Napinga CWT kukusanya maoni ya walimu ya kuunda bodi ya walimu

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,486
Mimi kama mwalimu napinga kwa nguvu zote juu ya suala la chama cha walimu Tanzania, CWT kukusanya maoni ya walimu yanayotakiwa kutolewa kwa ajili ya uundaji wa bodi ya walimu. Zipo bodi mbalimbali za kitaaluma nchini, sidhani kama bodi hizo maoni ya wanataaluma hao yaliratibiwa na kukusanywa na vyama vyao vya wafanyakazi.

Msingi wa kupinga jambo hili ni mahusiano mabaya yaliyopo kati ya walimu na chama hiki ambacho kimekuwa kinafyeka 2% ya mishahara ya walimu, utapeli wa hisa wanazomiliki walimu katika benki inayodaiwa ni ya walimu pamoja na mambo mengine mengi ambayo yanajenga uadui kati ya walimu na chama hicho ambacho imefikia mahali hata viongozi wake wanaogopa kutembelea walimu mashuleni kufanya nao vikao kwa ajili ya mahusiano yao mabaya kwao.

Ni rai yangu kuwa suala la maoni ya kuundwa bodi ya walimu yafanywe na walimu wenyewe ili wawe huru kutoa na kuratibu maoni ya uundaji wa bodi itakayozingatia nidhamu ya kazi, maslahi kwa walimu, hadhi na heshima ya kazi ya ualimu, n.k


Screenshot_20210716-211637.jpg
 
Mimi kama mwalimu napinga kwa nguvu zote juu ya suala la chama cha walimu Tanzania, CWT kukusanya maoni ya walimu yanayotakiwa kutolewa kwa ajili ya uundaji wa bodi ya walimu. Zipo bodi mbalimbali za kitaaluma nchini, sidhani kama bodi hizo maoni ya wanataaluma hao yaliratibiwa na kukusanywa na vyama vyao vya wafanyakazi.

Msingi wa kupinga jambo hili ni mahusiano mabaya yaliyopo kati ya walimu na chama hiki ambacho kimekuwa kinafyeka 2% ya mishahara ya walimu, utapeli wa hisa wanazomiliki walimu katika benki inayodaiwa ni ya walimu pamoja na mambo mengine mengi ambayo yanajenga uadui kati ya walimu na chama hicho ambacho imefikia mahali hata viongozi wake wanaogopa kutembelea walimu mashuleni kufanya nao vikao kwa ajili ya mahusiano yao mabaya kwao.

Ni rai yangu kuwa suala la maoni ya kuundwa bodi ya walimu yafanywe na walimu wenyewe ili wawe huru kutoa na kuratibu maoni ya uundaji wa bodi itakayozingatia nidhamu ya kazi, maslahi kwa walimu, hadhi na heshima ya kazi ya ualimu, n.kView attachment 1856314
Hapa wanatumia akili kubwa kuwashikilia walimu ambao ndio wateja wao, maana kama board itaundwa simply CWT Haina nafasi. Na itakuwa inawarubuni Walimu huko.
 
Mimi kama mwalimu napinga kwa nguvu zote juu ya suala la chama cha walimu Tanzania, CWT kukusanya maoni ya walimu yanayotakiwa kutolewa kwa ajili ya uundaji wa bodi ya walimu. Zipo bodi mbalimbali za kitaaluma nchini, sidhani kama bodi hizo maoni ya wanataaluma hao yaliratibiwa na kukusanywa na vyama vyao vya wafanyakazi.

Msingi wa kupinga jambo hili ni mahusiano mabaya yaliyopo kati ya walimu na chama hiki ambacho kimekuwa kinafyeka 2% ya mishahara ya walimu, utapeli wa hisa wanazomiliki walimu katika benki inayodaiwa ni ya walimu pamoja na mambo mengine mengi ambayo yanajenga uadui kati ya walimu na chama hicho ambacho imefikia mahali hata viongozi wake wanaogopa kutembelea walimu mashuleni kufanya nao vikao kwa ajili ya mahusiano yao mabaya kwao.

Ni rai yangu kuwa suala la maoni ya kuundwa bodi ya walimu yafanywe na walimu wenyewe ili wawe huru kutoa na kuratibu maoni ya uundaji wa bodi itakayozingatia nidhamu ya kazi, maslahi kwa walimu, hadhi na heshima ya kazi ya ualimu, n.kView attachment 1856314
chama mfu
 
Kuanzisha bodi ya kitaaluma ya walimu is a total drunkardness in a straight forward language au bila kupepesa macho. Kwani kunahitajika professionalism gani ya kumfundisha mtoto a e i o u au 1+1 =2? My answer would be; a VERY basic level of professionalism. Hizi bodi zinatakikana kwenye fani zinazohitaji taaluma yenye ufanisi wa hali ya juu (high level of proficiency) kama engineering, medical, financial management to mention the few. But sio ualimu.
 
Hivi walimu mna matatizo gani?..taaluma karibia zote nchini na duniani zina mabaraza au bodi za kitaaluma..sasa nyie ambao mnazalisha wataalamu hamtaki kuwa na mabaraza ya kuthibiti taaluma..no wonder serikali inawapuuza mana hamjielewi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mimi kama mwalimu napinga kwa nguvu zote juu ya suala la chama cha walimu Tanzania, CWT kukusanya maoni ya walimu yanayotakiwa kutolewa kwa ajili ya uundaji wa bodi ya walimu. Zipo bodi mbalimbali za kitaaluma nchini, sidhani kama bodi hizo maoni ya wanataaluma hao yaliratibiwa na kukusanywa na vyama vyao vya wafanyakazi.

Msingi wa kupinga jambo hili ni mahusiano mabaya yaliyopo kati ya walimu na chama hiki ambacho kimekuwa kinafyeka 2% ya mishahara ya walimu, utapeli wa hisa wanazomiliki walimu katika benki inayodaiwa ni ya walimu pamoja na mambo mengine mengi ambayo yanajenga uadui kati ya walimu na chama hicho ambacho imefikia mahali hata viongozi wake wanaogopa kutembelea walimu mashuleni kufanya nao vikao kwa ajili ya mahusiano yao mabaya kwao.

Ni rai yangu kuwa suala la maoni ya kuundwa bodi ya walimu yafanywe na walimu wenyewe ili wawe huru kutoa na kuratibu maoni ya uundaji wa bodi itakayozingatia nidhamu ya kazi, maslahi kwa walimu, hadhi na heshima ya kazi ya ualimu, n.kView attachment 1856314
Ndugu Mwalimu CWT hawachukui maoni ili bodi iundwe, Serikali ishaunda Teachers Professional Board na sheria ya kuundwa kwake tayari imeshapitishwa bungeni. Ikatengeneza kanuni zitakazoongoza na ya uendeshaji wa hiyo bodi na wakazipeleka kwa kuwaita kuzijadili hizo kanuni, miongoni mwa wadau walioitwa ni cwt. Baada ya wadau kuzijadili wakaona hizo kanuni zina mapungufu makubwa hivyo makubaliano kati ya serikali na wadau wakiwemo cwt ni kupendekeza kanuni hizo ziweje na wapi wanaona kuna shida hivyo kuja na mapendekezo mapya ili serikali iweze nayo kupitia maoni ya wadau kama wataona inafaa au la!

Mambo ya msingi yanayolalamikiwa ni kama haya yafuatayo;
1.Ili uwe Mwalimu unatakiwa upate leseni ambayo utapeleka kwenye bodi, hii ni baada ya wewe kuhitimu taaluma ya ualimu kwa ngazi yeyote.

2.Mwalimu atatakiwa kulipa ada ya leseni sh 50000/= kila mwaka.

3.Unatakiwa kuhuisha leseni yako kila mwaka ili uendelee kuwa na sifa ya kuwa mwalimu.

4.Unatakiwa upate mafunzo ambayo yatakufanya uweze kuingia kwenye mtihani wa bodi ili ufaulu na kukidhi vigezo vya kupewa leseni. Kumbuka mafunzo haya yatagharamiwa na mwalimu mwenyewe kwa ada amabayo itadhibitiwa na bodi.

5 Utafanya mtihani usiopungua masaa 48.
Haya ni baadhi tu ya sehemu ya kanuni ambazo zitaongoza bodi ya kitaaluna ya waalimu. Kwahiyo mwalimu kama unaweza nenda moja kwa moja kwenye kamati ya bunge kujaribu kuboresha hizi kanuni.

Jambo lingine linalopigiwa kelele ni kwamba bodi hii imechukua kazi au majukumu ambayo yalikuwa yanafanywa na taasisi zingine kuwahusu waalimu kama vile TSC. Kwani ilivyo na majukumu ya bodi ni pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kinidhamu kwa mwalimu jambo ambalo linafanywa na TSC.
 
Jamani wataalaam wa Sheria is there a way we can petition and send NSSF Tanzania to international Court of Law or Tribunal at the Hague?

Please advise kwa sababu wabunge na wawakilishi wetu wamejitahidi kutosha.Bahati mbaya shirika linanufaisha mapapa wachache.
Wahanga njooni tupeane mwanga huenda tutakomboa kizazi chetu
 
Mambo ya msingi yanayolalamikiwa ni kama haya yafuatayo;
1.Ili uwe Mwalimu unatakiwa upate leseni ambayo utapeleka kwenye bodi, hii ni baada ya wewe kuhitimu taaluma ya ualimu kwa ngazi yeyote.

2.Mwalimu atatakiwa kulipa ada ya leseni sh 50000/= kila mwaka.

3.Unatakiwa kuhuisha leseni yako kila mwaka ili uendelee kuwa na sifa ya kuwa mwalimu.

4.Unatakiwa upate mafunzo ambayo yatakufanya uweze kuingia kwenye mtihani wa bodi ili ufaulu na kukidhi vigezo vya kupewa leseni. Kumbuka mafunzo haya yatagharamiwa na mwalimu mwenyewe kwa ada amabayo itadhibitiwa na bodi.

