Kim nana pakua elimu tuipate hapa jukwaaniMwanasaikolojia wa Kike anahitimisha kuwa wanawake wote wanapenda kufanya kazi chini ya uangalizi wa mwingine, wanapenda kufanya kazi katika vyeo vya kawaida sio kama bosi...
Wanawake wote wanapenda kuhisi kuwa uwepo wao unatambulika na kuhitajika
Anaendelea kuwa anaamini mahitaji Haya mawili ya kiroho yanatokana na ukweli kuwa wanawake wanaongozwa na MIHEMKO (EMOTIONS) wakati wanaume huongozwa na AKILI....
Mara nyingi inaonekana kwamba si kwamba wanawake sio wana akili sawa na wanaume, Bali wakati Fulani huwazidi wanaume
Udhaifu wao pekee ni kuwa wana JAZBA sana . Kufikiri kwa wanaume kunatekelezeka zaidi, wanahukumu vizuri zaidi, na wanaaaelekeza wengine ( ni wakurugenzi) vizuri zaidi
Ubora wa roho (AKILI) ya mwanaume kuizidi ya mwanamke ni kitu kilichopangwa na maumbile yenyewe....
Jitihada yoyote mwanamke atayofanya kubadilisha ukweli huu itakuwa ni KUJISUMBUA BUREE....
Wanawake lazima waukubali uhalisia kuwa wako vile kwa sababu WANA MIHEMUKO SANA NA WANAHITAJI USIMAMIZI WA MWANAUME katika maisha yao.
Lengo kubwa LA maisha ya KE ni KUJIHAKIKISHIA HATIMA YAKE YA BAADAE. na akishalipata huziambia kwa heri shughuli zake nyingine
Ni mwoga kufanya mambo ya hatari.
uoga ni hisia za moyoni, ili kuzishinda KE anahitaji msaada wa ME....Kazii zozote zinazohitaji kufikiri muda wote zinamchosha...
Shy land kula tution ya buree
Mie nitoe humoo, Mwanaume ndo kiongozi wa mwanamke. .
Huyu bado hujamwelewa hebu msome tena.
Hint: She is being sarcastic!
unajaribu kubishana na mungu.IQ ya mwanamke nu fupi kufanya maamuzi wala uongoziSijui nianze vipi, lakini kwa ufupi kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu sisi wanawake wa tanzania nasema kwa niaba ya wengi tumechoka na mfumo dume.
Kila mahali unaenda unakuta midume imejitutumuaaaaaa, mara miruzi fyuuuuuuuu, mara anti samahani oooooooh ~!@#@$%#@^#&$* tumechoka.Haya tuanze na majumbani mwetu, kila kitu kipaumbele anapewa mwanaume. Shule yeye, urithi yeye, nyumba yeye.
Tukija makazini hivyo hivyo, tunafanywa kama vitu, hupati kazi mpaka utangulize kitu.Jamani tumechoka.Tukija katika uchumi, tunadhalishwa sana na hatuthaminiwi juzi shangazi yangu karudi nyumani kakuta mjomba kauza mazao yote aliyolima.
Tumejaribu tumeshaweza kuwa na benki yetu, maana nyingine zimekuwa zikitunyanyapaa na hazijui mahitaji yetu. Kutokana na malaamiko yaliyomo vyuoni na sisi tunataka chuo chetu kikuuu tusinyanyaswe kijinsia na mijibaba mikware yenye kutoka udenda ionapo mwanamwali.
Bado kwenye nafasi za uongozi wa nchi hii tumesahauliwa tunadharauliwa sana. Yaani isingalikuwa wabunge wa viti maalimu, wabunge wanawake wangekuwa wa kuhesabu. Mwaka huu na sisi tunataka raisi mwamamke.
Historia ambayo imepindishwa pindishwa kuhusu uhuru wa nchi hii. Wanawake hawatajwi kabisaaaaa. Nauliza: Hivi ni wanaume peke yao ndio waliopigania uhuru wa nchi hii. Ni budi sasa iandikwe upya. Sisi tulishiriki kwa hali na mali zaidi, tena zaidi kupigania uhuru wa nchi hii, tulikuwa wahamasishaji wakubwa mikoani kuanzia Usangi mpaka Uyole. Mtwara mpaka Ngara. Kama si wanawake wa nchi hii usingepatikana. Toka uhuru tumekuwa tukipewa ahadi hewa, mnatutumia tu kushida huku mkituachia kanga, tishert , elfu kumikumi na sahani za wali miharagwe, lakini hamtekelezi madai yetu. Mwaka huu nasema hatukubali tena kutumiwa. PATACHIMBIKA
Kwa kumalizia ni haki katika nchi hii, sisi kinamama wa nchi hii mifumo ya mahakama imejaa mfumo dume tunaonewa mahakamani hatupati haki. Mahakimu wengi wanaume, wazee wamahakama wengi wanaume, majaji weeeeeeengi wanaume. Tena nauliza toka uhuru mpaka sasa mbona kumekuwa na wasomi wengi wanawake?, mbona hakuna jaji mkuu mwanamke. Ni wakati sasa na sisi wanawake tupate mahakama zetu. Mashauri yote ya yanayousisha wanawake yapelekwe kwenye mahakama zetu, natena nasema na sisi ni raia wa nchi hii.
ONYO :
​TUNAJUA TUNATAKA NINI KATIKA NCHI HII NA SISI NI WALIPA KODI PIA.
- WANAUME ACHENI WANAWAKE TUDAI HAKI ZETU.
- WANAUME ACHENI BUNGE NA SEREKALI WAFANYE KAZI ZAO PINDI WATAKAPOAMUA KUTEKELEZA MADAI YETU.NASEMA ACHENI KABISA
- MADAI YETU NI YAMSINGI OLE WAKE ATAKAYEYAPUUZIA NA KUKEBEHI
Tukiwezeshwa tunawezaaaaa
eti mamaafacebook yule spika mjengoni ana mume?