Napitia katika changamoto kubwa

Napitia katika changamoto kubwa

Pole sana mpendwa usikate tamaa wakati wa Bwana ukifika atakupatia hitaji la moyo wako.
 
* MAMBO AMBAYO BINTI ANATAKIWA AYAEPUKE ILI KILA MWANAUME ATAMANI KUMUOA 🤭

Ujumbe huu ni muhimu sana kwako kwa unayopitia sasa!



Kabla sijaandika hayo mambo binti lazima ujue kwamba mwanaume kabla hajaamua kujilipua kwako anasoma hili andiko



*Mwenye busarahuyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia* .


Mithali 22:3


Mwanaume kabla hajafanya maamuzi ya kusema wewe unamfaa huchunguza mabaya yako .


Akiona unavituko anaweka alama







Maana yake hufai kuwa mkewe.




Sasa naomba tuangalie vijitabia ambavyo binti unatakiwa uviepuke kabisa ili uwe wa kuvutia kisura na kitabia pia .Huku ukichanua kama





Yaani rose flower kwa kila mwanaume anataka akuoe na inafikia hatua unashindwa kufanya maamuzi

Inabidi uingie rohoni kwenye






Maana yake kwenye maombi umwulize Mungu kati ya hawa wanaonijia yupi mume wangu sahihi


JAMBO LA KWANZA



Epuka kuwa mwongeaji saana .


Kuna mabinti akianza kuongea na mwanaume anaongea kama cherehani yaani hapumziki .

Mwanaume anawaogopa sana binti wa aina hiyo.

Umesemeshwa kidogo tuu , ukaanza Ooooh sijui imefika wapi na wapi , Mara Oooh fulaniii yupo hivii

Acha tabia hiyo .



JAMBO LA PILI





Epuka sana mazoea ya haraka .


Mara tu ukutanapo na huyo mwanaume usioneshe kumzoea sana na kuongea naye kana kwamba ni shemeji yako atakukimbia ‍♂‍♂‍♂‍♂



Wiki moja unaanza Oooh nimekumiss ,Oooh unamiradi gani , unabiashara gani , mara ooooh umekula nini

Acha ujinga


Usiharakie kumzoea sana



JAMBO LA TATU




Epuka kuwazoea marafiki wa yule mwanaume .


Kuna mabinti mara tu wakutanapo na marafiki za mwanaume tayari kanaanza kiherehere cha kujichekesha ovyo .


Yaani siku ya kwanza tu kanaomba namba za simu na za what's app .


Mwanaume akikuona tu na hiyo tabia anaweka alama







Yaani hufai kuolewa


Hata marafiki zake watamwambia ,

Aiseeee jamaa yetu huyu mwanamke hakufai yaani ni mapepe mmmmh mara hii tu katuzoea

Mpige chini , tafta mke anayejiheshimu .

JAMBO LA NNE





Epuka kuweka picha zako mtandaoni sana ukiwa na mapozi ya kihuni , mara umebinua midomo , mara umeonyesha maziwa



Akikuona huko unajipost ovyo na likes 500 plus 200 comments tena wengi ni wanaume

Hapo ujue unajikosesha mume


JAMBO LA TANO



Epuka saana uvaaji unaopingana na imani yako .


Suruali na Kaptura pamoja nguo za kukuchora na kuanika mwili wako na vingine vingi ambavyo vinadhalilisha mwili wa mwanamke .


Epuka hayo ili kila mwanaume akuonaye aseme huyu ndiye ............



JAMBO LA SITA



Jiepushe na marafiki wasio na ushuhuda mzuri



Mwisho wa kunukuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi ningepata majibu ya haya maswali ningejua wapi pakuanzia.

1. Muonekano wako upoje? Mwanaume yeyote humpenda mtu kwa muonekano tu na mengine hufuata, je unahisi upo vibaya sana kimuonekano ndio maana no one is considering you?

2. Ukikutana na watu huwa una waongelesha vipi? Cjajua njia sahihi ya kukuuliza hili swali lakini namaanisha kuwa ukikutana na mtu wa kiume huwa ukiongea nae unakuwa katika hali ipi? Yaani mkali, unapanic, sura inakuwa haivutii au unakuwa kawaida tu

3. Hivi huwa hautongozwi au unatongozwa na watu unaoona hawakufai?

4. Kuna vitu vidogo vidogo vinafukuza wanaume. Mfano ukiwa na Iphone 6s nakuendelea huwa tunaona ur so expensive we cant afford you, ukiwa mzuri saaaaana pia siyo rahisi kila mtu kukufuata coz tuna hisi tutapangwa,

