Nataka kuagiza VW Touareg V6

Nataka kuagiza VW Touareg V6

ujiandae kisaikolojia kuna kushinda garage kila weekend wenzako wakiwa wanaenda site wewe ni mwendo wa garage
 
Wakuu, nataka kuagizia sasa gari ya ndoto yangu, gari inayokonga mtima wangu si ingine bali ni VolksWagen Touareg V6.
Hii gari kila nikiiona road naweweseka jinsi ilivyo body yake kubwa na muonekano wa kiume/kibabe.

Hii ni SUV yenye cockpit moja matata sana na ya kipekee.
Budget yangu ni M 35, sasa naomba kupata hints kwa mjuzi ambaye alishawahi kumiliki au kuwa close na mtu mwenye hili dungu.
Mad Max RRONDO Hamritzer
View attachment 3284747View attachment 3284748View attachment 3284749
Nunua kitu roho inapemda!
 
VolKswagen touareg ina matoleo matatu.

2002 mpaka 2010 toleo la kwanza.
2010 -2018 toleo la pili.
2018 mpaka sasa toleo la tatu.

Magari haya ni mazuri na very comfortable kwa speed na perfomance yake ya hali ya juu.

Kama zilivyo gari nyingine zilivyo na changamoto pia VW ina changamoto zake kama mfuko wa umeme, gear box na utumiaji wa mafuta mkubwa V6.
Muhimu ujue fundi mzuri sio unapeleka kwa kila fundi. Pia epuka kupeleka kwa mafundi bila kufanya diagnosis.

Kwa hela yako hapo utapata generation ya kwanza ila ukikaza utapata generation ya pili.

Ila mwisho wa siku tambua magari haya brand za ulaya ya value yake ina depreciate kwa kasi sana. Ukinunua milioni 35 baada ya miaka mitatu utauza milioni 18.
 
Hiyo gari ukifanya kitu cha kijinga inakutukana huwa inakuuliza mpaka.maswali are you crazy,kuna jamaa ilimuuliza hivyo akabonyeza yes hapohapo ikajipigq lock
Bwana mkubwa hahahaha kama unatupiga fix kunogesha hii gari poa tu hahaha
 
Chukua VeWe T hiyo mzee. Hutajuta hiyo gari, watakuja watu wajatumia hiyo gari kukuzuzua hapa, nakwambia hawajatumia hiyo gari, alietumia hiyo gari, mwenye roho safi hatakushauri vinginevyo mkuu.

VeWe kuna magari walidesa ila sio Tuuer.
Natumia hii gari mwaka wa nne sasa, nilimvua mtu Rusumo Border pale. Sijutii hii gari kwa standard, durability, flexibility, comfortability (pure leather yoga seat), driving confidence, powerful v6 diesel engine, off-road capabilities (vumbi, tope, changarawe), performance and Speed. Torque ya kibabe and fuel efficiency, gari ya "mjeremani" hiyo inanusa diesel mzee.
Chimbo ya vipuri "genuine" ya hii gari ni kwa Kagame tuu hapo, ukiwa Rusumo, Nyakanazi au Benako wanakuletea mkononi toka Kisabo, Kigali.

Nyongeza: Rwanda wanazo LHD, vijana wa kinyarwanda wakipata hela wana option ya Porsche Cayenne na Tuuer.
Kwa hizi gari za ulaya kama ina umri wa zaidi ya miaka 5 haifai. Kila siku utaenda gereji
 
Hizi gari ukinunua Brand New, umelamba Dume. Ila used ni tatizo kubwa sana.
Spares parts ni very expensive!
Ukiwa na fedha za kutosha kuzinunua, unakutana na issue nyingine mbili kubwa
1. Pesa ya kuzinunua unazo ila spares parts hujui ununue wapi
2. Ukizipata spares parts mafundi ni shida kubwa,hawapo,waliopo hawayajui hayo magari ya Germany.
3. Ukipata breakdown njiani,utalala hapo hapo.
Tuishi humu📌
 
Pesa ya kununua Brand New tunatoa wapi mkuu sisi watumishi wa kima cha chini?
vp mwana jamii forums ulifanikiwa kupata VolksWagen gari ya ndoto yako? nicheki inbox nikupe contacts za showroom unayoweza kupata Touareg na ndugu zake Tiguan kwa budget uliyokadiria au inaongezeka kidogo tu
 
Mkuu ulishawahi kuagiza gari UK ukapata hii experience? Nimeuliza tuu si kwa ubaya Kiongozi.
Hapana mkuu
Mimi nipo kariakoo kuna ndugu yangu wa karibu Sana anamiliki discovery 4 aliagiza Toka UK lkn hii gari imemletea shida Sana... baadae alikuja mwarabu mmoja anauza magari akamshauri anunue disco 4 za kutoka Australia..
Masanja huu ni ushuhuda Tu ambao sina uzoefu nao Kwa magari ya UK pia nipo tayari kuelimishwa zaidi ili na Mimi nipate elimu
 
mkuu hii bei ya Total ni bei utakayolipia mpaka bandarini au imekaaje hizi Car price na Total Price tofauti ikoje?
Hiyo bei ni CIFyaani hapa kuanzia usafiri melini ,ukaguzi wa gari pamoja na bei ya gari husika...mziki sasa utakuja kwenye calculator ya TRA, bandarini na BIMA, huku ndiko kuna balaa la kupasuka pesa nyingi
 
Hapana mkuu
Mimi nipo kariakoo kuna ndugu yangu wa karibu Sana anamiliki discovery 4 aliagiza Toka UK lkn hii gari imemletea shida Sana... baadae alikuja mwarabu mmoja anauza magari akamshauri anunue disco 4 za kutoka Australia..
Masanja huu ni ushuhuda Tu ambao sina uzoefu nao Kwa magari ya UK pia nipo tayari kuelimishwa zaidi ili na Mimi nipate elimu
PureView zeiss mkuu nimekupata. Mimi Nina experience ya kununua magari UK. Gari zangu zote nilizowahi kumiliki na ninayoimiliki, nimenunua UK. Sijawahi kupata experience mbaya ya gari kushinda garage au kuwa na kutu. Nadhani pia, inategemea na mwaka na uimara wa gari wakati unanunua.
Imagine Leo Tupo 2025, mtu anapambana kutafuta usafiri wa 2005. Miaka 20. Kiukweli hata kama ni chuma, likely utashinda garage.

Mwisho wa siku kila mtu ana experience yake ya magari, based on the budget.
 
PureView zeiss mkuu nimekupata. Mimi Nina experience ya kununua magari UK. Gari zangu zote nilizowahi kumiliki na ninayoimiliki, nimenunua UK. Sijawahi kupata experience mbaya ya gari kushinda garage au kuwa na kutu. Nadhani pia, inategemea na mwaka na uimara wa gari wakati unanunua.
Imagine Leo Tupo 2025, mtu anapambana kutafuta usafiri wa 2005. Miaka 20. Kiukweli hata kama ni chuma, likely utashinda garage.

Mwisho wa siku kila mtu ana experience yake ya magari, based on the budget.
Shukran Sana mkuu
Najua Sisi wabongo tuna mambo mengi
 
Back
Top Bottom