FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,776
Napinga ujengwaji wa barabara za juu au flyover Dar, badala yake hizo fedha zipelekwe kwanza Mikoani, Wilayani ambako hamna Barabara, kwa mfano kwenye kuunganisha Mikoa kwa Mikoa kama vile Tabora-Mbeya, Mtwara- Ruvuma, Kondoa-Handeni, Ifakara- Handeni-Lushoto, Arusha- Musoma n.k.
kwa kufanya hivyo kutawezesha pia Watu waishio mikoa mingine kujikomboa kiuchumi, Dar tayari tuko mbali sana kiuchumi ukilinganisha ni mikoa mingine, hivyo haileti maana kuendelea kuwekeza fedha zote hapa Dar!
Halafu isitoshe kabla hata ya kufikiri kujenga hizo flyover kwanza barabara za mitaani zote zijengwe na kupitika kama walivyofanya Barabara za oysterbay,Masaki, ambazo zimewaondelea foleni wakazi wa huko ingawaje uwiano wa watu wenye magali kwa wakazi wa huko ni mkubwa kuliko sehemu yoyote ile ya nchi yetu hivyo basi wajenge kwanza br pia sehemu kama za Sinza, Magomeni, Temeke, Vingunguti, n.k yaani flyover ziwe hatua ya mwisho kabisa.
Tumekosoma kupinga kwako lakini ningekushauri badala ya kupinga hapa JF uende mahakamani ukasimamishe ujenzi unaoendelea hivi sasa. Kama hujui njia za kwenda kufanya pingamizi mahakamani, mtafute mchungaji Mtikila akupe darsa, ana uzoefu mkubwa sana wa mambo ya mahakama na kesi baina yake na Serikali zingine kashinda zingine kashindwa mpaka kafungwa.
Kupinga hapa JF ni kama kumpigia mbuzi guitar hakuna anaeweza kukusaidia zaidi.