Mkuu hebu tusaidie kimoja
mimi nikiajiri kampuni ya ujenzi si wanapaswa wao kutafuta hao wataalam wote?
au mimi tena mteja nitafute wataalamu woote hao na bado nitafute kampuni ya ujenzi?
je wewe una kampuni ya ujenzi?
au unafanyaje shughuli zako
suppose nimekuja kwako nataka kujenga ghorofa 5 nina milioni 500 tunaanzia wapi hadi wapi?
Katika fiesibility stage wakati wazo la kutaka kujenga say structure ya aina fulani likija unatakiwa kukaa chini na mtu mshauri mwenye displine ya masuala ya fedha say mchumi ambaye atafanya utafiti usioacha shaka kwamba kiwango cha fedha unachotaka kudump kwenye mradi huo hutakuwa umepotea!
Baada ya mtu huyo naamini kabisa utakuwa una kiwanjaama eneo lililo mbali na mgogoro(kwa kuamini kwamba suala la lease ama title deed utakua umekwisha liweka sawa)
As Archtect utanifata,utanieleza adhma yako, nitatembelea site na kukushauri accordingly kisha kwa kufuata mahitaji yako nakaa chini natengeneza so called preliminary sketch kwa maana ya draft ya kwanza,nitakaa na wewe chini tutaijadili kama kuna ammendments zozote kisha narudi studio kumaliza design!
Baada ya kumaliza design tutam appoint structural Engineer kwa ajili ya ku calculate forces,kuandaa bar bending schedule,kudesign column/beams,slabs,stairs na kama kuna special mechanical item tunamshirikisha specialist.
Baada ya zoezi hili kukamilika file la Architect kwa pamoja na la Engineer linapelekwa kwa Economist(QS) whom ata quatify material na costs. Baada ya hapo unaweza kutangaza tenda ama kumchagua mkandarasi utakayeona anafaa (kwa msaada wa mhandisi mshauri-Consultant)
Note. Wakati documents zote zimekamilika utapeleka manispaa kwenye ofisi za ardhi ili kupewa kibali cha ujenzi Building Permit.
Baada ya Hapo file la Architect na QS utalipeleka kwenye bodi ya AQRB na lile la Engineer utalipeleka ERB ili kila moja upate sticker baada ya mradi kukaguliwa na kusajiliwa.
Mwisho kabisa huyo Contractor/Mjenzi uliyempata kama akiwa na daraja linalomruhusu kwa scale hiyo ya mradi naye anapewa usajili CRB na kupata Sticker. Kutoka hapo mradi unaendelea ila ukiwa unakaguliwa na wataalam kwa kila stage!