Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 949
- 2,865
Ndugu zangu Watanzania napendekeza Wazungu wagombee nafasi ya Urais ili watuletee maendeleo,tumeona katika shughuli za kimaendeleo tumewapa bandari ndugu zetu DP World,tumefanikiwa, Tanesco napo panasua sua tumwongezee DP World aweze kuleta Umeme wa uhakika wakikataa tuwaite tena Net Solution ili watuendeshee shirika letu la Umeme,bado tuna idara nyingi pia zimedorora kama idara za maji zote za mijini na vijijini nchi nzima kama nyongeza,baada ya hapo wapewe na hospitali/zahanati/vituo vya afya vyote nchi nzima kama bonus ila nimeona tunazunguka bure tufanye kama walivyofanya Zimbabwe,wamewaita tena Wazungu waje walime kwenye mashamba makubwa plantations maana Wazimbabwe hawawezi kulima,Wazungu wameitikia wito wamekuja na wameanza kulima, Zimbabwe imeanza kuwa ya kijani badala ya jangwa,kwa nini sisi Watanzania tusiwaite Wazungu waje wagombee urais na chawa wawapigie kampeni washinde urais na nchi yetu iongozwe tena na mzungu,tuanze kula nyama za kwenye kopo,tufufue kile kiwanda cha Tanganyika Packers, tufufue Ceramic kiwanda cha vyombo vya Udongo pale Morogoro,Tufufue viwanda vya nguo Polyester na Mwatex,Viwanda vya kutengeneza magari aina ya Nyumbu,viwanda vya kutengeneza viatu kama Moro Shoes,Wazungu walete ofisi zao kubwa kubwa za UN na NGO's makubwa tuongee kiingereza kama Kenya,hatutaongea kiswahili tutaongea kiingereza,mnaonaje Watanzania!?