Fanya kazi kama mtumwa ili baadae uishi kama mfalme.Maisha si rahisi wandugu wapendwa,ujasiriamali huu unaozungumzwa kiwepesi hapa utapotosha watu,kujiajiri ni kazi kama kuajiriwa tena pengine ni ngumu kuliko kuajiriwa ila ujasiriamali haukwepi,lazima ufanyike maana ajira zenyewe sio guarantee,hukawii kupigwa chini.
Ndugu usiache kazi kabla biashara yako haijasimama otherwise utajuta.Wewe ni kijana na huu ndio wakati wako wa kujijenga so you must work harder to make it,hapa namaanisha kwamba lazima ubaki na ajira yako huku ukiwa na mradi wako pembeni,mradi ukishasimama ukazalisha hapo ndio unaweza kuacha kazi.Fanya savings,jinyime ili upate mtaji na jitume ktk kusimamia hiyo biashara