Natafuta Shamba


OK! Nashukuru sana Mama Joe, nami ngoja nifanye michakato, Mungu akipenda tutajumuika huko pamoja.
 
samahani huko ekari wanauza sh ngapi na usafiri ni wa uhakika kwenda huko?
 
Usafiri upo unaweza panda basi za Bagamoyo/Msata pale Mwenge wakifika njiapanda ya msata nadhani ni kijiji cha kwanza kushoto. Au unaweza panda hiace Mbezi mwisho stand mpya za msata kabla ya kufika njiapanda unashukia Mazizi sijaipitia hii njia ila ipo. Kutoka Mwenge hadi kijijini kilometa 140. Bei laki 2.5-3. Karibu
samahani huko ekari wanauza sh ngapi na usafiri ni wa uhakika kwenda huko?
 

Mama joe nami naweza pata kashamba huko?
 
Utapata natokea huko saahizi. Watu wameshika zaidi barabarani na hasa hii mpya ya msata, huku kwenye kona kuelekea Morogoro hawakujua sana. Karibu

Bei nzuri mananasi vp yanakubali?
 
Kwakweli mimi nilitaka zaidi maji na mitiki. Mananasi kwavile yanakubali sana kata ya Kiwangwa hata hapa nadhani yatakubali. Nitaulizia tena kwa wenyeji kwani huku watu wa nje wachache wamelima mitiki na wana ng'ombe wenyeji nnavyoelewa wanalima mahindi tu sio nanasi
Bei nzuri mananasi vp yanakubali?
 

Mambo vp Mkuu upo?
 
Msata,ipi.
Je ni Kihangaiko, au Madesa, au hii njia ya kuja Bagamoyo? Mimi niko Madesa kuelekea Mkoko. Siku twende pamoja dada.

Mkuu yaani mimi nimepata shamba eneo la mkoko huko msata, heka 20 (si haba). Tena wiki jana nimetoka kuangalia ujenzi wa kibanda. Umeme bado, nitaanza na solar kama Jirani yangu mmoja huko shambani.
Pia kuna mtu mwingine jirani huko shamba ameshaanza kilimo cha nanasi.
Nafuatilia sana post zako, Asante kwa elimu nzuri kwenye jukwaa hili.
 

wanauzaje huko?
 

Mananasi yanachagua sana.

Kiwangwa yenyewe sio yote inaota mananasi
 
Karibu mkuu wanaanzia laki 2.5 hadi laki 3. Maji yaliyopo ni bomba ingawa sijalifatilia bado, mie nimeona migomba, mitiki, mahindi na wansema matikiti ila kiukweli hapa ni mapori eneo kubwa hakuna anaelima. Wachache wanavishamba vidogo vya mahindi ingawa udongo ni mzuri uko tifu kwa hiyo kwa maji ya bomba au kisima waweza lima chochote. Kwa mvua za msimu mahindi yanakubali na tikiti inapoishia mvua
 
Mkuu Mama Joe hapo kwenye laki 2.5-3 unamaanisha nn?
 
samahani huko ekari wanauza sh ngapi na usafiri ni wa uhakika kwenda huko?
Kuhusu usafiri hauna haja ya kupitia Bagamoyo kwa sababu itakulazimu ulipe nauli kubwa na hata unaweza ukaunga mabasi...Kama uko Dar nenda Ubungo pale stand ya vidala dala kwenye njia ya kutokea kule yanakosimama magari ya msasani na mwananyamala pembeni yake utayaona magari ya UBUNGO/MBEZI-MSATA yanapakia..Nauli ni sh 4500/- mpaka hapo Mazizi
 
Sorry namaanisha eka moja inauzwa kwa laki mbili na nusu hadi laki laki tatu kutegemea na umbali na shamba pia

Inamaana nikiingia ndani zaidi naweza kupata kwa bei nafuu zaidi?

Hapo ulipo wewe umbali gani kutoka barabara kubwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…