Nasikia kuna uchawi wa kumfunga mtu asipate kazi ya kuajiriwa baada ya kumaliza chuo, wala riziki katika biashara yake, hili swala lina ukweli?

Inasemekana kuwa tanzania haina nafasi za ajira za kutosha za kuwaajiri wasomi wote wanaohitimu vyuo vikuu, ila cha kushangaza nilisoma baadhi ya thread humu, kuna watu wali-comment kuwa walikosa kazi baada ya ku-graduate chuo, ila baada ya wao kwenda kwa waganga na kuogea madawa waliopewa na waganga, baada ya mda mfupi sana walipata kazi ya kuajiriwa yenye mshahara mzuri..waganga waliwaambia hao watu kuwa walifungwa kichawi ili wasipate kazi, sasa sielewi ina maana wote waliokosa kazi miaka mingi baada ya kumaliza chuo wamelogwa?

Tufundishane dalili za kufungwa kichawi usipate riziki kwenye biashara yako /au usipate kazi ya kuajiriwa..na kama kuna watu waliokutana na hivi visanga m-share experience zenu humu
Dah msoto kitu kibaya yani ukute na we ni kati ya graduates waliokosa kuajiriwa sasa unatafuta kisngizio. Mkuu pambana maisha siyo kuajiriwa tu unaweza pambana ukatoka aisee Mungu hutenda kwa wakati wake tena ulio sahihi ila juhudi zako na maombi ndiyo muhimu.
 
KAJINI KA KUDATISHA WATU,NOMA SANA WANDUGU.
USIOMBEE,(UTAVUTISHWA MIBANGE WE NA KUNYWESHWA MIPOMBE BILA KUJITAMBUE MPAKA UCHOMOLEWE NA NDG MWENYE UPENDO WA KWELI)
 
Tuna jukumu kubwa mno la kuilemisha jamii kuhusu uchawi... Si kila kitu ni uchawi... Swala la ajira ni kilio cha dunia.. Dunia haina uwezo wa kutoa ajira kwa wasomi wake wanaohitimu kila mwaka
Huyo unayedhani anakuroga naye ni mtafutaji kapuku tu kama wewe.. Yaani aache ishu zake aende kukuroga.
Zinahitajika malighafi nyingi mpaka kumroga mtu
Kingine ni wahitimu wengi kuchagua kazi na mazoea ya kutaka kuajiriwa kuliko kujiajiri.. Lakini pia kuna watu wana connection na wengine huhonga... Sasa watu kama hawa hawawezi kukwambia ukweli
Kuhusu hili la kupata kazi mara baada ya kwenda kwa mganga ni imani tuu.. Ingekuwa waganga wa kienyeji wana uwezo wa kukufanya upate ajira kungekuwa hakuna haja ya kusoma

Jr

Kuna point umeingelea hapo kati naomba nisaidie kufahamu zaidi.

Kwamba “zinahitajika malighafi nyingi mchawi azipate ili kumroga mtu fulani na ili arogeke kisawasawa”.

Je ni malighafi gani hizo @ Mshana?

Awareness is empowering!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah msoto kitu kibaya yani ukute na we ni kati ya graduates waliokosa kuajiriwa sasa unatafuta kisngizio. Mkuu pambana maisha siyo kuajiriwa tu unaweza pambana ukatoka aisee Mungu hutenda kwa wakati wake tena ulio sahihi ila juhudi zako na maombi ndiyo muhimu.
Mkuu usimbeze kijana. Kuajiriwa ni haki yake, na kuwezeshwa kujiajiri ni haki yake pia.
Serikali yeyote iliyo makini moja ya mkakati wake wa msingi ni pamoja na hilo. Maana ukisema apambane na maisha bila kumuonyesha mpangilio, basi itakuwa bahati kama hataamua kufuata njia za kihalifu ambazo nazo pia sio za kubeza maana matajiri wengi zimewatoa na Leo wako nyumba za ibada na kutoa misaada kwa jamii.
Hivi kila wahitimu wa elimu za juu 50,000 kila mwaka wakaamua kujiajiri katika ujambazi baada ya muda mfupi hata Nigeria si tutawaacha mbali?
CCM waache kuwatumia vijana kwa maslahi yao bali wawatengenezee future yao, hilo ni bomu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiachana na uchawi ule wa zongo unaokaa machoni.. Huo mwingine lazima upate vitu visivyopungua vinne kisha uchanganye na madawa halafu ufanye manuizi
Kuna point umeingelea hapo kati naomba nisaidie kufahamu zaidi.

Kwamba “zinahitajika malighafi nyingi mchawi azipate ili kumroga mtu fulani na ili arogeke kisawasawa”.

Je ni malighafi gani hizo @ Mshana?

Awareness is empowering!


Sent using Jamii Forums mobile app

Jr
 
Mkuu usimbeze kijana. Kuajiriwa ni haki yake, na kuwezeshwa kujiajiri ni haki yake pia.
Serikali yeyote iliyo makini moja ya mkakati wake wa msingi ni pamoja na hilo. Maana ukisema apambane na maisha bila kumuonyesha mpangilio, basi itakuwa bahati kama hataamua kufuata njia za kihalifu ambazo nazo pia sio za kubeza maana matajiri wengi zimewatoa na Leo wako nyumba za ibada na kutoa misaada kwa jamii.
Hivi kila wahitimu wa elimu za juu 50,000 kila mwaka wakaamua kujiajiri katika ujambazi baada ya muda mfupi hata Nigeria si tutawaacha mbali?
CCM waache kuwatumia vijana kwa maslahi yao bali wawatengenezee future yao, hilo ni bomu

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeelewa nilichokiandika? Mimi nimemjibu kwa mtazamo wake wa uchawi hayo mengine ume assume wewe
 
Ukiachana na uchawi ule wa zongo unaokaa machoni.. Huo mwingine lazima upate vitu visivyopungua vinne kisha uchanganye na madawa halafu ufanye manuizi

Jr


Alaa kumbe?!

Kumbe haina haja ya kuogopa wachawi ambao wako mbali nasi au siyo.

Sasa naomba nisaidie kufahamu hivyo vitu visivyopungua 4 vinavyochanganywa na madawa na kufanya manuizi ili mtu arogeke


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inasemekana kuwa tanzania haina nafasi za ajira za kutosha za kuwaajiri wasomi wote wanaohitimu vyuo vikuu, ila cha kushangaza nilisoma baadhi ya thread humu, kuna watu wali-comment kuwa walikosa kazi baada ya ku-graduate chuo, ila baada ya wao kwenda kwa waganga na kuogea madawa waliopewa na waganga, baada ya mda mfupi sana walipata kazi ya kuajiriwa yenye mshahara mzuri..waganga waliwaambia hao watu kuwa walifungwa kichawi ili wasipate kazi, sasa sielewi ina maana wote waliokosa kazi miaka mingi baada ya kumaliza chuo wamelogwa?

Tufundishane dalili za kufungwa kichawi usipate riziki kwenye biashara yako /au usipate kazi ya kuajiriwa..na kama kuna watu waliokutana na hivi visanga m-share experience zenu humu
Hakuna mambo ya kichawi ni hali yenyewe tuu.Japokuwa kuna watu ambao tunaenda mwaka wa 7 bado wanasugua benchi na Digrii zao safi tu.
 
Kuna point umeingelea hapo kati naomba nisaidie kufahamu zaidi.

Kwamba “zinahitajika malighafi nyingi mchawi azipate ili kumroga mtu fulani na ili arogeke kisawasawa”.

Je ni malighafi gani hizo @ Mshana?

Awareness is empowering!


Sent using Jamii Forums mobile app
#Akilinjema uchawi jambo la kipuuzi sana na wala haliitaji malighafi nyingi vile udhaniavyo!,mfano,chukua jina lako halisi liandike kwenye karatasi nyeupe,chukua buibui mweuzi muweke hapo,andika namba 3,5,7 na 9,popote tu kwenye hiyo karatasi fungasha vyote vifunge pamoja kwa uzi mweusi,ichomeke kwenye papai kaizike makaburini uone utakavyopandishwa vyeo.
 
Inasemekana kuwa tanzania haina nafasi za ajira za kutosha za kuwaajiri wasomi wote wanaohitimu vyuo vikuu, ila cha kushangaza nilisoma baadhi ya thread humu, kuna watu wali-comment kuwa walikosa kazi baada ya ku-graduate chuo, ila baada ya wao kwenda kwa waganga na kuogea madawa waliopewa na waganga, baada ya mda mfupi sana walipata kazi ya kuajiriwa yenye mshahara mzuri..waganga waliwaambia hao watu kuwa walifungwa kichawi ili wasipate kazi, sasa sielewi ina maana wote waliokosa kazi miaka mingi baada ya kumaliza chuo wamelogwa?

Tufundishane dalili za kufungwa kichawi usipate riziki kwenye biashara yako /au usipate kazi ya kuajiriwa..na kama kuna watu waliokutana na hivi visanga m-share experience zenu humu
Mkuu inaonekana ww ni muhanga wa tatizo la ajira.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
#Akilinjema uchawi jambo la kipuuzi sana na wala haliitaji malighafi nyingi vile udhaniavyo!,mfano,chukua jina lako halisi liandike kwenye karatasi nyeupe,chukua buibui mweuzi muweke hapo,andika namba 3,5,7 na 9,popote tu kwenye hiyo karatasi fungasha vyote vifunge pamoja kwa uzi mweusi,ichomeke kwenye papai kaizike makaburini uone utakavyopandishwa vyeo.
Hii itanifaa mimi maana toka jiwe aingie sijawa promoted

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchawi wa kufungwa usipate kazi upo na dalili zake kama uchawi mwengine tu.Ila kuamini kuwa hujapata kazi sabab kuna mtu amekufanyiwa uchawi pia ni uchawi na utakua umejiroga mwenyewe. Nini cha kufanya? Usiende kwa waganga wala usiamini kuwa kutokupata kazi kwako sabab ni uchawi licha ya kuwa uchawi upo, bali kuwa patient, subir na endelea kupambana. Kinachowashinda wengi siku hizi ni subra (patience), muda mwengine mambo yanachelewa kutufikia ili tukiyapata tujue thamani yake.
Patience is most fitted.

Sent using Jamii Forums mobile app
👊👊👊👊 I second you!
 
Back
Top Bottom