Wana MMU....
Kwa heshima na taadhima bila taraghani wala tahanani naomba mniweke kwenye sala zenu ili safari yangu iwe ya mafanikio.
Ni ombi la dhati kabisa na nawasihi msilichukulie kuwa takriri wala tashtiti za Ngabu.
Hii si mara yangu ya kwanza kujaribu bakhti yangu katika medani za wapendanao.
Miaka takriban hamstaashara ilopita nilijaribu lakini mambo yakaenda mramba.
Sasa napiga tena moyo konde nijaribu nione.
Naomba niwashirikishe kwa picha mtiririko wa safari yangu kuanzia Ubungo hadi Ikungulyabashashi....karibuni sana.
Safari ni hatua na yangu ilianza jana saa kumi na mbili asubuhi pale Ubungo....
View attachment 366753
Mishale ya saa tano hivi tukaigongea hodi Morogoro.....mimi huyo hapo naongea na mchepuko kwenye simu.
View attachment 366754
Shinyanga tukaingia usiku....nikalala hapo hapo stendi kwenye vibanda na asubuhi nikajidamka na kupanda Ally's hadi Ikungu....
View attachment 366755
View attachment 366756
Hatimaye majira ya alasiri nikakanyaga nyumbani Ikungulyabashashi...
View attachment 366758
Karibuni nyumbani. Karibuni sana. Na karibuni wanzuki.
Mlete town waje wakusaidie mjini kiongozi.
Bora ukomae na vicheche wwa mjini.
Hao mangumbaru wa kwenu wakijanjaruka utalia.
Yaani wewe jamaa wewe... salute, hiyo si ni stand ya zamani hapo Shy. Piga picha pande za Ikungulyababshashi naweza kuikumbuka pia.
Ni dalili nzuri za kutafuta mke toka usukumani maana hawa wengine ni vichomi.
..tena ukimpeleka huko USA ndio atakupa shinikizo la damu hadi usahaulike. Nakumbuka jamaa alienda US akaishi huko miaka kadhaa, baadae akaona arudi home kuoa. Alioa na kumpeleka mkewe US ili kuendelea na maisha, kumbe yule dada alikuwa na mtuwe huko.Huh!?!
Basi nimeghairi...acha nikimbizane tu na hawa akina Ralina wa mjini manake naweza kufa kwa shengesha na shinikizo bure!
ngabu on fleek you are amongest of my role models in jf much appreciation.cc usa baby
Hapo niaje.....unapatambua? Ni maeneo ya mnadani. Ila Wasukuma tuko washamba eeh heheeee
View attachment 366781
Downtown Ikungulyabashashi....cheki kikwangua anga hicho. Owner wake alikuwa Nyarugusu huko teh teh
View attachment 366788
Hiyo bodaboda ni yangu by the way....
And who's that. ....? (nanii)
I told you not to quote me coz I know it's going to infinity...
Kasie.
Mkuu wanzuki inangenezwaje kweli nisaidie maana ilikuwa kinywaji changu miaka ya 90 wakati nikiwa kanda hiyo.Wana MMU....
Kwa heshima na taadhima bila taraghani wala tahanani naomba mniweke kwenye sala zenu ili safari yangu iwe ya mafanikio.
Ni ombi la dhati kabisa na nawasihi msilichukulie kuwa takriri wala tashtiti za Ngabu.
Hii si mara yangu ya kwanza kujaribu bakhti yangu katika medani za wapendanao.
Miaka takriban hamstaashara ilopita nilijaribu lakini mambo yakaenda mramba.
Sasa napiga tena moyo konde nijaribu nione.
Naomba niwashirikishe kwa picha mtiririko wa safari yangu kuanzia Ubungo hadi Ikungulyabashashi....karibuni sana.
Safari ni hatua na yangu ilianza jana saa kumi na mbili asubuhi pale Ubungo....
View attachment 366753
Mishale ya saa tano hivi tukaigongea hodi Morogoro.....mimi huyo hapo naongea na mchepuko kwenye simu.
View attachment 366754
Shinyanga tukaingia usiku....nikalala hapo hapo stendi kwenye vibanda na asubuhi nikajidamka na kupanda Ally's hadi Ikungu....
View attachment 366755
View attachment 366756
Hatimaye majira ya alasiri nikakanyaga nyumbani Ikungulyabashashi...
View attachment 366758
Karibuni nyumbani. Karibuni sana. Na karibuni wanzuki.
DFPA ni plate # za miradi, hahahaa. Hii story ya si ya kuichukulia kibubusa. Bodaboda ya mradi....
Usisahau picha za kina Ngolo, Ng'washi, Kija, Minza, Nsamaka na Holo.
Sorry mkuu, hivi nawewe una asili ya Usukumani?Mhola gete....
bora uoe hamisi