Napinga ujengaji flyover Dar

Napinga ujengaji flyover Dar

hata hiyo reli waliijenga dar kwanza!

SIO KWELI!

Reli ya Kwanza Nchini kwetu ilijengwa kutoka Tanga mpaka Moshi (KLM) na lengo lilikuwa ni kuifikisha mpaka Musoma, halafu ya Kutoka Dar Mpaka Tabora-Mwanza/Kigoma ikafwatia baadae, tena sana tu!
 

SIO KWELI!

Reli ya Kwanza Nchini kwetu ilijengwa kutoka Tanga mpaka Moshi (KLM) na lengo lilikuwa ni kuifikisha mpaka Musoma, halafu ya Kutoka Dar Mpaka Tabora-Mwanza/Kigoma ikafwatia baadae, tena sana tu!
Kumbuka miaka hiyo tanaga mzizima bagamoyo kilwa lindi ilihesabika kama jimbo moja tu!
 
Kumbuka miaka hiyo tanaga mzizima bagamoyo kilwa lindi ilihesabika kama jimbo moja tu!

Tena, SIO KWELI!

Mji wa Tanga ulijengwa na kuendelezwa na Wajerumani kama Bandari na lengo lilikuwa ni kuhudumia Mikoa ya Kaskazini yaani KLM,Arusha Mpaka Musoma/Mwanza yaani eneo la Ziwa Nyanza lote, na haukuhusiana na Bagamoyo au Dar kwa lolote lile, yaani Mtawala wa Tanga alikuwa ni mwingine na wa Dar alikuwa ni Mwingine ingawaje wote walikuwa chini ya Serikali moja!

Bagamoyo ndiyo ilikuwa Mji Mkuu wa kwanza wa Wajerumani lkn waliamua kuhamia Dar kwa ajili ya kujenga Bandari ambapo eneo la Dar kina chake chake ni cha asili ikilinganishwa na Bagamoyo ambapo ilikuwa ni lazima kuongeza kina!

Hivyo basi Reli ya ktk Dar kwenda Mrg-Do-TBR-Shy-Mwanza/Kigoma ilijengwa kwa ajili ya kuhudumia Eneo lote la Kati na Magharibi mwa nchi, na kulikuwa na mpango mwingie kama huyo pia wa kujenga Reli kutoka Mtwara (Bandari) mpaka Ziwa Nyasa ili kuunganisha Mikoa ya Kusini Magharibi kama Songea,Mbeya Iringa n.k na Bandari lkn haukukamilika kwa sababu ya Wazungu kuondoka nchini!

Hivyo utaona kwamba Ingawaje Dar ilikuwa ni Mji Mkuu lkn bado Miundo mbinu ya kwanza haikujengwa huko!
 
Kesi inarudi palepale lazima ujenge kwenye mlango wa nchi kwanza kabla huko uani kwa nchi!milango ya nchi ndio hiy Dar ,TAnga,BAgamoyo,Mtwara !sasa huko uani subirini kwanza tumalize flyover zetu!
 
Foleni inaweza kupungua bila ya kujenga flyovers (km mleta uzi alivyosema) kwa kujenga barabara zote za mitaani ili zipitike kiurahisi.
 
Northern bypass ukiingia mjini kama unatokea namboole stadium. Picha hizi hapa
fin001pix.jpg

images

images
Nashukuru mkuu nilikuwa sijapaona mahali hapa!
 
Hii ramani sikubalini nayo! Una maana ziwa Nyasa lote ni mali ya Malawi? Hebu kairekebishe kwanza kabla ya kuipost humu ndani.

naona hujui kusoma ramani!!!!!!
hapo hakuna mpaka mbona!.
 
'' Dar tayari tuko mbali sana kiuchumi ukilinganisha ni mikoa mingine ''

Acha masihara kijana......
 
naona hujui kusoma ramani!!!!!!
hapo hakuna mpaka mbona!.
Yawezekana kweli mimi sijui kusoma ramani na wewe ni msomi wa ramani zaidi yangu. Hebu nijuze basi mpaka wa Tanzania unaishia wapi katika hiyo ramani ilibandikwa.
 
Kwa mtazamo wangu hizo "flyover" hazitosaidia kivile. Tatizo la foleni Dar kweli ni sababu ya magari mengi na barabara chache, ila lazima tukubali MIPANGO ya kupunguza foleni imekuwa mibovu. Hivyo namuunga mkono mtoa thread. Pia kuna vibarabara "vidogo" vya nje kidogo ya Dar ila ni vya muhimu kweli, vingeboreshwa kwa kiwango cha lami. Mfano: barabara ya mlimani (chuoni) inayotokea Kimara Baruti, Kinyerezi road ingetakiwa ipanuliwe na itengenezwe lami mpaka Mbezi, kisha nyingine toka Kinyerezi ipite mpaka huko Pugu, chanika, mpaka mbagala, kongowe kisha Kigamboni. Yaani hizi ziwe barabara kubwa. Wenye magari wangekuwa na machaguo kadhaa ya kupita wanapoenda au kurudi makwao/ maofisini. Pia ingependeza kama mji mpya wa kisasa (maofisi), ungejengwa huko nje ya Dar mjini, yaani Kisarawe. Foleni zingepungua.


Kisarawe....Mkoa wa Pwani!!!!!
 
Yawezekana kweli mimi sijui kusoma ramani na wewe ni msomi wa ramani zaidi yangu. Hebu nijuze basi mpaka wa Tanzania unaishia wapi katika hiyo ramani ilibandikwa.
mbona nimesha sema katika ramani hiyo mpaka wa tz na malawi haujaoneshwa...
 
Back
Top Bottom