Nijibu tu hizo swali zangu mama

Huwa natamani kusikia saut zenu watu kama nyie au hata niwaone sura nijue nini tatizo. Maana nahisi nikikuona tu mara moja nitagundua shida ipo wapi. Any way watu wakuzaa nao wapo kibao ila na wenyewe sijui huwa wanabagua wakuzaa nao ila humu wapo watakao kubali maana tiali wanakujua nini shida yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daahh! It's so sad Kwa mtu uliyejitunza namna hiyo kupitia changamoto hizo. Hata hivyo, Mungu ni mwaminifu sana. Naamini asbh yako inakuja, huna haja ya kukata tamaa. Mungu hatutendei tutakavyo sisi, bali jinsi yeye aonavyo vyema Kwa utukufu wake. Usijivunjie heshima Kwa namna yoyote, bali kuwa mvumilivu umsubiri Mungu atafanya. The only thing I can advise.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za Jumapili wanajamii.

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa. Napitia katika changamoto kubwa sana.

Hapo mwanzo kipindi ninasoma niliona si vyema kujiingiza katika mahusiano ya kufanya mapenzi kwani niliona yatanivuruga na ningejikuta napitia katika mahusiano mengi kitu ambacho sijawahi kukipanga maishani.

Nikamaliza chuo vizuri namshukuru Mungu.katika kutafuta ilikuwa ngumu kidogo nilitafuta mpaka nikakata tamaa nikaomba Mungu mpaka nikaona inatosha. Katikati ya kukata tamaa nikamuomba Mungu basi anipe kitu kimoja kwanza mme au kazi. Ila la kazi ndio nililoliwekea msisitizo kwani kwa kipindi hicho familia yangu ilikuwa inapitia changamoto nyingi kwa hiyo nikaona kazi itanisaidia kupunguza changamoto ama la basi niolewe ili nipunguze mzigo kwa familia yangu.

Siku isiyotarajiwa nikaitwa interview na nikapata kazi nzuri ambayo sikuwahi hata kufikiria wala kuiwaza. Nikashukuru Mungu na kuanza maisha mapya ya kazi na kusaidia familia yangu. Nikajikita kwenye kumuomba Mungu anijalie mme mwema atakayenifaa na kuongoza familia tutakayoipata katika misingi ya imani ta dini ya kikristo. Sikubagua kabila wala atakuwa mkirsto wa aina gani maadamu awe anaabudu jumapili maana mimi nilikuwa tiari kuhama katoliki ili tulee familia yetu tukiwa na muongozo wa dini moja.

Sikuwahi kudhani nitafikia huku maana mpaka sasa imekuwa ngumu kama ni Mungu hachelewi ama hawahi basi kwangu mimi kwa sasa imekuwa ni shida kubwa. Nimefunga novena nimesali sana mpaka naona nimeanza kuathirika na hili swala. Mwaka jana tarehe moja nikaona basi kama mme wangu hayupo nipate tu mwanamme nitakae zaa nae lakini awe mkirsto maana siko tiari kumtenga baba na mtoto wake hata kama hamhudumii, nikiamini kuwa uwezo wa kulea mwenyewe ninao hata kama watoto watakuwa zaidi ya mmoja niko tiari kupambana na maisha.

Nikaona kwa sababu nitakuwa pekeangu nikaanza kuwekeza ili watoto wangu wanikute nimejiandaa. Na penyewe Mungu akaona wakati wangu bado. Mwaka huu mwezi wa pili akatokea mme wa mtu kitu ambacho sijawahi hata fikiria kuwa kunasiku nitaangukia huko, Mwanzoni nilitaka tuzungumze mapema kabla hatujazoena sana matakwa yangu lakini akawa mtu wa kuona nampangia sheria mapema na kudai hizo mipango ninazotaka kupanga nae tukiwa hatujafika mbali ni mipango gani. Nikaona isiwe tabu.

Ikafika siku ya kukutana nikamwambia mimi sijawahi kabisa hakuamini na nikamwambia kama anajiamini aendelee ila ajue atakuwa na deni la kulipa, akatafakari akaona viatu ni vikubwa akaondoka.

Chenga zikaongezeka nikajiuliza ni nini shida, tukapanga tukutane ili tuone hatima ni nini kati yetu. Akaja na kudai yeye hayuko tiari kutoa bikira ya mtu asiye na mpango nae. nikamuelewa na nikaona yuko sahihi.Nikamuuliza wewe ulivyoanza ulitegemea mimi ni mti sina hisia za kufanya mapenzi akadai alijua anajihusisha na mapenzi ya kila mtu ana mtu wake hivyo wanakutana kulizishana tu. Akaniambia nahitaji nini hasa kwake nikamwambia kama ulishaona hisia zangu unadhani nahitaji nini? Niliona nisianze kutaja shida niliyonayo kwanza nimsikilize yeye ndio na mimi niseme ya kwangu. Yeye akadai aliona ni mahusiano ya kula na kuondoka. Akaniambia kama niko tiari ataweka sheria za kutuongoza za maandishi ili baadae tusijekupeana shida. Nikamwambia sheria zako utazoniwekea nitazifuata vilivyo japo najijua ninawivu lakini wewe ni mme wa mtu tiari nitavumilia.

