Bi dentamol
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 1,038
- 2,189
- Thread starter
- #21
lady in action my dear, nahisi tangu naingia jf nakusoma unavyolia tu maskini. Ni yule yule mtu ambaye hadi alikutolea mahari nadhani au ni mwingine? Hujawahi kumove on?
Inawezekana sijawahi kupitia uliyoyapitia, but utaendelea kulia hadi lini, sema imetosha sasa. Huitaji kulia tena, unadeserve kuwa happy. Maisha yako lazima yaendelee no matter what. Mungu alikuleta duniani kwa ajili ya kusudi maalumu. Siku ya mwisho ikifika, Una kitu chochote cha kuangalia nyuma na kusema " Mungu Ahsante kwa maisha niliyoishi? Au unakipi cha kuwa proud nacho?
Kuna muda tutalalamika hadi tunamkufuru Mungu. Unaona kama kuachika ndo mwisho wa maisha yako. But trust me, nimekuja kujua hakuna kitu cha muhimu kama "Afya bora". Una Vitu vingi sana vya kuwa grateful navyo. Upo hai, una afya, una familia, una watu wanaokujali n.k. Hata siku moja hakuna siku utasema nina maisha perfect, but ukienjoy hata hivi unavyoviona ni vidogo kwako, basi maisha utayaona perfect. Usimtegemee binadamu mwingine kukupa furaha, Jipe furaha wewe mwenyewe. Maisha ni yako, hakuna mtu atakayeyaishi isipokuwa ni wewe mwenyewe. Kwa nini ujiharibie maisha yako?
Sema Mungu nakushukuru kwa maumivu niliyoyapata kwa mwanaume yule. Najua yule hakuwa wangu, ila alikuwa njia tu ya kunifikisha kwa mume uliyenipangia. Usichukulie Kila situation negatively, learn to have "the right perspective". Amini tu hakuwa wako, na Mungu alimuondoa kwako kwa kusudi maalumu kwa sababu alijua huko mbeleni angekukwamisha mahali.
Be grateful for every pain and experience. Anza mwanzo mpya, don't endure life, but rather learn to enjoy your life. Jione wewe una thamani, na lazima ufanye kitu kwa ajili ya maisha yako. Please Tafuta wanasaikolojia uongee nao, Usisahau na kuomba sana. Mungu atatenda kitu kwa ajili yako. Itafika siku utajicheka na kutamani hata kujipiga kofi ukikumbuka Ulivyokuwa unamlilia mtu asiye hata na habari na wewe. Hata ungekuwa mzuri kama malaika, alichokipanga Mungu kingetokea tu. My prayers are with you darlin
nimesoma ujumbe wako nimekikuta nalia tu bt namshukuru mungu kwan najua kaniandalia mtu sahihi..... ndo yule yule my ni mwaka na kitu sasa
Last edited by a moderator: