Nashtuka sana nikipigiwa simu.

Nashtuka sana nikipigiwa simu.

Pressure kutoka kazini au nyumbani. Ungekuwa mtu wa rohoni ningekwambia unatakiwa kuomba kwa kunena kwa lugha kimoyomoyo hata ukiwa barabarani hiyo hali ingekata yenyewe lakini sijui imani yako.

Pili angalia kama unapata usingizi wa kutosha. kama pressure ya kazi ni kubwa chukua likizo
Kama unadaiwa mwambie mtu akushauri namna ya kudeal na huo mkopo
Nenda kapime afya hospital
Weka simu silent hau mlio usio na msisitizo au msukumo. Ukiweka mlio mlio wa kiong'ora cha police unategemea nini.

Mimi kuna ringtone au milio ya muzic ambayo way back miaka ya mwanzo kazini mabosi wangu waliokuwa wakinipigia enzi hizo nikisikia mlio fulani najua ni bos gani na tayari najua ni kuhusu report zimebuma yaani ni full panic na ukipokea simu jamaa hanyamazi anaongea nusu saa kwa kulalamika na kufoka hapo unakuta umekosea kitu kidogo kweli kumbe jamaa wengine wanaanzia mbali wanataka wakutoe kazini

Mpaka leo nikiisikia lazima moyo uende mbio kwa sekunde kadhaa japo nishaachana nao.

Kuna mmoja nilikuwa nimemuweka.... tone ya ndege kuita porini . Ikianza tu ....mama yangu najua tayari kimewaka.
 
Una negative attitude change hiyo kwanza.
Kama una dini jikite katika ibada na kuyasoma maneno ya dini yako na jitahidi uyaamini.
Pia waweza jaribu tajihudi,vile vile badili circle ya watu wako na matumizi ya muda wako.
Acha kuangalia movie za kutisha.
Asante kwa ushauri wako mkuu ntaufanyia kazi
 
Tatizo la kukosa hela hilo mkuu, jishughulishe kusaka hela ! Hela zinampa mtu Ujasiri
 
kikubwa ni hofu tu iliyo tokana na kupokea taarifa mbaya mfululizo kupitia simu.

itaisha taratibu kadri utakavyo pokea simu za kheri... mimi kuna watu wakinipigia hadi naona nataka kata roho (hawana kawaida ya kunipigia) yaani huwa nahis ni taarifa mbaya kumbe walaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom