Natamani hata kunywa sumu, mapenzi jamani...

Natamani hata kunywa sumu, mapenzi jamani...

Mshukuru Mungu huyo jamaa hujaandikiwa, kwani inaonekana hata kama mngeoana lazima ndoa yenu isingekuwa kama unavyofikiria, achana nae, wewe naamini ni msichana mzuri, asikusumbue yeye zilipendwa wako au mwanamke wake.

Kuwa jasiri, muombe Mungu atakupa haki yako na utafurahi.

Huhitaji kuhama chumba wala kuona aibu au kufuatilia taarabu zao.

Chapa kazi, kuwa busy na mambo yako naamini atakuja kugundua kuwa kafanya kosa kubwa na inawezekana akakupigia magoti lakini atakuwa amechelewa.

Huhitaji kumpigia simu we anza mstakabnali mpya kabisa.
Hujanyang'anywa uhai hilo ndio kubwa bado unayo maisha yako na fursa nyingi,songa mbele kishujaa.
 
Usinywe sumu mwaya, mwenzako kuna mtu nilikuwaga nimempenda kiasi kwamba nilidhani nikachaachana nae ntakufa, na nkawa najidanganya kuwa nkimkosa yeye siwezi pata mwingine wa kumpenda kama yeye, kitu ambacho si kweli. Mwenzio baada ya kuniacha nkawa ni wa kulia kila kukicha wakati ninayemlilia anaponda raha, siku moja nkamwambia yaani natamani nife kwa ajili ya yeye kuniacha, unajua aliniambiaje? aliniambia nikifa watakaopata hasara ni wazazi na ndugu zangu, na niliona ni kweli. Mwisho wa siku nikampata wakunipenda nikampenda kweli hadi sasa tunadunda bila shida wala karaha.

Hivyo na wewe nakwambia kuwa "UTAKAPO KUNYWA SUMU UKAFA, WATAKAOUMIA NI NDUGU ZAKO NA WAZAZI WAKO WALA SI YEYE" achana naye, mchulie kama hajawahi kuwa mpenzi wako utashangaa mwenyewe utampata aliye sawa na wewe na hutajuta kamwe. Na utashangaa hilo dumejike linaludi kujikosha tena loh!! Raha jipe mwenyewe bana. Kwani umezaliwa naye huyo????

mimi ni msichana wa miaka 26, naishi arusha nilikua na mchuchumba wangu ambae tumedum nae kwa miaka 2 na kupanga mambo mengi ya kuoana wote tumepanga nyumba moja japo kila mmoja anakaa chumbani kwake dec nilisafiri kwenda likizo nyumbani mwanza nimerudi jan 10 nimekuta kaanzisha mahusiano na dada jirani tena tumepanga nae nyumba moja nifanyeje wana JF yaani wanapika na kupakua yule dada ananiwekee nyimbo za mafumbo. taarabu, mpaka nakosa ham ya kuishi nilipomtaka nimuulize mchumba wangu imekuaje maana hatukukosana kabisa hataki kupokea cm yangu ananisalimia tu basi nampenda sana jamani naumia nashindwa niongee na nani anisaidie mimi niende wp jaman haaa kwel dunia haina huruma
 
acha hiz mdada ww mkaushie 2,tatiz n mazoea ulioweka kwamba wakati kama huu unakuanae pamoja ndokinachokuumiza ila baada ya muda utakua fresh2 na mtoe akilini m2 km huyo watu tunatafuta kupendwa yeye anachezea wali kuku wakat mbele kuna njaa kali?mpotezee mdada asikuumize kichwa ukazeeka mapema coz ya mapenz
 
pole sana dada jack 1, ila hiyo ndio dunia ya mapenzi ni jambo la kawaida sana na sio ww wa kwanza kukutokea kitu kama hicho, yamewakuta w2 makubwa zaidi yako.,hapo ni kuhama nyumba hiyo ili ucendelee kuteseka na kuufikiria unyama aliokufanya huyo jamaa , hapo utaweza kumsahau kwa haraka zaidi.,kingine nitakuunganisha na jamaa wangu yeye ni mshauri wa haya mambo anaitwa DISMASS LYASSA nadhani atakusaidia katika ushauri pia,. Msamehe bure na ucchukue hatua za kujihukumu mwenyewe yaani KUJIUWA kwa namna yeyote ile kwani ni DHAMBI kubwa alafu utampa KICHWA huyo MJINGA kwamba kuna m2 alikufa kwa ajili yake, Kama na ww unaweza MLETE MWANAUME hapo ndani ili umuonyeshe kwamba na ww ni NOUMA wala usihangaike kumpigia SIMU hapo utakuwa unazidi kumpa BICHWA,.zingatia haya yangu kisha utakuja kuniambia MATOKEO yake
 
