JOASH MUSSA
JF-Expert Member
- Oct 2, 2011
- 515
- 199
Napinga ujengwaji wa barabara za juu au flyover Dar, badala yake hizo fedha zipelekwe kwanza Mikoani, Wilayani ambako hamna Barabara, kwa mfano kwenye kuunganisha Mikoa kwa Mikoa kama vile Tabora-Mbeya, Mtwara- Ruvuma, Kondoa-Handeni, Ifakara- Handeni-Lushoto, Arusha- Musoma n.k.
kwa kufanya hivyo kutawezesha pia Watu waishio mikoa mingine kujikomboa kiuchumi, Dar tayari tuko mbali sana kiuchumi ukilinganisha ni mikoa mingine, hivyo haileti maana kuendelea kuwekeza fedha zote hapa Dar!
Halafu isitoshe kabla hata ya kufikiri kujenga hizo flyover kwanza barabara za mitaani zote zijengwe na kupitika kama walivyofanya Barabara za oysterbay,Masaki, ambazo zimewaondelea foleni wakazi wa huko ingawaje uwiano wa watu wenye magali kwa wakazi wa huko ni mkubwa kuliko sehemu yoyote ile ya nchi yetu hivyo basi wajenge kwanza br pia sehemu kama za Sinza, Magomeni, Temeke, Vingunguti, n.k yaani flyover ziwe hatua ya mwisho kabisa.
Mambo ya Kitaalamu, waachiwe wataalamu, hii ni sawa na wakati wa Nyerere ambapo alikuwa anafanya mambo ya ki taalamu bila utaalamu na hatimaye ilisababisha hasara kadhaa hata kupelekea uchumi wetu kuyumba, tusiendeshwe na mihemko, mtu unahemka unataka jambo flani liwe bila kuangalia faida na hasara zake
huko mikoni, inatakiwa yaboreshwe mashamba ili tukuze kilimo sababu tuna ardhi ya kutosha tena yenye rutuba