Likasu
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 857
- 441
Acha unyanyasaji wa wanawake
sio unyanyasaji huo. Kuliwahi kuwa na post "Natafuta mwanaume wa kuzaa nae" mbona hamkusema ni unyanyasaji kwa wanaume ?
Acha unyanyasaji wa wanawake
Tangu nikiwa na umri wa miaka 25 nilitamani kuwa na mwenza lakini kwa bahati mbaya sijajaliwa kumpata ambaye naona tunaweza kuanzisha familia pamoja. Naomba nieleweke kuwa I'm not so selective au sio kila mwanamke hafai au sio mwaminifu katika mahusiano ila mimi kwa bahati mbaya sijajaliwa kumpata wa ubavu wangu, kwani kila nimpataye tunakosa chemistry kabisa huku naona uzee unazidi kupiga hodi. Wakati nasubiri kujaaliwa kupata mchumba nimeamua kutafuta mwanamke nitakayepata nae mtoto tu (kuzaa naye) ili kwa pamoja tuwe na mtoto wetu.
Nina umri wa miaka 32, urefu 180cm na uzito 84kg. Mweusi, nimeajiriwa, kipato cha wastani, nina umbo la wastani na dini yangu ni mkristu. Ninajiheshimu na kuheshimu wengine na tabia ni ya kuridhisha. Ninaishi Arusha maeneo ya Makao mapya. Mwanamke awe mwenye tabia njema ili mtoto aweze kujifunza mazuri kutoka kwa wazazi. Umri wake usiwe zaidi ya miaka 45. Awe anajishughulisha ili asiwe tegemezi kwa asilimia 100 kwani gharama za matunzo ya mtoto tutasaidiana kwa kadiri ya uwezo na tutakavyokubaliana. Awe tayari tukapime afya zetu kabla ya kuanza mchakato pia kupima DNA baada ya mtoto kuzaliwa. Sibagui dini, rangi, elimu, umbile wala kabila.
Kwa mwanamke mwenye hitaji kama langu ambaye yupo serious aniandikie email john.joseph843@gmail.com
You are warmly welcome.
Nilkubali kuwa mke kabisa, maana nilihisi kungekuwa na chemisrty. Lakini bada ya kuona hilo jina la John, moyo ukatumbukila nyongo. Kina John...
Kwasababu bado unaendelea kutafuta wa kumuoa usiwe na Haraka ya kuzaa nje ya ndoa, malezi ya watoto wa nje ya ndoa ndani ya ndoa ni magumu sana, Ni wachache wanaweza kulea ki ukweli ukweli, Kama unataka mtoto Haraka tafuta mke haraka, Na kuhusu Chemistry wewe angalia weakness zako, tafuta mwanamke ambaye ataweza kuziba nyufa ulizozonazo.
Mfano, kama wewe mkali tafuta mke mtaratibu, kama wewe una hasira sana, tafuta mke mwenye uvumilivu, Hivyo jipekue wewe kwanza, Halafu uangalia aina ya mke unayemuhitaji, Watoto wanahitaji malezi na wewe unahitaji malezi! Hutawezaje kulea mtoto bila mama yake?