Akaja na sheria na mipango mingi sana asee.sheria nyingi nilivyotafakari nikaona nyingi zinamlenga mtoto ambaye mimi ndio ninayemhitaji zaidi. na yeye akaona labda ni mmoja tu wakati mimi nishajipangia wakunitosha kabisa. Kwa maelezo yake nikaona hayuko tiari kuwa na mtoto nje ya familia na nikitokea kumpata basi nitoe mimba ama atamchukua. Nilichoka viungo vyote. Akaniuliza unalolote nikamwambia nizungumze nini wakati sheria zimekuwa ngumu.

Haki ya Mungu yaani natamani siku zirudi nyuma nizunguke na wanaume kama wafanyavyo wengine. Hukukujitunza kwangu kunanifanya nilie kila siku na kuomba Mungu usiku kucha kisa nilimtunzia mtu bikira. Jamii inayonizunguka itanitia wazimu maana swali la unaolewa lini limenichosha kabisa. Basi kama siolewi hata mtoto tu ni shida kumpata.

Kwasasa ninashida na mtoto kuliko maelezo na niendako nadhani nitawehuka. Msaada wenu tafadhalini sana.

NB. Hapo mwanzo nilifunga novena kwa muda wa mwaka mmoja na kuomba na kukabidhi mwili wangu uwe kwa ajili ya mtu mmoja tu ambaye ndio atakayekuwa mme au baba wa watoto wangu. Ndio maana inaniwia vigumu kuingia mahusiano mbalimbali.
Sipati picha hayo mabazazi yalivyojazana huko PM kwako yakipambana kupewa ruhusa ya kuivunja bikra yako!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usipanic life begins at 40 ukiacha desperation wako atakuja ila sasa hivi ikikurupuka utaumia atajitokea mhuni akulize. God's time is the best loh , hafu zawadi ya maisha ni muhimu kuliko huyo mume unayemlilia ukiona case za wanawake kuhangaika kuwatuliza waume kuanzia kanisani had kwa waganga ungetulia tu upate sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
Ungekuwa wewe ungeweza kuvumilia nyege miaka 30?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo inawezekana kwa muonekano wako Wa inje na imani yako hujui kujisitiri,yaani Wenda mavazi yako yanakufanya uonekane kama Malaya.Ukitaka kuolewa kwanza jua kujistiri,vaa nguo za heshima,na kuhusu kumtafuta mwanaume Wa kuzae naye utakuja jilaumu sana huko mbeleni
 
Habari za Jumapili wanajamii.

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa. Napitia katika changamoto kubwa sana.

Hapo mwanzo kipindi ninasoma niliona si vyema kujiingiza katika mahusiano ya kufanya mapenzi kwani niliona yatanivuruga na ningejikuta napitia katika mahusiano mengi kitu ambacho sijawahi kukipanga maishani.

Nikamaliza chuo vizuri namshukuru Mungu.katika kutafuta ilikuwa ngumu kidogo nilitafuta mpaka nikakata tamaa nikaomba Mungu mpaka nikaona inatosha. Katikati ya kukata tamaa nikamuomba Mungu basi anipe kitu kimoja kwanza mme au kazi. Ila la kazi ndio nililoliwekea msisitizo kwani kwa kipindi hicho familia yangu ilikuwa inapitia changamoto nyingi kwa hiyo nikaona kazi itanisaidia kupunguza changamoto ama la basi niolewe ili nipunguze mzigo kwa familia yangu.

Siku isiyotarajiwa nikaitwa interview na nikapata kazi nzuri ambayo sikuwahi hata kufikiria wala kuiwaza. Nikashukuru Mungu na kuanza maisha mapya ya kazi na kusaidia familia yangu. Nikajikita kwenye kumuomba Mungu anijalie mme mwema atakayenifaa na kuongoza familia tutakayoipata katika misingi ya imani ta dini ya kikristo. Sikubagua kabila wala atakuwa mkirsto wa aina gani maadamu awe anaabudu jumapili maana mimi nilikuwa tiari kuhama katoliki ili tulee familia yetu tukiwa na muongozo wa dini moja.

