Napinga ACT-Wazalendo kushiriki kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) huko Zanzibar

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,677
218,188
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile.

Uchaguzi wa Zanzibar kama ulivyokuwa uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano ulighubikwa na uchafu wa kila aina , watu wamedhulumiwa ushindi , wametekwa , wameteswa na kuuawa, viongozi kadhaa wa ACT WAZALENDO akiwemo Maalim Seif, Ismail Jussa na Mazrui wamekamatwa na kuteswa vibaya sana, huku viongozi wengine kama Khamis Bakari wakifariki baada ya kujeruhiwa kwa risasi , nyumba kadhaa kisiwani Pemba zimeteketea kwa kupigwa mabomu huku vikongwe wakiumizwa bila hatia yoyote.

Walioyafanya haya wapo na wanafahamika na ndio hao hao wanaotaka ushirikiano kwenye serikali na ACT inakubali ? sababu ya kukubali ushirika huu ni zipi hasa? maana ukikubali ujinga huu ni kwamba umeyakubali mauaji ya wazanzibar na mateso yao kwamba yalikuwa halali , nani atakuamini tena?

Kwa vile mimi ni Mcha Mungu , Mpenda haki na mpinga uonevu , natangaza hadharani kupinga ACT kuingia kwenye SUK ili kujiepusha na dhambi ya kujitakia ya kushabikia mateso na mauaji ya kisiasa ya raia wasio na hatia yoyote , Nawatakia kila la heri na fanaka watakaoshiriki kwenye Uharamia huo

Mungu ibariki Zanzibar.

Nakala: Juma Duni Haji
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile...
Unajisi mtupu! Zto alitaka "kumpindua" Mbowe kwa kutaka madaraka-uenyekiti, hivyo kwa hili waliloliamua, sishangai katu!
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile...
Kamati kuu ya ACT imeamua, wewe unapinga kama nani?! Pambana na yanayoendelea kwenye chama chako.
 
Kwann hamtaki ushirikiano? Haiwezekani uchaguzi kurudiwa, haiwezekani TL kushinda, haiwezekani Mbowe kuwa waziri mkuu.

Inawezekana kushirikiana Mbowe, TL na ccm, kuhubiri TZ yenye amani huko duniani, kuvutia wawekezaji wapya, biashara, utalii,umoja wa kitaifa na mshikamano.
 
🤣🤣

Mkuu RBC...

Siasa ni tofauti na HARAKATI....

Japo ndani ya siasa pia kuna harakati ni zile za WEIGHING TOUGH DECISION MAKING.....while HARAKATI ni FIRM na haziyumbi....

ACT ni CUF ya zamani...

CUF ya zamani imelalamikia karibu chaguzi zote za Zanzibar....ya mwaka huu si MAPYA....

CUF ilipigika sana kuwa nje ya siasa za ZANZIBAR baada ya kuususa ule UCHAGUZI wa pili....

Wao wanaijua ZANZIBAR na siasa zake kuliko SISI....

Kama wazanzibari wengi walio NYUMA ya mh.Maalim Seif wangekuwa na UONI kama wako basi hakika HUU MSIMAMO WALIOUTOA UNGEBADILIKA....



Mbio za SIASA ni NDEFU MNO....
Wale wanaozifanya kuwa FUPI kwa "kuwahadaa baadhi ya wafuasi wao" wanatushangaza Sana....


USIKATE TAMAA KAMANDA HIZO NDIZO SIASA....
 
walichofanya ACT wananikumbusha enzi za shule, mnaazimia kwa pamoja kugoma bt badae wenzenu wanajitoa mnabaki kuzagaa tu, hapa naona ngoma nzito imebaki kwa chadema.
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile..
Unapinga wewe kama nani?
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile...
Kabla ya yote watuambie kwanza matokeo ya uchaguzi wameyatambua au vipi, na kwanini?
 
Hivi unajielewa ? ACT Wametoa Tamko tayari unapinga Nini? Wenye chama wameamua
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile...

Nakala : Juma Duni Haji
 
1456109.jpg
 
Wewe endelea kupinga wenzio wanajiunga na kupiga pesa. Shauri yako utapinga mpaka kesho uchaguzi uchaguzi uchaguzi wakati wenzio wanaujua ukweli na wanasonga mbele.

Siku nyingine utambue kuwa kupinga matokeo na kutokukubali kushindwa ni kuendelea kukiweka chama hai kwa kuwa wananchama wajinga wataendelea kuamini waliibiwa wakati ukweli upo wazi walishindwa
 
Focus ya Maalim siku zote ni Zanzibar. Mambo ya Bara huwa ni by the way kabisa kwao. Ni kweli kuwa Zitto kwa vyovyote atachafuka katika suala lote hili. Itabidi afanye kazi ya ziada kuwapa imani wapinzani wenzake makini bara. Hasa baada ya chama chake sasa kuwa chama kikuu cha upinzani Bungeni kama wale 19 wataonekana kuwa wamekosa sifa za kuwa wabunge.

Amandla...
 
Back
Top Bottom