Usijiue binti yangu, Mungu amekuonyesha kuwa huyo sio mtu sahihi kwako haijalshi mmepanga nini bali ni nini mpango wa Mungu ktk mahusiano yenu, kwa hiyo kama ameamua kuwa na mahusiano na mwingine basi wewe mngojee Mungu akupe Mume wako. Mungu ni mwaminifu hadanganyi, hashindwi na ana upendo wa kweli. Pia nakushauri uende kwa kiongozi wako wa kiroho ili akupe ushauri wa kiroho kwa sababu maamuzi unayotaka kufanya ni ya kukumaliza na hiyo ndiyo kazi ya shetani. Mungu akubariki sana.
 
Kwani dada kabla ya kuonana nae ulikuwa unaishije? Mpotezee
 
hakunaga mapenzi yaleeeee ya kugandana ni zama za kale, source, kiba
 
huhitaji kuumia kivile bali mshukuru mungu kwa sana maana amekufunulia jinsi alivyo huyo unaye mwuita mchumba wako huyu si mtu sahihi hata kidogo tulia angalia ustarabu mwingine
 
mimi ni msichana wa miaka 26, naishi arusha nilikua na mchuchumba wangu ambae tumedum nae kwa miaka 2 na kupanga mambo mengi ya kuoana wote tumepanga nyumba moja japo kila mmoja anakaa chumbani kwake dec nilisafiri kwenda likizo nyumbani mwanza nimerudi jan 10 nimekuta kaanzisha mahusiano na dada jirani tena tumepanga nae nyumba moja nifanyeje wana JF yaani wanapika na kupakua yule dada ananiwekee nyimbo za mafumbo. taarabu, mpaka nakosa ham ya kuishi nilipomtaka nimuulize mchumba wangu imekuaje maana hatukukosana kabisa hataki kupokea cm yangu ananisalimia tu basi nampenda sana jamani naumia nashindwa niongee na nani anisaidie mimi niende wp jaman haaa kwel dunia haina huruma

....miaka yote "24" ambayo hukuwa naye, uliishi ishije mpaka leo hii uone maisha hayawezekani bila yeye?
 
603084_588999697794554_1579616267_n.jpg
cheers!
 
kumbe alishakukataaga zamani ikawaje akakupa tena mimba

au huyu ndo yule handsome uliompenda
 
kumbe alishakukataaga zamani ikawaje akakupa tena mimba

au huyu ndo yule handsome uliompenda

Mwache mwenzio bana.
Mbona unamkunbusha machungu ya kutendwa?
Hivi bado tupo naye kimwili kweli au alijirestisha in piis
 
mimi ni msichana wa miaka 26, naishi arusha nilikua na mchuchumba wangu ambae tumedum nae kwa miaka 2 na kupanga mambo mengi ya kuoana wote tumepanga nyumba moja japo kila mmoja anakaa chumbani kwake dec nilisafiri kwenda likizo nyumbani mwanza nimerudi jan 10 nimekuta kaanzisha mahusiano na dada jirani tena tumepanga nae nyumba moja nifanyeje wana JF yaani wanapika na kupakua yule dada ananiwekee nyimbo za mafumbo. taarabu, mpaka nakosa ham ya kuishi nilipomtaka nimuulize mchumba wangu imekuaje maana hatukukosana kabisa hataki kupokea cm yangu ananisalimia tu basi nampenda sana jamani naumia nashindwa niongee na nani anisaidie mimi niende wp jaman haaa kwel dunia haina huruma

Mrudie mungu vinginevyo niungishe nikuupe sumu
 
Mwache mwenzio bana.
Mbona unamkunbusha machungu ya kutendwa?
Hivi bado tupo naye kimwili kweli au alijirestisha in piis

huyu anazingua

na si vyema kabisa kutishia watu wazima kumbe hamna lolote

hii home of great thinker ukijifanya kanjanja watu wehu vilevile
 
Na we tafuta bwana uwe unapika nae hapo! Umlili jamaa tu yake ina tv au!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom