Nataka kuacha kazi

Nataka kuacha kazi

Maamuzi sahihi kabisa, kwa kweli ukigonga 40 bado unategemea ajira majanga.
 
aisee mnanitamanisha na mimi niache kibarua changu! maaana malengo yanazidi chelewa
 
Ni jambo jema sana kuamua kujiajiri.
Ushauri wangu ni huu, angalia miradi yako unayoitegemea kama imejengwa ktk misingi imara ya kuhimili ushindani wa mitaji ya wengine,kuna miradi mingine inaingiza fedha za chap chap lakini ikipita misuko suko kidogo tu, mradi chali.

Uoga ni dhambi, choma meli tukutane ng`ambo ya ziwa.


Mkuu Malila, mwaka huu nitakutafuta kwenye mambo ya shamba.
 
Si kazi kuacha kazi bali kazi kupata kazi, tunatafuta kazi wewe unaacha kazi,think twice,nyaka mil 500 ndo uache kazi

Hajasema anaacha kazi ili akakae nyumbani kwake bila kazi, nilivyomwelewa mimi ni kwamba, anabadirisha kazi, nijuavyo mimi, kazi anayokwenda kuifanya ni ngumu zaidi na inahitaji kujituma zaidi na tija yake ni kubwa, kazi ya sasa anayofanya, anajituma kwa kiwango cha kumridhisha bosi wake,ni ngumu kwa sababu inamnyima uhuru na tija yake kwake ni ndogo, kibaya zaidi umri unakwenda.

Kwa ufupi ni kwamba, mafanikio ya kazi anayofanya kwa sasa ni mali ya mtu mwingine, yy huambulia bonus. Mafanikio ya kazi anayokwenda kuifanya ni yake yeye kama yeye, na kinyume chake ni sahihi. Kajipima kaona bora akajitume.
 
Unasumbuliwa na woga.
Woga wako ndio umaskini wako.
 
do you have guts? if yes do.............otherwise it is petty talk.
 
Nimelelewa mazingira ya kujiajiri nakaza huko huko. Sema ikitoka opportunity ya UN aisee nitaacha private investment ziendeshwe na ndugu zangu ambao wapo kwenye bizness zetu na kupata exposure kidogo.
Tatizo la private bizness ni kutopata exposure hasa za kusafiri!
 
Ndugu yangu hongera kwanza kwa kufikiria hilo mm nilishaquit zamani nilifanya 4.5yrs na sasa niko pazuri sana. Ushauri wangu ni huu ulipotarget kupata mil300 ni mbali sana na unaweza usifike kirahisi. Ila mm nilitumia formula hii; km naweza zalisha pesa sawa na mshahara net nikiwa bado utumwani basi inanitosha sana kuondoka nikaemploy nguvu zangu zote. So inawezekana tu kaza buti. Halafu ukijiajiri utajua kuwa economy kwani ulichopata leo hutakitumia ovyo kwani hujui kesho kutakuwaje. Walioajiriwa huwa hata wanaoverspend kwani wanajua mshahara unakuja tar zile ishirini naaa... So kaza buti!

Sent from my BlackBerry 9790 using JamiiForums
 
Kaka hilo wazo la msingi. Mimi pia nimespecialize kwenye mipango na miradi ila cha muhimu uangalie nini utakuwa unaingiza kwa siku katika private investment kiasi kwamba turnover yako isiwe chini ya matumiz yako pamoja na familia. Pamoja na wazo hilo mimi nakushaur uliendeleze zaid kwan ajira huru inakufanya uamue how much to produce in relation to market tofaut na kaz ya kuajiriwa ambayo mshahara unakuwa constant for long time and no room to add more. Kama vip tutaftane kaka
 
Wasalam wapendwa

Si kwamba nimechanganyikiwa, hapana. Naona kama nachelewa kutimiza malengo yangu na kazi niliyo nayo ni ya kuajiriwa na ofisi zake ni vijijini. Kwa miaka 10 nimekekuwa nikisafiri kutoka ninakoishi (naishi moja ya jiji hapa nchini) kwenda ofisini. Zifuatazo ni hasara na changamoto ninazoziona kwenye ajira hii

1 Nina shughuli zangu mbadala (miradi) huko jijini, kila wiki 1 au 2 lazima nione maendeleo yake, hii hunigharimu sana kifedha kiasi cha Tshs 80,000 hadi 100,000 kwa mwezi.

2 kipato changu kinachotokana na ajira si kikubwa sana ukilinganisha na shughuli binafsi nilizonazo

3. Shugughuli za ofisi zina nature ya kumlazimisha mwajiriwa kufanya kazi mchana, usiku hadi weekend (sometimes) bila overtime au incentives in turn

4 Sipendi kuhamishia familia huko kazini kwangu maana nitaongeza gharama za maisha na kupoteza dira na malengo yangu

5 Sioni kama ajira rasmi itanipa kipato thabiti kabla ya umri wangu wa uzeeni

6 Nataka kutumia Elimu yangu ya " shahada ya udhamili ya usimamizi wa miradi" kuendeleza miradi yangu binafsi

7 Naona kama utumwa fulani kuwa mwajiriwa, hii inanifanya au niwe mtoro kazini au ku Underform kazini kwangu

Kwa sasa bado naendelea, ila miradi yangu itakapokuwa na thamani ya 300mil nita resign with good will, na hili nitalifanya ndani ya miezi 18 ijayo kuanzia leo.

Just to share with you friends, you can advise otherwise, maana haya maisha nayo hubadirika, nipe uzoefu na mawazo yako tafadhari...

Mkuu wazo lako ni zuri saana na binafsi nadhani uzip huu ulipaswa kuuweka Jukwaa la ujasiriamali kule ungepata mawazo mazuri saana ya namna ya Kuchoma meli moto. Kwa mtazamo wangu naami sasa ni muda wa kufanya maamuzi hayo kuliko kuendelea kupoteza hiyo elfu 80 au 100,000 ambazo ni pesa ungeweza kuingiza katika miradi na wewe kuweza kuisimamia kwa umakin zaidi.
Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom