Nataka niachane na Wanawake nisifanye mapenzi tena

Nebuchadneza

JF-Expert Member
Oct 6, 2023
415
1,032
Habari ndugu zangu.

Mimi ni mwanaume rijali kabisa, sina shida yeyote nina watoto wawili, sasa baada ya kujithamini kwa muda mrefu nimedhamiria kutoka moyoni kutojihusisha na wanawake tena.

Yaani ni stop kufanya mapenzi, niwe mtu wa mazoezi yaani nifanye mazoezi kufa na kupona, nitoe sumu zote mwilini, nirekebisha magoti yangu maana nimekuwa mtu wa kufanya mapenzi ovyo.

Pia vyakula nitakavyokula visiwe vya mafuta na chumvi ya viwandanai, nile matunda fresh na maji ya kutosha, nna hakika nitarudi kama zamani nilipokuwa na miaka 15.

Unajua baada ya kutoa shahawa zako kipururu nafsi yako inakuwa na huzuni na kuwaza kujifikiria ya nini sasa umefanya mapenzi, ghafla unakuwa mpole, yote haya yanatokana kwa tamaa za kipuuzi.

Sasa nataka niwe mtu wa mazoezi, yawe ndo mwanamke wangu. Sex sex ina raha pale unapotoa shahawa lakini baada ya hapo ni majuto tu.

Basi nakaribisha mawazo yenu kunisaidia mimi kijana wenu.
 
Back
Top Bottom