Sikuwahi kudhani nitafikia huku maana mpaka sasa imekuwa ngumu kama ni Mungu hachelewi ama hawahi basi kwangu mimi kwa sasa imekuwa ni shida kubwa. Nimefunga novena nimesali sana mpaka naona nimeanza kuathirika na hili swala. Mwaka jana tarehe moja nikaona basi kama mme wangu hayupo nipate tu mwanamme nitakae zaa nae lakini awe mkirsto maana siko tiari kumtenga baba na mtoto wake hata kama hamhudumii, nikiamini kuwa uwezo wa kulea mwenyewe ninao hata kama watoto watakuwa zaidi ya mmoja niko tiari kupambana na maisha.

Nikaona kwa sababu nitakuwa pekeangu nikaanza kuwekeza ili watoto wangu wanikute nimejiandaa. Na penyewe Mungu akaona wakati wangu bado. Mwaka huu mwezi wa pili akatokea mme wa mtu kitu ambacho sijawahi hata fikiria kuwa kunasiku nitaangukia huko, Mwanzoni nilitaka tuzungumze mapema kabla hatujazoena sana matakwa yangu lakini akawa mtu wa kuona nampangia sheria mapema na kudai hizo mipango ninazotaka kupanga nae tukiwa hatujafika mbali ni mipango gani. Nikaona isiwe tabu.

Ikafika siku ya kukutana nikamwambia mimi sijawahi kabisa hakuamini na nikamwambia kama anajiamini aendelee ila ajue atakuwa na deni la kulipa, akatafakari akaona viatu ni vikubwa akaondoka.

Chenga zikaongezeka nikajiuliza ni nini shida, tukapanga tukutane ili tuone hatima ni nini kati yetu. Akaja na kudai yeye hayuko tiari kutoa bikira ya mtu asiye na mpango nae. nikamuelewa na nikaona yuko sahihi.Nikamuuliza wewe ulivyoanza ulitegemea mimi ni mti sina hisia za kufanya mapenzi akadai alijua anajihusisha na mapenzi ya kila mtu ana mtu wake hivyo wanakutana kulizishana tu. Akaniambia nahitaji nini hasa kwake nikamwambia kama ulishaona hisia zangu unadhani nahitaji nini? Niliona nisianze kutaja shida niliyonayo kwanza nimsikilize yeye ndio na mimi niseme ya kwangu. Yeye akadai aliona ni mahusiano ya kula na kuondoka. Akaniambia kama niko tiari ataweka sheria za kutuongoza za maandishi ili baadae tusijekupeana shida. Nikamwambia sheria zako utazoniwekea nitazifuata vilivyo japo najijua ninawivu lakini wewe ni mme wa mtu tiari nitavumilia.

Akaja na sheria na mipango mingi sana asee.sheria nyingi nilivyotafakari nikaona nyingi zinamlenga mtoto ambaye mimi ndio ninayemhitaji zaidi. na yeye akaona labda ni mmoja tu wakati mimi nishajipangia wakunitosha kabisa. Kwa maelezo yake nikaona hayuko tiari kuwa na mtoto nje ya familia na nikitokea kumpata basi nitoe mimba ama atamchukua. Nilichoka viungo vyote. Akaniuliza unalolote nikamwambia nizungumze nini wakati sheria zimekuwa ngumu.

Haki ya Mungu yaani natamani siku zirudi nyuma nizunguke na wanaume kama wafanyavyo wengine. Hukukujitunza kwangu kunanifanya nilie kila siku na kuomba Mungu usiku kucha kisa nilimtunzia mtu bikira. Jamii inayonizunguka itanitia wazimu maana swali la unaolewa lini limenichosha kabisa. Basi kama siolewi hata mtoto tu ni shida kumpata.

Kwasasa ninashida na mtoto kuliko maelezo na niendako nadhani nitawehuka. Msaada wenu tafadhalini sana.

NB. Hapo mwanzo nilifunga novena kwa muda wa mwaka mmoja na kuomba na kukabidhi mwili wangu uwe kwa ajili ya mtu mmoja tu ambaye ndio atakayekuwa mme au baba wa watoto wangu. Ndio maana inaniwia vigumu kuingia mahusiano mbalimbali.
nina ugwadu sijabandua demu siku nyingi.
kama upo tayari njoo tuzungumze.
 
Sehemu pekee ulokosea ni hapo ulikoweka limitation ktk dini.....unapomuomba Mungu usiweke kiulizo chochote we pokea vile majibu yanakuja......angeweza kuja muislam na akawa ndo nwenye ulikuwa unamtaka.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dada angu hongera kwa kujitunza me nkushauri tu omba amani ya moyo na kila jambo lina mda na wakati wake Plz usipanic utapata familia bora kabisa Mungu hashindwi Dada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom