Chillah
JF-Expert Member
- Oct 12, 2016
- 9,332
- 10,613
unafahamu sana mkuu. nishasikia habari pale za huyo mdogo wake na Tiba
mkuu nilikuwa ktk haka kautafiti baada ya kumaliza chuo nikawa sina cha kufanya mtaani... ndipo nkamtafuta rafiki yangu mtaalamu wa geology frm UDSM tukaanza kuzurura dodoma mpka maeneo ya dongo mzee... tukapata story ya huyu dada, na alitaka wazurumu watu wengine maeneo ya madini ili achimbe yeye... bahati mbaya wale walikuwa tayari wana leseni so ikawa ngumu kwa kuwa haiwezekani kutolewa leseni mbili ktk eneo moja....
ila hii sekta kwa wasio ijua unaweza sema watu wanacheza tu ila ina pesa sana... ni kutafuta masoko kwanza pili ndipo utafute mzigo ulipo... sasa sisi tulijikuta tumepata maeneo lakini soko hatuna hapo ndipo tulipo kwama mpaka leo
pia ktk hii sekta kuzurumiana ni jambo la kawaida sana, una takiwa kuwa na roho kidikteta ndipo utakula mema ya nchi