Nataka kufungua shule ya sekondari

Nataka kufungua shule ya sekondari

malembeka18

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2018
Posts
3,717
Reaction score
4,295
Wadau nipeni ushauri kwenye sector ya elimu, nataka kufungua sekondari vipi biashara katika sector ya elimu hasa sekondari Ikoje.

Taratibu zipi zakufuata kufungua sekondari na vigezo Gani vyakuzingatia kudumu kwenye biashara na kupata watoto.
 
Wadau nipeni ushauri kwenye sector ya elimu,nataka kufungua secondary vip biashara katika sector ya elimu hasa secondary Ikoje,
taratibu zipi zakufuata kufungua secondary na vigezo Gani vyakuzingatia kudumu kwenye biashara na kupata watoto
Mkuu tupo wote...mi eneo nishaandaa kabisa ila sijapata consultant...mi nilitaka nianze na ya Advanced tu Mbeya huko...plot ipo tena eneo zuri ila sijapata assurance bado uncertainties zinanitisha huku kichwani mpaka nipate comfort ya consultant au mzoefu wa hii biashara maana ni biashara kama katoto kachanga kama ilivyo biashara ya media
 
Wadau nipeni ushauri kwenye sector ya elimu,nataka kufungua secondary vip biashara katika sector ya elimu hasa secondary Ikoje,
taratibu zipi zakufuata kufungua secondary na vigezo Gani vyakuzingatia kudumu kwenye biashara na kupata watoto
Taratibu za kuzingatia:
Ukikata kuanzisha shule, nenda ofisi ya afisa elimu sekondari utapata mwongozo sahihi wa kuzingatia ila baadhi tu kwa uchache ni uwepo wa madarasa yasiyopungua manne, maabara zilizokamiliza zenye vifaa zisizopungua tatu, jengo la utawala na viwanja vya michezo.
Usipokidhi vigezo hivyo kupata usajili wa shule ni utata:

Changamoto:
Kikubwa uwe na uwezo wa kusimamia vema shule yako kama zifanyavyo shule za RC na uajiri walimu mahiri wenye kuleta matokeo bora, vinginevyo kama huna uhakika wa kufikia vigezo hivyo, heri uwekeze hela yako kwenye sector nyingine.

Pia biashara ya shule binafsi kwa sasa imeathiriwa na ukata mifukoni mwa wananchi na ukosefu wa future Kwa wasomi waliozaliwa familia zenye uchumi duni hali iliyopelekea mwamko wa wazazi wengi kuacha kupeleka watoto wao shule binafsi.

Maoni:
Bora kuanzisha chuo cha kati kinachotoa fani na taaluma ngazi ya cheti hadi stashahada kuliko kuanzisha shule ya sekondari.
 
Back
Top Bottom