Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,143
Nina ndoto ya kuwa mwanasiasa. Nataka kushiriki,kama kiongozi wa kisiasa,katika kuiongoza na kuijenga nchi yangu-Tanzania. Nina ndoto ya kuwa mwanasiasa mahiri. Nataka kujiunga na wanasiasa vijana waadilifu na wenye uchungu wa kweli wa ukombozi wa kifikra na kiuchumi wa watanzania.Ni mzaliwa wa Wilaya ya Kibaha,Mkoa wa Pwani ingawa ni mngoni. Tanzania yetu inaruhusu kuchanganyika kama hivi.
Sasa nina miaka thelathini.Ni msomi wa sheria kwa Shahada ya kwanza niliyohitimu mwaka 2009 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Nikiwa shuleni na Chuo Kikuu na hata Taasisi ya Mafunzo ya Sheria kwa Vitendo,almaarufu kama Law School of Tanzania,nimewahi kuwa kiongozi wa ngazi mbalimbali.Nilianzia umonita hadi Urais.CV yangu ikihitajika nitaiweka hapa
Wajuzi wa siasa za nchi hii niongozeni.Nifanyaje? Chama gani cha kisiasa kitanifaa? Kwanini? Nisaidieni wakuu
Sasa nina miaka thelathini.Ni msomi wa sheria kwa Shahada ya kwanza niliyohitimu mwaka 2009 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Nikiwa shuleni na Chuo Kikuu na hata Taasisi ya Mafunzo ya Sheria kwa Vitendo,almaarufu kama Law School of Tanzania,nimewahi kuwa kiongozi wa ngazi mbalimbali.Nilianzia umonita hadi Urais.CV yangu ikihitajika nitaiweka hapa
Wajuzi wa siasa za nchi hii niongozeni.Nifanyaje? Chama gani cha kisiasa kitanifaa? Kwanini? Nisaidieni wakuu