Fahamu mambo mbalimbali kuhusu Kilimo cha Korosho

Lumumba
Shukran sana mkuu, nilibahatika kupata shamba Masasi na kwa sasa lipo kwenye maandalizi nitaomba ushauri wako kipindi cha kupanda mbegu mwezi November,
 
Nina shamba langu la hekari 50. Lipo Rufiji. Nataka kulima Korosho. Naomba nisaidiwe namna ya kupata mbegu bora na jinsi nitakavyozipata. Nimebahatika katika mtandao kupata mwongozo toka Bodi ya Korosho. Taarifa nilizoziona ndani yake ni pamoja na kwamba mbegu bora zinapatikana Naliendele.

Pamoja na ombi la awali, pia naomba kwa yeyote mwenye mawasiliano na watendaji wa kituo cha utafiti Naliendele anipatie contacts ama kama mtu anayemfahamu mkulima wa Korosho anayetayarisha mbegu bora, anisaidie mawasiliano mawasiliano ya mhusika nawasiliane kwa ajili ya kupata mbegu hizo.

Ni imani yangu wadau wapenda maendeleo mtanipatia msaada huo. Asanteni. Nasubiri kwa hamu kubwa kuwezeshwa niingie kazini.
 
Nakushuru sana kwa namba ya simu uliyotoa, lakini kila ninapopiga iko busy. Nimetuma ujumbe nao bado haujajibiwa.

Members, bado ninauhitaji sana wa mbegu hizo na abc za upandaji au ulimaji wa Korosho kama nilivyoeleza awali. Bado tumaini langu la kusaidiwa katika jukwaa hili ni kubwa.

Asante.
 
Wasiliana nasi sasa kwa mahitaji ya miche bora ya korosho kwa shilingi 1000 tu.

WhatsApp/call/text
0766006128
0655715184
0683433440
Ofisi zipo kilombero &kibaha (opening soon).
Vile vile tuna miche mbali mbali ya mbao kwa shilingi 400 tu
 
Wasiliana nasi sasa kwa mahitaji ya miche bora ya korosho kwa shilingi 1000 tu.

WhatsApp/call/text
0766006128
0655715184
0683433440
Ofisi zipo kilombero &kibaha (opening soon).
Vile vile tuna miche mbali mbali ya mbao kwa shilingi 400 tu

Habari
Kiongozi hv kwenye shamba la heka moja inaingia miche mingapi ya korosho?
 
Mbegu za mikorosho zinatolewa bure haziuzwi, kama uko Rufiji nenda ofisi za wizara ya kilimo watakuelekeza mahali vitalu vya miche vilipo hapo Rufiji.
 
Mwaka huu Miche ya mikorosho haitolewi bure. Kama una shida ya Miche Na utaalamu wa jinsi ya kuhudumia Shamba LA mikorosho contact 0784474935
 
Nimefurahishwa na uzi huu. Bahati mbaya nimeingia wakati umeshaenda sana lakini natumaini mchango wangu unaweza kusaidia. Mimi ni mmoja wapo wa watu waliohamua kuingia kwenye hiki kilimo cha Korosho.

Ni mmoja wapo wa walipata ardhi Manispaa ya Lindi na kupambana na kusafisha misitu. Mpka sasa hivi bado tuko site tunapambana maana kazi ya kusafisha misitu si kazi lelemama.

Huko tunaambiwa na wataalamu kuwa tupande kwa upana wa 12m x 12m, hivyo tunaweka miche 25 kwa ekari. Miche wanatoa bure.

Naweza kukubaliana na Lumumba nadhani ni kweli tunapoteza ardhi kwa kupanda miche 25 kwa ekari lkn ni ngumu kutofuata masharti ya wataalamu na Board ya Korosho wanaotoa miche.

Nadhani wazo la kupanda mingi alafu ukapunguza ikianza kushikana ni wazo zuri kabisa. Ntajaribu kuwauliza wataalamu na kuleta mrejesho.

Kagalala - Uliweza kupata mrejesho juu ya hili suala - kama wataalamu wa bodi ya korosho wanaridhia kupanda miche 120 kwa ekari (kwa upana wa mita 5-6 x 6-7)? Nauliza kujua kama ukiomba miche yao (ile wanayogawa bure) kama watakubali kukupa miche zaidi ya kipimo chao cha 25 kwa ekari.
 
Kagalala - Uliweza kupata mrejesho juu ya hili suala - kama wataalamu wa bodi ya korosho wanaridhia kupanda miche 120 kwa ekari (kwa upana wa mita 5-6 x 6-7)? Nauliza kujua kama ukiomba miche yao (ile wanayogawa bure) kama watakubali kukupa miche zaidi ya kipimo chao cha 25 kwa ekari

Kwanza hakuna miche ya bure this year hiyo ilikuwa ni programme ya 2017/2018. Sina hakika na idadi ya miche unayoweza pewa kwa ekari ila wanasisitiza miche 28 tu kwa ekari!
 
Katika pitapita zangu kwenye kata mbalimbali zilizopo Lindi, aise nimejifunza kuwa watu wengi waliochukua miche ya korosho msimu huu hakika wamekwenda kuipanda katika mashamba niseme machafu au ambayo hayakuandaliwa vizuri!

