Nataka kufyatua tofali inchi 4, inawezekana?

Nataka kufyatua tofali inchi 4, inawezekana?

Wazo la kabwela

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2013
Posts
1,883
Reaction score
1,465
Wataalamu habari???

Nimekaa nikawaza kutokana na ugumu wa pesa na uhitaji nilionao... nataka kujenga ukuta/ uzio wa eneo langu sasa nafikiria badala ya kufyetua tofali ya inchi 5' au 6, basi nifyetua tofali za inchi 4' je? Inawezekana?? Na kitaalamu imekaaje??, kumbuka ni kwa ajili ya uzio tuu ambao ili kuukazia nafikiria kufunga lenta mbili yani katikati na mwisho kabisa kwenye kozi ya 8 au 9 ya ukuta..... naomba ushauri wenu wadau
 
Kuna aina nyingi za uzio, kuna watu wanaweka fence wanapanda mochongoma au maua

Angalia unayomudu kwa sasa
 
Umepiga mahesabu kulinganisha gharama au imekujia tu kichwani ?
Utasave gharama kiasi kama ukitumia matofali ya 4inch ila beams na columns ni idadi ile ile kama ukitumia matofali ya 5inch . Ila kuongezea idadi ya beam kwenye kwenye ukuta wa 4inch sidhani kama utasave gharama kama unavyofikiri. Kuwa na uhakika utasave kiasi gani ndio utafute ushauri wa kitalaamu.
 
Weka ratio kubwa ya cement of which unaweza kurudi kule kule
 
Ama uache space kati ya tofali itakuwa nafuu zaidi
 
Nionavyo tofali za inch 4 zinafaa kwa kuta za ndani ya jengo ambazo hazibebi mzigo zaidi ya uzito wake zenyewe.

Kwa ukuta wa uzio/fence sio mwafaka sana - kwa vile ukuta wa fence unaweza kukutana na shuruba kubwa mfano majambazi, kuangukiwa miti, vimbunga nk
 
Back
Top Bottom