5 Utafanya mtihani usiopungua masaa 48.
Haya ni baadhi tu ya sehemu ya kanuni ambazo zitaongoza bodi ya kitaaluna ya waalimu. Kwahiyo mwalimu kama unaweza nenda moja kwa moja kwenye kamati ya bunge kujaribu kuboresha hizi kanuni.

Jambo lingine linalopigiwa kelele ni kwamba bodi hii imechukua kazi au majukumu ambayo yalikuwa yanafanywa na taasisi zingine kuwahusu waalimu kama vile TSC. Kwani ilivyo na majukumu ya bodi ni pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kinidhamu kwa mwalimu jambo ambalo linafanywa na TSC.

1.Kwani kupata lesseni ya kitaaluma mbona jambo la kawaida ktk fani zingine. Uliza wafamasia, manesi

2. Huitaji kwenda mafunzo ili kujibu mtihani wa kitaaluma, kama ulishasoma utapitia ulivyosoma na kama ni mzoefu vingi utaulizwa unavyovifanyia kazi.

3. 50,000 ada ya kuhuisha leseni bado ni rafiki sana ukilinganisha na kada zingine.
 
1.Kwani kupata lesseni ya kitaaluma mbona jambo la kawaida ktk fani zingine. Uliza wafamasia, manesi

2. Huitaji kwenda mafunzo ili kujibu mtihani wa kitaaluma, kama ulishasoma utapitia ulivyosoma na kama ni mzoefu vingi utaulizwa unavyovifanyia kazi.

3. 50,000 ada ya kuhuisha leseni bado ni rafiki sana ukilinganisha na kada zingine.
Leseni ni jambo la kawaida ni kweli kwani hata kada nyingi hufanya hivyo, lakini hapa tatizo linakuja pale unaposema hii leseni lazima uhuishe kila mwaka. Ukiwa na akili angalau ya upili utajua lengo hapa ni kukusanya pesa kila mwaka. Wangeweza weka interval angalau kila baada ya miaka mitatu.

Pia kanuni zinaelekeza kwamba lazima usome na ulipie mafunzo, si kwamba utajibu kwa kadiri ya wewe ulivyosoma, maana yake ni kwamba lazima ulipie mafunzo haya utake usitake ni kodi nyingine hii.
 
Ndugu Mwalimu CWT hawachukui maoni ili bodi iundwe, Serikali ishaunda Teachers Professional Board na sheria ya kuundwa kwake tayari imeshapitishwa bungeni. Ikatengeneza kanuni zitakazoongoza na ya uendeshaji wa hiyo bodi na wakazipeleka kwa kuwaita kuzijadili hizo kanuni, miongoni mwa wadau walioitwa ni cwt. Baada ya wadau kuzijadili wakaona hizo kanuni zina mapungufu makubwa hivyo makubaliano kati ya serikali na wadau wakiwemo cwt ni kupendekeza kanuni hizo ziweje na wapi wanaona kuna shida hivyo kuja na mapendekezo mapya ili serikali iweze nayo kupitia maoni ya wadau kama wataona inafaa au la!

Mambo ya msingi yanayolalamikiwa ni kama haya yafuatayo;
1.Ili uwe Mwalimu unatakiwa upate leseni ambayo utapeleka kwenye bodi, hii ni baada ya wewe kuhitimu taaluma ya ualimu kwa ngazi yeyote.

2.Mwalimu atatakiwa kulipa ada ya leseni sh 50000/= kila mwaka.

3.Unatakiwa kuhuisha leseni yako kila mwaka ili uendelee kuwa na sifa ya kuwa mwalimu.

4.Unatakiwa upate mafunzo ambayo yatakufanya uweze kuingia kwenye mtihani wa bodi ili ufaulu na kukidhi vigezo vya kupewa leseni. Kumbuka mafunzo haya yatagharamiwa na mwalimu mwenyewe kwa ada amabayo itadhibitiwa na bodi.

5 Utafanya mtihani usiopungua masaa 48.
Haya ni baadhi tu ya sehemu ya kanuni ambazo zitaongoza bodi ya kitaaluna ya waalimu. Kwahiyo mwalimu kama unaweza nenda moja kwa moja kwenye kamati ya bunge kujaribu kuboresha hizi kanuni.

Jambo lingine linalopigiwa kelele ni kwamba bodi hii imechukua kazi au majukumu ambayo yalikuwa yanafanywa na taasisi zingine kuwahusu waalimu kama vile TSC. Kwani ilivyo na majukumu ya bodi ni pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kinidhamu kwa mwalimu jambo ambalo linafanywa na TSC.
2.Mwalimu atatakiwa kulipa ada ya sh 58,000/= kila mwezi. Na CWT bila aibu
 
2.Mwalimu atatakiwa kulipa ada ya sh 58,000/= kila mwezi. Na CWT bila aibu
Nadhani watu tunatakiwa kujielimisha kuhusu tofauti ya chama cha wafanyakazi na bodi ya kitaaluma ya taaluma fulani.

Hapa utakatwa kote, chama cha wafanyakazi wanachukua tozo zao na kwenye bodi utalipa.
 
Back
Top Bottom