Nadhani kuna haja ya elimu ya kutosha itolewe kwa wakulima juu ya maandalizi ya shamba hatua kwa hatua mpaka mche wa mkorosho unapopandwa!

Mengi ya mashamba hayo yanamilikiwa na watu waliopo mijini ambao wameweka vijana au mwanakijiji msimamizi ambae anatoa taarifa ya maendeleo ya shamba kupitia simu au picha za watsup!

Ndugu zangu ambao mna interest ya kuwekeza katika kilimo hiki napenda niwakumbushe kuwa kazi ya kilimo hata siku moja haijawai kufanywa au kusimamiwa kwa simu.

Wengi wetu tumeweka mategemeo makubwa sana tukiwa na calculator zetu mezani tuki reffer ile bei ya 3970 kwa kilo times namba ya kilo kwa mkorosho mmoja times idadi ya ekari ulizoambiwa na “mfanyakazi/msimamizi” wako kule Lindi kuwa zimepandwa msimu huu.

Changamoto ni kubwa na kinachoendelea Lindi na maeneo mengine katu hayataweza kututoa hapa tulipo kama juhudi binafsi katika kusimamia uwekezaji huu hazitachukiwa!

Naomba magwiji wa kilimo hiki ambao wamejaa tele katika jukwaa hili watufundishe hatua mbali mbali za maandalizi ili kuokoa jahazi ambalo kwa mtazamo wangu tayari limeshageuzwa lilikotoka na linakaribia kuzama!!

“”NIISHIE HAPO KWA SASA””
Hapa

Sie wa mbali hautushauri kulima huko korosho? Najiona nimekuwa so interested lkn mamangu kanikatisha tamaa kuwa inahitaji close supervision, na wakati wa mavuno korosho hudondoka hivyo ni rahisi kuibiwa. Nimekatishwa tamaa lkn bado roho haitaki kuacha Jambo hili, nawe umesisitiza hapa.
 
Hapa

Sie wa mbali hautushauri kulima huko korosho? Najiona nimekuwa so interested lkn mamangu kanikatisha tamaa kuwa inahitaji close supervision, na wakati wa mavuno korosho hudondoka hivyo ni rahisi kuibiwa, nimekatishwa tamaa lkn bado roho haitaki kuacha Jambo hili, nawe umesisitiza hapa.

Ni kweli! Ushauri wa mama yetu upo sahihi kabisa! Uwekezaji wowote unahitaji usimamizi (supervision) ya hali ya juu! Kumbuka kuwekeza ni jambo moja na kusimamia uwekezaji wako ili kufikia malengo uliyojiwekea ni jambo jingine!

Kuhusu kuibiwa wakati wa mavuno hiyo ni kweli ila inategemea na nguvu kazi uliyojiwekea katika hicho kipindi cha miezi miwili ya mavuno ili kuhakikisha hakuna upotevu mkubwa kwa njia hiyo!

Bado nakusisitiza amka na ifuate NDOTO yako!
All the best!
 
Very very educative thread! Tunahitaji mijadala ya namna hii siyo mijadala ya porojo porojo tu ambazo hazitusaidii chochote! big up wadau wote wa hii thread!
 
HABARI,
"Mandison,
Gharama za kuanzisha kilimo cha koroso sio kubwa sana haizidi laki moja kwa heka,Korosho ni zao linalokubali katika mikoa mingi hapa tanzania ukiacha mikoa yenye umaarufu, MTWARA, LINDI, PWANI, TANGA, iko mikoa mipya.

KamaTABORA,SINGIDA,DODOMA,SOGWE,RUKWA huko kote zao la korosho linastawi vizuri fanya mawasilianano na kituo cha utafiti wa kilimo cha naliendele. Watakupa maelekezo mengi sana nadhani maswali yako yote utapata majibu pale.
Naliendele Agricultural Research Institute (NARI)


Contact
Zonal Director (South),
Naliendele Agricultural Research Institute (NARI),
10 Newala Road, P. O. Box 509, Mtwara.
Tel.: +255 732 934 035
Fax.: +255 732 934 103
e-mail: utafiti@iwayafrica.com

LUMUMBA
Habari Lumumba
Binafsi nimeanza kupanda korosho lakini mbegu zilizotumika sio miche bali ni korosho zenyewe, je kuna athari yoyote mkuu?
Shamba langu lipo wilaya ya Masasi , mbuyuni kitongoji cha Mitonji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kuwa unataka kuanza kupanda habari ya madawa sitakueleza.Tafuta shamba maeneo ya kusini mwa Tanzania(lindi ,mtwara,tunduru).Miche tunapanda kipindi cha mvua ambapO halmashauri husika wanagawa niche kupitia serikali za vijiji.Kumbuka mbegu wanayotoa ni ya miaka mitatu,ila mavuno yanaongezeka kadri ya umri wa mti unavyoongezeka.Uzoefu unaonyesha kuwa mashamba mengi yanamilikiwa na Wazee,hivyo kuna umuhimu wa vijana kuanza kupanda miti mipya kwenye maeneo mapya ili kutransfer uchumi uje kwetu.Kwa wale wanaonunua mashamba yenye miti iliyozeeka wanachofanya no kupanda niche mipya na kukata ya zamani pale mipya inapoanzaa kuzalisha.
Asante kwa taarifa Je, mkuu msimu wa kupanda ni miezi ipi ambayo kuna mvua. Nahitaji kujua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom