubwa wa fedha za umma.
  2. Matumizi makubwa (yenye hati chafu) nje ya bajeti,
  3. Kuingiza familia yake ktk mfumo wa dola
  4. kuridhia waziri wake kuingia mikataba ya kitaifa hotelini ugenini.
  5. kuwaachia majambazi wa EPA baada ya kurudisha walichoiba walipotishiwa na DOLA
  6. Kutofanya homework yake vyema kuhusu chanzo cha umaskini wa watanzania.
  7. Ikulu yake kutumia pesa nyingi kwa ukarabati usioonekana.
yapo mengi ndugu yangu nafasi haitoshi

Sidhani kama mzee madrassa al sul atajibu hili
 
naomba utapatie data zilizokuwa kwenye ilani ya ccm ili tulinganishe bajeti na uhalisia uliopo,
yaani useme ccm waliahidi kujenga zahanati 20 ila wamejenga 50, pia utupatie na gharama halisi iliyotumika
kujenga zahanati hizo na utueleze ni kiasi gani cha pesa tanzania inapoteza kwa ufisadi, hapo tutatoa
uchambuzi makini.....

Ziko mtandaoni
 
Tuma ujumbe huu kwa watu 50 thanks

 
Last edited by a moderator:
TandaleOne,


  1. Kujenga Zahanati bila kujua kuwa watu wamezitumia hizo zahanati haiwanufaishi watanzania
  2. Kuongeza idadi ya vituo vya afya bila kuwa na takwimu watu wangapi wamepata huduma bora za afya haisaidii
  3. Idadi ya madaktari walioondezeka inahusu wale waliofanya kazi nchini au ni waliosajiliwa bila kujali wameenda kufanya kazi wapi?
  4. Matokeo ya idadi ya wauguzi kuongezeka ni nini?
  5. Baada ya kugwa vyandarua malaria morbidity imepungua kiasi gani? maana niliona watu wanatumia vyandarua kuvua samaki?
  6. Ongezeko la machine za ulizozitaja zimesababisha wagonjwa wangapi wkapata huduma bora za afya? na maisha kiasi gani yameokolewa kutokana na mashine hizo?
  7. HUKO KWETU WAZEE HUJISIFIA IDADI YA NG'OMBE HUKU WAKIENDELEA KUISHI MAISHA YA KIMASIKINI.NG'OMBE HALIWI MPAKA AFE NA HAUZAWI MPAKA KUWE NA KESI LAKINI HAWEZI UZWA KWA SHUGHULI ZA MAENDELEO.
  8. Tueleze outcomes ya hayo uliyoyasema ili utuondoe shaka la sivyo tutajua unahitaji msaada wa haraka.
 
Back
Top Bottom