Natafuta mke mwenye VVU

Natafuta mke mwenye VVU

Acha uongo wewe DAWA unayo kivipi?..Ukimwi hauna dawa acha kudanganya watu wewe utakuwa unatibu secondary infections tu kama T.B, Kuharisha n.k na yule kilaza aliyesema kufa mwenyewe kakosea sana naomba huko aliko ateme mate chini..Mungu amsamehe bure!
Pole sana, hayo ni majaribu tu, je mkeo alipima akakutwa -ve?, ni-PM dawa ninayo.
 
Nimefurahishwa na mwenendo wa michango ya wadau katik hii thread wameonekana kukerwa na PERRY aliyetoa jibu la dhihaka katik ishu sensitive kama ya mtoa mada.

Kimsingi katika jamii hii hakuna ambaye hajaguswa na athari za HIV/AIDS, anaweza kuwa ama mwenza, mtoto, mzazi,ndugu, jirani au jamaa umempoteza au ana maambukizi au anaugua.

Na si kila anayepata eti ni mzinzi SI kWELI na saiv thanks to ARVs watu wanaathirika bt wanatumia dawa na kuishi miaka mingi had wanalea na kusomesha watoto had wanajitegemea.

Mama wa rafiki yangu mume wake alifariki miaka 13 iliyopota lakini mama aliendelea kutumia dawa na sasa watoto waliokuwa wadogo sasa hiv wako vyuo vikuu na bado yuko kazini akiendelea kuwahudumia. So plz huna sababu ya kumnyanyapa muathirika eti kw sababu tu ni muathirika.
 
Acha uongo wewe DAWA unayo kivipi?..Ukimwi hauna dawa acha kudanganya watu wewe utakuwa unatibu secondary infections tu kama T.B, Kuharisha n.k na yule kilaza aliyesema kufa mwenyewe kakosea sana naomba huko aliko ateme mate chini..Mungu amsamehe bure!

Ukimwi hauna dawa kwako wewe kwani ndivyo ulivyofundishwa na kuaminishwa. Hakuna kisicho na dawa isipokuwa kifo, hata ukoma ulikuwa hauna dawa hivyo hivyo.
 
Ila kwa ushauri, tulia katika sehemu yako ya dini utapata pumziko tu. Maana yake mueleze Mungu wako anaona, anajibu. Njia hii itakuchanganya zaidi kaka.
Atakuja huyu akitoka huyu atatokea mwingine.mwisjo wa yote jibu sahihi utalikosa.
Muumba wako anakujua, na anakuona.
 
Naungana na aliyekupa namba za simu ili uegemee kwa Mungu, achana kabisa na PM uliyotaja. Badala ya neno 'PM', weka Mungu, alafu usubiri uone jibu jema kutoka kwa Mungu.
 
we mdudu umepima? Nawasiwasi na akili yako ndio hawa watoto wa form 4 wanao subiri majibu huku wanakuja kujaza wingi shenzi kabisa

Ni kweli, watoto wamekuwa wengi sana humu JF, ndio maana kunakuwa na comments za ajabu ajabu. Tuwavumilie na tuwasamahe bure badala ya kushindana nao na kuumiza vichwa.
 
bora umejitambua kuwa wewe ni marehemu unayetembea
 
Huyo anaye jiita Perry hiv Kweli anaakili anadhani watu wanayapenda hayo matatizo? Kaka unajiona upo salama kumbe Li mkelako jamaa wanalipiga miti alafu unajiona ipo salama k u m. A. wewe.
 
bora umejitambua kuwa wewe ni marehemu unayetembea

kila m2 ni marehem anayetembea tena waweza tangulia wewe kwa ki2 kidogo sana ukamuacha muathirika wa ukimwi 20+ mbele ni watu wazima wangapi wanaopoteza uhai bila ata kuugua na tena kwa dakika chache na kuwaacha waathirika duniani?
 
Ukimwi hauna dawa kwako wewe kwani ndivyo ulivyofundishwa na kuaminishwa. Hakuna kisicho na dawa isipokuwa kifo, hata ukoma ulikuwa hauna dawa hivyo hivyo.
Aisee we huko hapa sayari ya Duniani au sayari ya mars manake huku Duniani tunajua UKIMWI hauna dawa..!Naic wewe ni yule mzee wa loliondo..
 
Mkuu kwanini usitengeneze na mkeo kwani huyo anakujua vema na anaweza kuchukuliana na wewe. Jaribu kutafakari ni wapi mmeudhiana mpaka akaamua kuondoka na ukiona umekosea basi nenda muombe radhi muendelee na maisha na ikiwa yeye hajaathirika mtaelekezwa namna ya kuishi pamoja. I believe ukiomba msamaha na kujiweka karibu na Mungu huo ugonjwa utaponywa bila shida. Nina wasi wasi na mahusiano mapya ambayo unayatafuta hata hivyo kila la kheri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom