Nasimama na Yanga

Fohadi

JF-Expert Member
Jul 24, 2020
770
2,408
Tunaweza tusikichukulie kwa jicho la tatu ila kitendo kilichofanywa na yanga ni cha kishujaa na manufaa makubwa ya soka letu. Kama hii mechi ingechezwa leo saa 1 usiku basi tayari ndio ingekuwa michezo ya TFF kila siku kucheza na ratiba kwa sababu wangejua kumbe hakuna kitu chochote kinachoharibika.

Ingefikia kipindi ratiba za mechi zingekuwa zinabadilishwa kiholela tu bila sababu za msingi. Mfano, ungekuta siku nyingine mechi ya timu A na timu B inaahirishwa/inasogezwa masaa mbele kwa sababu tu uwanja haujajaa kwa muda huo...au ungekuta siku nyingine watu na timu zipo uwanjani halafu mechi inasogezwa muda mbele ili kupisha tu hotuba au kikao cha watu fulani au labda mechi zingekuwa zinaahirishwa kwa sababu tu kuna dalili mvua itanyesha.

Kiufupi, ingefikia stage mechi zingekuwa zinasogezwa mbele kwa sababu zisizo na mashiko. Lakini leo Yanga wameonesha kuwa uswahili hautakiwi na hawajataka kabisa kulea tabia hii.

Ningewakosoa Yanga endapo tu sababu za kusogeza mechi mbele zingekuwa na mashiko lakini mpaka sasa sababu hazijawekwa wazi. Endapo kama sababu zingekuwa zimewekwa wazi na zina mashiko, hakuna mtu au timu ambayo ingekataa kucheza saa 1. Kutokuwekwa wazi kwa sababu za kusogeza mechi mbele inatufanya sisi tuamini kuwa sababu hazikuwa na mashiko ndio maana zimefichwa...ASANTENI YANGA.
 
Wewe kweli uto, mbona haukugoma mechi ya uto na Azam ilivyosogezwa mbele ndani ya siku ya mchezo kutoka saa 1 jioni kwenda saa 2 na robo usiku? Sema mmepata sababu ya kuepuka kipigo kutoka kwa mnyama Simba.
 
Ni haki yako.... Unaweza kusimama na chochote hata kama ni nguzo ya umeme.

Bahati yenu mmepata kisingizio! Leo ilikuwa mkimbie na kyupi mkononi
 
Wewe ni Shaffi?

Acheni ujinga,mnajua kabisa siasa ilivyo katika kila kitu kinachofanyika nchini.
Aliyeagiza mechi iahirishwe ni serikali.Kwa hiyo unajaribu kusema TFF iigomee serikali?
TFF ina vyombo vya usalama?Uwanja ni wao hadi waigomee serikali?

Najua makanjanja mnatafuta pa kutokea lakini busara wakati mwingine hupunguza migogoro.
Ninachoona hapo tatizo ni ukweli tu haujasemwa na serikali iliyowataka TFF wasogeze muda iseme tu ukweli.
Tunaweza tusikichukulie kwa jicho la tatu ila kitendo kilichofanywa na yanga ni cha kishujaa na manufaa makubwa ya soka letu. Kama hii mechi ingechezwa leo saa 1 usiku basi tayari ndio ingekuwa michezo ya TFF kila siku kucheza na ratiba kwa sababu wangejua kumbe hakuna kitu chochote kinachoharibika.

Ingefikia kipindi ratiba za mechi zingekuwa zinabadilishwa kiholela tu bila sababu za msingi. Mfano, ungekuta siku nyingine mechi ya timu A na timu B inaahirishwa/inasogezwa masaa mbele kwa sababu tu uwanja haujajaa kwa muda huo...au ungekuta siku nyingine watu na timu zipo uwanjani halafu mechi inasogezwa muda mbele ili kupisha tu hotuba au kikao cha watu fulani au labda mechi zingekuwa zinaahirishwa kwa sababu tu kuna dalili mvua itanyesha.

Kiufupi, ingefikia stage mechi zingekuwa zinasogezwa mbele kwa sababu zisizo na mashiko. Lakini leo Yanga wameonesha kuwa uswahili hautakiwi na hawajataka kabisa kulea tabia hii.

Ningewakosoa Yanga endapo tu sababu za kusogeza mechi mbele zingekuwa na mashiko lakini mpaka sasa sababu hazijawekwa wazi. Endapo kama sababu zingekuwa zimewekwa wazi na zina mashiko, hakuna mtu au timu ambayo ingekataa kucheza saa 1. Kutokuwekwa wazi kwa sababu za kusogeza mechi mbele inatufanya sisi tuamini kuwa sababu hazikuwa na mashiko ndio maana zimefichwa...ASANTENI YANGA.
 
Mkuu usiwe shabiki maandazi. Unapoona hili jambo halifai kwa maendeleo ya soka letu unatakiwa kukemea kwa nguvu zote, sio lila jambo unaleta ushabiki wa kipuuzi.
Mechi yenu na Azam mbona ilisogezwa imebaki lisaa moja Kuna tofauti gani na hii
 
Mechi yenu na Azam mbona ilisogezwa imebaki lisaa moja Kuna tofauti gani na hii
Walichofanya TFF ni sahihi sio sahihi? Hiyo game ya Azam taarifa ya kupostpone ilitoka muda gani?
 
Mechi ya Azam ilitolewa taarifa siku tano kabla ya mechi
Tatizo kuna watu wanafatilia soka kwa taarifa za vijiwe vya kahawa na draft kisha hawafanyi utafiti wanazibeba kama zilivyo.
Kwanza ni upumbavu kutolea mfano kuvunjwa kwa kanuni kama kigezo cha kutaka tena kanuni ziendelee kuvunjwa eti kwasababu ni kawaida kuvunja kanuni za soka.
 
Tunaweza tusikichukulie kwa jicho la tatu ila kitendo kilichofanywa na yanga ni cha kishujaa na manufaa makubwa ya soka letu. Kama hii mechi ingechezwa leo saa 1 usiku basi tayari ndio ingekuwa michezo ya TFF kila siku kucheza na ratiba kwa sababu wangejua kumbe hakuna kitu chochote kinachoharibika.

Ingefikia kipindi ratiba za mechi zingekuwa zinabadilishwa kiholela tu bila sababu za msingi. Mfano, ungekuta siku nyingine mechi ya timu A na timu B inaahirishwa/inasogezwa masaa mbele kwa sababu tu uwanja haujajaa kwa muda huo...au ungekuta siku nyingine watu na timu zipo uwanjani halafu mechi inasogezwa muda mbele ili kupisha tu hotuba au kikao cha watu fulani au labda mechi zingekuwa zinaahirishwa kwa sababu tu kuna dalili mvua itanyesha.

Kiufupi, ingefikia stage mechi zingekuwa zinasogezwa mbele kwa sababu zisizo na mashiko. Lakini leo Yanga wameonesha kuwa uswahili hautakiwi na hawajataka kabisa kulea tabia hii.

Ningewakosoa Yanga endapo tu sababu za kusogeza mechi mbele zingekuwa na mashiko lakini mpaka sasa sababu hazijawekwa wazi. Endapo kama sababu zingekuwa zimewekwa wazi na zina mashiko, hakuna mtu au timu ambayo ingekataa kucheza saa 1. Kutokuwekwa wazi kwa sababu za kusogeza mechi mbele inatufanya sisi tuamini kuwa sababu hazikuwa na mashiko ndio maana zimefichwa...ASANTENI YANGA.
Yanga vs Biashara ilkuwaje? Vipi na ile ya Yanga vs Azam?
 
Mkuu usiwe shabiki maandazi. Unapoona hili jambo halifai kwa maendeleo ya soka letu unatakiwa kukemea kwa nguvu zote, sio lila jambo unaleta ushabiki wa kipuuzi.
Yaani mechi kusogezwa mbele kwa masaa 2 ndio kunaathiri maendeleo ya soka?
 
Mechi ya Azam ilitolewa taarifa siku tano kabla ya mechi
Kulikuwa na taarifa mbili zilizotolewa kusogeza muda wa game ya uto na azam; ya kwanza ilikuwa hiyo iliyotoka siku 5 kabla ya mchezo, ilisogeza muda kutoka saa 10 jioni kwenda 1 usiku, ya pili ilitolewa siku ile ile ya mchezo ikisogeza muda kutokea saa 1 jioni kwenda 2 na robo usiku.
 
Tff wengi ni simba. Mganga wa Simba alitoa shariti mechi ichezwe kukiwa na giza. Huu mpango uliihusisha Simba moja kwa moja.
 
Mechi yenu na Azam mbona ilisogezwa imebaki lisaa moja Kuna tofauti gani na hii
Lete lalamiko lingine , angalia taarifa zimetolewa tarehe ngapi kwanza
IMG_20210508_222934.jpg
IMG_20210509_070537.jpg
 
Back
Top Bottom