Wong Fei
JF-Expert Member
- Apr 13, 2016
- 5,509
- 7,263
Kitu kinaweza kuwa kilekile lakini kikabadilishwa maana. Shikamoo ni salamu anayopewa mtu anayekuzidi umri na haimanishi shikamoo ni utumwa. Vipi kuhusu kugonga, kugongewa, shoga, tigo? mbona hayajawekwa kwenye maana ya msingi? Na kwanini yamepewa maana ya ziada? Kasome kitabu cha Semantiki na Pragmatic utajifunza mengi kuhusu lugha ya KIswahili. Watu wengi hawajui Lugha ya Kiswahili ndiyo maana wanaona shikamoo ni utumwa.Shikamoo humaanisha hivi...nipo chini ya miguu yako, mimi si lolote kwako, sina thamani juu yako, nakutukuza, unachoagiza kwangu kutekeleza ni wajibu, mimi ni dhaifu kwako, ukitaka kunipiga nipige tu hata siwezi kujitetea kwako mkuu nk.
Kwa muktadha huu inabidi shikamoo ihifadhiwe maktaba ya Taifa.
